Skip to main content

WANAWAKE WENYE TABIA HIZI WANANYEMELEWA NA SARATANI YA MATITI

 



HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@

SARATANI ya matiti (breast cancer) inaendelea kuwa miongoni mwa magonjwa yanayoongoza kwa kusababisha vifo vya wanawake duniani kote.

 

Hali hii ni ya kutia wasiwasi zaidi katika nchi zinazoendelea Tanzania ikiwemo, ambapo idadi kubwa ya wagonjwa hufika hospitalini wakiwa katika hatua za mwisho za ugonjwa huo.

 

 

Tafiti mbalimbali zinaonesha kuwa kuchelewa kupata huduma za uchunguzi na tiba kunachangia, kwa kiwango kikubwa vifo vinavyotokana na ugonjwa huu.

 

Takwimu za kimataifa za mwaka 2022 zilizotolewa na Global Cancer Observatory (GLOBOCAN), na ile ya wizara ya Afya ya mwaka 2024 zinaonyesha kuwa, saratani ya matiti ni ya pili kwa wanawake baada ya saratani ya shingo ya kizazi.

 

 

Takribani asilimia 14.4 ya wagonjwa wapya wa saratani nchini, ni wa saratani ya matiti, hali inayoifanya kuwa moja ya magonjwa yanayoongoza kusababisha vifo.

 

Shirika la Afya Duniani (WHO), linasema takribani wanawake milioni 2.3 waligundulika kuwa na saratani ya matiti mwaka 2020, na kati ya hao zaidi ya 685,000 walifariki dunia.

 

Hii inafanya saratani ya matiti kuwa aina ya saratani inayoathiri wanawake kwa kiwango kikubwa zaidi duniani.

Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI) Tanzania ya mwaka 2023, inaonesha kuwa zaidi ya wanawake 3,500 waligunduliwa na saratani hiyo.

 

Asilimia 70 ya wagonjwa hao walifika hospitalini wakiwa katika hatua ya tatu au ya nne ya ugonjwa, hatua ambazo nafasi ya kupona huwa ndogo.

 

WATAALAMU WA AFYA

Mratibu wa vituo vinavyotowa huduma ya kinga  Pemba, dk. Rahila  Salim Omar anasema wanawake wengi hufika hospitali wakiwa tayari katika hatua za juu za ugonjwa.

 



Anasema saratani ya matiti imeendelea kuwa miongoni mwa magonjwa yanayoongoza kusababisha vifo kwa wanawake duniani.

 

Na Zanzibar kama sehemu ya dunia na inayokaliwa na wanawake, wala haijasalia nyuma katika changamoto hiyo.

 

Anabainisha kuwa, ongezeko la visa vya ugonjwa huo linaashiria haja ya kuchukua hatua madhubuti za kinga, uchunguzi wa mapema, na elimu endelevu kwa jamii.

 

 Ongezeko hilo linahusishwa na mabadiliko ya maisha, lishe duni, na kuchelewa kufika hospitalini kwa uchunguzi.

Daktari wa masuala ya akina mama hospitali ya Chakechake Dk. Rahila Salim Omar anasema wanawake wasiopenda kunyonyesha wako hatarini kupata  saratani ya matiti.

Anaelezea kesi nyingi zinazoripotiwa ni hatua (stage) ya pili, jambo ambalo linachangia ugumu wa matibabu.

“Ni vyema unapojigunduwa na maumivu ya ziwa, maboje ukimbilie spitali kwani tatizo linapoonekana mapema hutibika,’’anafafanua.

Fatma Hassan Khamis msimamizi wa vituo vya huduma rafiki kwa vijana Pemba, anasema saratani ya matiti ni ugonjwa unaoweza kutibika endapo utagundulika mapema.

 

Huku akitaja changamoto ya uchelewaji wa huduma inayosababisha idadi kubwa ya vifo, inaweza kuzuilika.

 

“Ushirikiano kati ya serikali, sekta binafsi, mashirika ya kiraia, na jamii kwa ujumla, unahitajika ili kuweka mazingira bora ya uchunguzi,’’anasema.

 

 SABABU NA HATARI YA SARATANI
Shirika la Afya Duniani (WHO) mwaka 2023, lilianisha kuwa, moja ya sababu kuu za saratani ya matiti ni pamoja na urithi wa vinasaba.

 

Nyingine ni, matumizi ya homoni kwa muda mrefu, unene kupita kiasi, na mtindo wa maisha usiofaa.


Kadhalika, wanawake wanaopata hedhi mapema au kukoma hedhi kwa kuchelewa, kutonyonyesha, na kutumia pombe mara kwa mara, wako hatarini.

“Utafiti unaonesha wanawake wanaonyonyesha kwa muda mrefu, wanapunguza kwa kiwango kikubwa hatari ya kupata saratani ya matiti,” anafafanua dk. Hidaya Omar, mtaalamu wa afya ya jamii wizara ya Afya Zanzibar.

Daktari wa magonjwa ya wanawake katika Hospitali ya Abdalla Mzee Pemba Mohamed Omar, anashauri wanawake kuwa makini na mabadiliko yoyote katika matiti yao.

Akitaja mabadiliko hayo anasema ni pamoja na uvimbe usioumiza, ngozi kubadilika rangi, chuchu kutoa majimaji yasiyo ya kawaida na maumivu yasiyo ya kawaida.

“Dalili hizi hazimaanishi kila mara kuwa ni saratani, lakini ni muhimu kumuona daktari mapema,” anashauri.

 MASHUHUDA WA UGONJWA

Massoud Ali Massoud wa Chakechake anasema  sababu ya mama yake mzazi kuumwa na ziwa, hadi hatua ya kukatwa na kupoteza maisha ni kuchelewa kufanya vipimo.

 

“Naamini mama angewahi mapema kufika hospitali angepona talianza kuumwa mwaka 2005 hadi 2008, ndipo alipofanyiwa matibabu baada ya kugundulikana kuwa ana saratani ya matiti,”anambuka.

 Asha Mohamed Kombo wa Mkanyageni Mkoani, anasema baada ya kuona ziwa lake limefanya ugumu (maboje) kwa ndani na mtoto wake hataki kunyonya, aliwahi hospitali kwa uchunguzi.

 

“Kumbe ilikuwa ni saratani, ingawa nilikuwa na hofu baada ya kumsikia daktari kuwa awahiwe haraka isijeikafikia hatuwa ya kukatwa ziwa lote,’’anasema. 

Aziza Juma wa Machomane nae anasema, alifanyiwa upasuaji wa ziwa katika hospitali ya Chake chake, baada ya kuwa na boje, ingawa hakuwa na maumivu.

 Fatma Sharif wa Kengeja, anasimulia mwaka mmoja uliopita, aliumwa na ziwa ila hakukaa nyumbani, badala yake alikimbilia kupata matibabu.

 

Mume wa Fatma anasema, hajawahi kumsikia mke wake kulalamikia kuumwa na ziwa hapo kabla, ingawa mara tu baada ya kujifungua hali hiyo ikaanza kujitokeza.

Akisimulia hali iliyomfika mke wa rafiki yake Abdalla Saidi wa Wawi, baada ya kuumwa ziwa alifanya woga kukimbilia hospitali ziwa lilikatwa.

 JAMII INASEMAJE

Rehema Kassim wa Kiwani anasema aliwahi kusimuliwa na bibi yake mwaka 1998, kuwa mama asiponyonyesha mtoto wake inavyotakiwa ni rahisi kuumwa na ziwa.

 

Ali Juma anasema wanawake wengi huathiriwa na saratani ya matiti, ila huwa hawajui.

 

NINI KWANI SARATANI YA MATITI?

Ni mabadiliko ya chembechembe hai, zilizopo kwenye matiti, saratani hii kwa kawaida, haina dalili katika hatua ya mwanzo.

Uchunguzi wa awali ndio utakaowezesha kugundua ugonjwa, katika hatua ya mabadiliko yaletwayo na saratani.

Kuvimba katika titi au kwenye makwapa, mabadiliko ya umbo na ukubwa wa titi, kutokwa na majimaji au damu katika chuchu.

 

MAMBO YA KUZINGATIA WANAWAKE
Wanapaswa kuvunja ukimya, kuondoa aibu, na kuelimishana kuhusu umuhimu wa uchunguzi mapema.

Wanawake kuwa na utamaduni wa  kujikagua matiti kila mwezi, siku chache baada ya heidhi kumalizika, na kufika hospitalini mara, wanapobaini mabadiliko yoyote.

 

Jingine ni jamii kutokuwa na imani potofu ya kutumia dawa za kienyeji badala ya kwenda hospitali, ambako ndiko unakojulikana tatizo na hatimae kupata matibabu.

MIKAKATI YA SERIKALI NA WADAU
Wizara ya Afya, imeanzisha programu maalum za uchunguzi wa saratani za wanawake, ikiwemo kampeni ya “Afya ya Mama, Tumaini la Taifa”.

Kampeni hizi, zinayolenga kuwafikia wanawake katika shehia zote za Unguja na Pemba na popote walipo.

Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui anasema, serikali imeimarisha vifaa vya uchunguzi wa saratani, katika hospitali za Mnazi Mmoja kwa Unguja na Abdalla Mzee Pemba.

Jingine ni kutoa mafunzo kwa wauguzi na madaktari, kuhusu utambuzi wa mapema.

 “Tunasisitiza wanawake wajitokeze kufanya uchunguzi wa matiti, angalau mara moja kila mwaka,’’anasisitiza.

Mashirika kama Zanzibar Cancer Foundation (ZCF) na Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), yanaendelea kutoa elimu na huduma za uchunguzi, bila malipo katika kampeni za kijamii.

Na hili hasa wakati wa mwezi wa Oktoba wa uhamasishaji wa saratani ya matiti duniani (Breast Cancer Awareness Month).

WHO, linaripoti kuwa, zaidi ya asilimia 90 ya wagonjwa wanaopatikana katika hatua za mwanzo, hupata nafuu kamili baada ya matibabu.

MWISHO

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...