Skip to main content

50 KWA 50 YAWATIA JOTO WANAUME KWENYE SAFU YA UONGOZI

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@

MATAIFA kadhaa ulimwengini, Tanzania ikiwemo zimeridhia mikataba na matamko ya usawa wa kijinsia na uwezeshaji wanawake kwenye uongozi.

 

Hii ni kama ilielezwa katika tamko maarufu la la Haki za Binadamu la mwaka 1948.

 

Zanzibar imesaini mikataba ya kikanda na kimataifa, lakini safari ya utekelezaji ni ndefu kwa sababu hadhi sawa  kwa wanawake na wanaunme katika uongoz.

 

Mara nyingi unapofanyika uteuzi nafasi wanazopewa wanawake huwa hazina hadhi sawa na zile wanazokabidhiwa wanaume.

 

Vyama vya siasa navyo vinawaacha nyuma wanawake katika kuwapa nafasi za kugombea kama, inavofanyika kwa wanaume na jina la mwanamke likipita huwa kama bahati mbaya.

 

 Taarifa ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC, inafafanua kuwa, kwa uchaguzi wa 2020, wanaume walioteuliwa na vyama kugombea kuingia katika Baraza la Wawakilishi walikua 190 na walioshinda ni 42 wakati wanawake walikuwa  61 na walioshinda ni wanane (8).

 

Taarifa za Shirika la Wanawake la Umoja wa Mataifa (UN Women) na Umoja wa Mabunge (IPU) za 2017 zimeonesha kuwepo ongezeko dogo la viongozi wanawake katika serikali na mabunge.

 

Maana katika majimbo 50 ua uchaguzi ya Zanzibar, wanawake katika baraza la kutunga sheria, wanane hii ni saw ana asilimia16, wabunge ni  wannne kwa asilimia 8, mawaziri ni sita sawa na asilimia 33 na Makatibu Wakuu ni saba sawa na asilimia 39.

 


Kati ya wakuu wa mikoa watano Zanzibar, wanawake ni wawili, huku wakuu wa wilaya 11, wanawake wakiwa watatu pekee, ambapo na masheha wanawake ni 81 kati ya 388.

 

KATIBA/SERA/MATAMKO

 Katiba ya Zanzibar ya 1984, kwenye kifungu cha 11 na cha 14, vimeweka wazi kuwa kila mzanzibari anayo haki na uhuru wa kushiriki kwa ukamilifu katika kufikia uamuzi juu ya mambo yanayomuhusu.

 

 Aidha Dira ya Zanzibar ya 2050 imeelezea jinsi gani masuala ya usawa wa jinsia juu ya kuondoa unyanyasaji na kuimarisha mifumo ya uwezeshaji wanawake.

 

Sera ya jinsia inaeleza ushiriki wa wanawake katika vyombo vya utoaji maamuzi, katika ngazi zote ni mdogo na kwa hivyo serikali, kwa kushirikiana na wadau wengine, itafanya juhudi kuona makundi yote na yaliyopembezoni.

Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika SADC)  ambayo mkataba wake ulitiwa saini mwaka 2008 inaeleza, kutaka kuondoa utafauti na kuwatenga wanawake katika nyanja mbalimbali za maendeleo na kusaidia kuwepo usawa wa kijinsia katika nchi wanachama na kufikia asilimia 50/50 kwenye  maamuzi.

 

Makubaliano yanayojulikana kama ‘Itifaki ya Maputo’ ambayo yalifanyika Msumbiji mwaka 2003, inacho kipengele kinachoonyesha haki ya wanawake, kushiriki katika siasa na  mchakato wa vyombo vya kutoa maamuzi.

 


Mkataba wa kimataifa wa kutokomeza aina zote za ubaguzi, (CEDAW) wa mwaka 1979 ambao unapinga aina zote za udhalilishaji na kusisitiza, ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi.

 

Ibara 12,  inasisitiza ushiriki sawa wanawake na wanaume kufikia asilimia 50/50 kwenye nyanja za maamuzi, serikalini na taasisi binafsi.

 

Aidha jukwaa la Mpango wa Utekelezaji wa Beijing mwaka 1995, ibara ya 7 kinataka ushiriki katika vyombo vya maamuzi kwa kuzingatia uwiano wa kijinsia kwenye ngazi zote za uongozi.

 

VYAMA VYA SIASA

  Anaewania nafasi ya uwakilishi wa Jimbo la Chambani Pemba, Bahati Khamis Kombo, ansema hali sio mbaya kwa viongozi wa chama chake cha CCM na serikali katika kuteua wanawake kuwa viongozi.

 

Anasema wanaume waliogombea wakilishi walikuwa 190 na walioshinda 42 na wanawake waliojitokeza walikuwa 61 na walioshinda ni wanane na kwahivyo  haja kwa wanawake kujiandaa vyema kwa uchaguzi zijazo.

 

Mwakilishi wa Wete Harusi Said Suleiman, anasema sera ya CCM na katiba yake, zinazingatia jinsia na muda chama kinahamasisha wanawake kugombea uongozi kwa nafasi mbali mbali.

 

Mwenyekiti wa mstaafu wa ACT Wazalendo, Juma Duni Haji, anasema chama hicho kinafuata sheria na mikataba iliyoridhiwa na kusistiza hakina mfumo dume.

 

Anasema kinapenda mno kuona wanawake wanashika nafasi kubwa ndani ya chama, na mfano wa uchaguzi wa 2025, walimteua Fatma Abdull-habibu Fereji, kuwa Mgombea mwenza wa Jamhuri ya Muungano.

 


‘’Ingawa yalioyotokea mmeyasikia, baada ya kuenguliwa lakini kama engepata kuendelea mgombea wetu Mpina na kushinda mwanamke engekuwa Makamu wa rais,’’anasema.

 

Naibu Mkurugenzi kutoka ADC, Mtumwa Faiz Sadik, anasema ili kuzipatia ufumbuzi changamoto wanazopitia wanawake,  ni lazima kuwepo mipango mizuri ya kutekeleza mikataba na maazimio ya kimataifa.

 

Mchakato wa kuwania uongozi kwa uchaguzi wa mwaka 2025 kwenye majimbo wanawake walihamasika na kufikia takriban 400  kutoka katika  vyama  vya siasa na hasa CCM, CHADEMA,  NCCR mageuzi, na ACT Wazalendo.

 

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Zanzibar, Abeda Rashid anasema, licha ya changamoto ziliopo, wanawake wamenufaika na fursa za uongozi ndani na nje ya vyama vya siasa.

 

Kwa mara ya kwanza nafasi ya Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo kuongozwa na yeye akiwa mwanamke mwenye ulemavu, kama ilivyo kwa Mhandisi Zena Ahmed Said, kushina nafasi ya Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi.

 

TAKWIMU ZA UCHAGUZI 2020 ULIOPITA 

Inafahamika kuwa, walioteuliwa na vyama kugombea ubunge kwa upande wa Zanzibar ni wanaume ni 257 na walioshinda 46 na wanawake walikua 81na walioshinda wanne.

 

Ujumbe wa baraza la Wawakilishi, walioteuliwa wanaume 190 na walioshinda 42, ambapo wanawake walikuwa 61 na walioshinda ni wanane.

 

Upande wa nafasi ya udiwani, ripoti hiyo ya ZEC inaeleza kuwa, wanaume ni 276 na walioshinda 85 ambapo wanawake walikua 74 na walioshinda ni 25.

 

NINI ATHARI YAKE

Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, anasema kwanza ni kukosa mtetezi, kwenye mausla yanayahusu wanawake, mfano huduma za mama na mtoto.

 

Asha Said Suleiman, mgombea uwakilishi Jimbo la Mtambile kwa tiketi ya ADC, anasema, kuendelea kuwekwa mkiani, kwenye utoaji maamuzi.

 

Hidaya Majaka Ali, mwenye ulemavu wa viungo, anasema kubwa ni kuendelea kuishi kwenye dimbwi la kufanyiwa kila kitu na wanaume, hata pake pasipohotajika.

 

NINI KIFANYIKE.

Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali, anasema moja ni waandishi wa habari, kuendelea kupaza sauti zao.

 

Mwakilishi msataafu wa Jimbo la Konde anawania tena nafasi hiyo, Zawadi Amour Nassor, anasema vyama viendelea kuwaamini wanawake katika uongozi.

Mwanamke aliyegombea Uwakilishi wa Jimbo la Kojani, Katija Ali Mbarouk, anasema wanaume wafundwe kuwa, majimbo hayana hatimiliki na wao.

 

 

Hata hivyo Dk. Nkya alishauri wanawake  kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa mwaka 203o na sio kusubiri nafasi za uteuzi au viti maalum.

 

 

        mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...