Skip to main content

VYAMA KUKOSA WAKALIMANI, VIZIWI ZAWAPITA UPANDE SERA, AHADI ZA WAGOMBEA

 



NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@

VYAMA vya siasa vitambue kuwa kuna watu wenye ulemavu wa uziwi na wana haki ya kusikiliza kampezni zao.

Kuna baadhi ya vyama havijazingatia mahitaji ya watu wenye ulemavu, hasa wale wenye uziwi, katika mikutano.

Jambo ambalo linalowanyima haki yao ya msingi ya kufatilia sera za vyama, ili siku ya kupiga kura wafanye uamuzi sahihi.    

Vipo vyama 17 vilivyosimamisha wagombea na 11 vimefanikiwa kusimamia wagombea urais, ingawa ni chama cha mapinduzi CCM pekee ndio kinachotekeleza ushirikishwaji wa watu wenye ulemavu wa uziwi.

Imefahamika vyama vyengine vimekuwa vikiendesha kampeni zao bila ya kuwashirikisha watu wenye ulemavu wa uziwi, kwa kukosekana kwa wakalimani wa lugha za alama.

Tena zipo asasi za kiraia kadhaa ikiwemo ile ya wanawake wenye ulemavu Zanzibar (JUWAUZA), Jumuiya ya Mazingira, Jinsia na Utetezi Pemba (PEGAO), Jumuiya ya Wanasheria wanawake  Zanzibar (ZAFELA) na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA-Zanzibar, zimekuwa zikipigia kelele na kutetea  haki za watu wenye ulemavu.



Hapa Kaimu Mratibu wa TAMWA-Ofisi ya Pemba Amina Ahmed, anasema hasa kundi la viziwi wamekuwa wakikosa sera za vyama, kwa kukosekana wakalimani.

‘’Ni kweli tumekuwa tukipiga kelele kila uchao, ili kuona wakati huu vyama vikinadi sera, zinakuwa sera jumuishi kwa wenzetu hawa,’’anasema.

Anasema wamekuwa wakitoa mafunzo kwa waandishi wa habari ili kuteteta haki za watu wenye ulemavu.

Kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) watu wenye ulemavu wapatao 8,021 wanatarajiwa kushiriki katika uchaguzi mkuu mwaka huu Zanzibar.

Mkurugenzi wa uchaguzi Idarous Faina anafafanua kua, kati ya hao wapo viziwi 1,667 wenye ulemavu wa ngozi wakifikia 102 na wasioona 678.



Mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu wa mwaka 2006 (CRPD), ibara ya 29 (a), inazitaka nchi wanachama, kuhakikisha kuwa, watu wenye ulemavu wanashiriki kikamilifu katika medani ya siasa.

Ukataba ukafafanua kuwa, tena iwe kwa misingi iliyo sawa na wingine, ikiwa ni pamoja na fursa ya kuchangua na kuchaguliwa.

‘’Watu wenye ulemavu, wanatakiwa kuwekewa mazingira sahihi ikiwemo kupata taarifa, ili kushiriki kikamilifu katika masuala ya umma bila ya ubaguzi wowte,’’umefafanua mkataba huo.

Sheria ya watu wenye ulemavu Zanzibar nambari 8 ya mwaka 2022, kifungu chake cha 29 kinaeleza umuhimu wa watu wenye ulemavu kuweza kufikia miundo mbinu mbali mbali pamoja, taarifa mawasiliano na haki zote za kibinaadamu za msingi.

Ikifafanua kuwa, suala la kuwepo kwa wakalimani kumbe kwa mujibu wa kifungu hicho na kile cha 28 (1)(d), kinachofafanua suala la kupata taarifa, ni jambo la lazima kwao.

Ndani ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kifungu cha 11 na 12, kikabainisha kuwa, usawa kwa binaadamu wote mbele ya sheria, binaadamu wote huzaliwa kupata uhuru, anastashiki heshima ya kutambuliwa kuthaminiwa utu wake wanayo haki bila ya ubaguzi wowote.

Hata kile cha 18, kinasisitiza haki ya kupokea, kutoa na maoni ni haki ya kikatiba, ingawa haikuwataja watu wenye ulemavu, ikijumuisha raia wote.

Taarifa ya fedha ya mwaka 2022/2023 ya Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, ilishirikiana na Madrasa Early Childhood Program, kuendesha mafunzo kwa viongozi kadhaa wakiwemo Makatibu wakuu, Maafisa Wadhamini, ili kuwajengea uwezo, wajibu wa kuwajali watu wenye ulemavu.

VIZIWI WENYE WANASEMAJE

Adinani Khamis Juma ni mlemavu wa uziwi akizungumza chini ya mkalimani wake, anasema vyama vya siasa, bado havijawashirikisha kusikiliza sera zao, wakati huu wa kampeni.



Anasema kwa kupewa ukalimani tu, anaona gari za matangaazao ya kampeni, ingawa baadae hajui nini kinaendelea.

 ‘’Kwa kweli mimi kupitia rangi za chama tu, ndio huwa najua kuwa kile ni ACT, CCM, AAFP, ADA TADEA au Chaumma, lakini sisikii sera na ahadai zao,’’analalamika.

Yumma Mohamed Mbarouk, anasema hata wakati mwingine hajui mikutano hiyo ya kampeni inafanyika wapi, hushuhudia foleni na gari na pikipiki tu.

Anasema, vyama vimewasahau kuwa nao, wanahitaji kusikia sera na ahadi, ili ikifika Oktoba 29, mwaka huu wafanye uamuzi sahihi.

Mohamed Khamis wa Wawi, anasema sikio lake ni kuwepo mkalimani wa lugha ya alamam, ili awafafanulie, ingawa hilo halipo.

Zaina Mohamed Ali, anasema vyama vya siasa vimekuwa viwaacha nyuma, na kuzisahau sheria, mikataba na katiba kwamba wanahaki sawa ya kupata taarifa kwa aina ya ulemavu wao.

‘’Wakati mwingine nakwenda kwenye mikutano mtupu na narudi sikuvuna jambo, kubwa nashuhudia wasanii tu,’’analalamika.

‘’Tunaathirika hatupati sera za vyama isapasavyo, labda kwa chama nnachokipenda ndio naweza kubagua kwa rangi tu,’’ anasema.

Mwalimu wa mkalimani wa lungha za alama Asha Issa Mohamed, anasema Chama cha Mapinduzi pekee, ndio kinachozingatia na kuwashirikisha watu wenye ulemavu wa uziwi.

‘’Wamekuwa wakituarifu na kutaka taratibu za kupatikana kwa mkalimani, na wale wenzetu ambao ni viziwi na ni CCM, hupata taarifa na sera za chama chao,’’anasema.

WANAJAMI

Fatma Ali Hamad, jamii anaeshiriki kwenye kampeni za vyama vya siasa, anasema watu wenye ulemavu wa uziwi, bado hawajazingatiwa mahitaji yao, katika kufikiwa na sera za vyama.



Issa Haji Mohamed, asema inawezekana vyama havihitaji kura za viziwi ndio maana, vimekuwa vizito kuwawekea mkalimani kwenye mikutano.

Mwanaisha Hassan Khamis, anasema sheria na mikataba hazijawasahau watu wa kundi hilo, ingawa baadhi ya vyama bado ni changamoto.

VYAMA VYA SIASA VINAJIBU NINI

Katibu wa CCM mkoa wa kusini Pemba Kajore Vyohoroko, anasema wamekuwa wakiwatumia wakalamani hasa wanapokuwa na wagombea ngazi ya urais, kusudi viziwi wapate sera.

Maana Katiba ya chama hicho, ya mwaka 1977 toleo la 2007, linaeleza kua CCM, kinaamini kwamba watu wote ni sawa.

Mwenyekiti wa chama cha ACT –Wazalendo Mkoa wa kusini Pemba Mohamed Abdallah anasema, hutumia watu wa karibu na viziwi, katika kufikisha ujumbe uliokusudiwa.

Anasema kuwa, bado chama kinaupungufu wa wataalamu wa lugha ya alama, hivyo inawawia vigumu kupata wataalamu wa kutosha wa kuwatumia katika mikutano yao.



‘’Tutafanya jitihada zetu ipasavyo kuhakikisha kundi hilo muhimu linapata ujumbe unaokusudiwa,’’ anasema.

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Alliance Afrika Farmers Party (AAFP) Omar Juma Said, anasema bado wako nyuma hawajapata muamko na elimu ya kuwafikia watu wenye ulemavu wa uziwi.

Anasema anajua kuwa, watu wenye ulemavu wana haki za msingi ya kuchagua, kusikiliza pamoja na kupata taarifa, ingawa kwa sasa suala la kuwapatia taarifa halijafanyika.

‘’Ni kweli watu wenye ulemavu wa uziwi hatujawashirikisha katika kusikiliza ilani ya chama chetu, mikutano yote tuloifanya hapakuwa na mkalimani wa lugha za alama,’’ anakiri.

Chausiku Khatib Mohammed ni Mgombea mwenza wa Urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzani kwa tiketi ya NLD, anakiri kuwa, hawajawashirikisha na wamesahau kama kuna watu wenye ulemavu wa uziwi.

 ‘’Kwa sisi tumesahau kabisa, kama kuna watu wenye ulemavu wa uziwi, mpaka sasa hatujawashirikisha juu ya kusikiliza ilani ya  sera za chama chetu, na kura zao tunazihitaji,’’anafafanua.

Asha Said Suleiman ni Mgombea Uwakilishi  wa  Jimbo la Mtambile Chama cha ADA-TADEA anasema, hawajawashirikisha watu wenye ulemavu katika kunadi sera zao.



Anasema hata kama wamepewa mafunzo na TAMWA juu ya ushirikishwaji wa watu wenye ulemavu, ingawa, hushindwa kwa gharama ya mkalimani.

‘’Mkakati wetu ni kupita nyumba kwa nyumba, kutangaza sera ya ilani ya chama chetu, kwa kila mwenye ulemavu wa uziwi, ili wasaidizi wao waweze kuwasaidia,’’anasema.



TUME YA HAKI ZA BINAADAMU NA UTAWALA BORA

Suleiman Salim Ahmad ni Afisa Mfawidh Tume ya haki za binaadamu na utawala bora Pemba, anasema ni kweli tume imegundua pengo lipo hasa katika mikutano ya hadhara.

Anasema wamekuwa wakitoa mafunzo kwa vyombo vya habari, ili kupeleka ujumbe juu ya haki za binadamu kwa kufanya makala vipindi na hata habari.

BARAZA LA WATU WENYE ULEMAVU

Mratibu wa barazala la Taifa la watu wenye ulemavu Pemba Mashavu Juma Mabrouk anasema wamekuwa wakinasihisha vyama vya siasa kwenye vyombo vya habari ili kuandaliwa mazingira rafiki kwa watu wenye ulemavu.

‘’Tumekuwa tukitetea haki za watu wenye ulemavu kupitia vyombo vya habari juu ya mchakato wa kampeni unaondelea kuwekwa wakalimani wa lugha za alama,’’ anasema.



JUMUIYA ZA WATU WENYE ULEMAVU

Maryam Mohamed Salum ni Afisa watu wenye ulemavu Pemba, anasema wamekuwa wakihamasisha sana serikali, tasisi na mashirika kuwa kila kitu washirikishwe watu wenye ulemavu.

Anasema ni CCM pekee, tena kwa mikutano ya ngazi ya urais, watu wao wenye uziwi, hunufanika na kinachozungumzwa.

                   MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...