Skip to main content

KATIJA MWENYE ULEMAVU WA VIUNGO, AWATIA HOFU WANAUME, ASEMA 2030 'HAIISHI MPAKA IISHE'

 

 NA ARAFA MAKAME, PEMBA@@@@

HAPA ni Kiuyu Minyungwini, wilaya ni ya Wete, mkoa wa kaskazini Pemba, na mbele yangu namuomba mjasiriamali, bila shaka ni mtu mwenye ulemavu wa viungo.

 

Niliharakia, kutaka kumjua ni nani, nilipomkaribia ana nadisha haya kangaa…kangaaa…na wale wa wapenzi wa madira na vipodozi nipooo.... njooo ujichagulie.

 

Kauli hizo, zilinifanya nisimame pembeni kidogo mwa nyumba ya Asha Haji Makame wa Kiuyu, nae mjasiriamali huyo, aligeuka nyuma ghafla, kwa hamu ya kutafuta wateja na alinifuata.

 

…..assalama alyekum, baada ya kuitikia mjasiriamali huyo, alimuuliza bi Asha kua amepata mgeni, na kumjibu ni mgeni wako.

 

‘’Au ndio huyo mwandishi wa habari aliyenipigia simu, juzi kuniambia anakuja, nilijua utachelewa kidogo ndio maana, nimeanza kutembeza biashara yangu,’’alisema.

 

‘’Kwani wewe ndio Katija Mbarouk Ali, nilikua nawasiliana na wewe bila ya kukufahamu, ndio  nimekuja kukuhoji,’’alidakiza mwandishi.

 

Ghafla, baada ya kutua mzigo wa kanga, madira na vipodozi, kumbe anapokaa Katija ni nyumba moja tu, na kumvuta mwandishi pembezoni.

 

MAZUNGUMZO

‘’Mimi ndie Katija Mbarouk Ali, nilienza kuipenda siasa tokea, mwaka 2016, kwa hamu tu ya kutaka kuwatetea wenzangu.

 


Akamueleza mwandishi wa kua, safari yake ya siasa iling’oa nanga miaka tisa iliyopita, baada ya hamu yake ya kutaka kutimiza ndoto za kuwahudumia wanawake na watu wenye ulemavu.

 

‘’Ni kweli mwandishi huu ulemavu wangu sikutaka kuufanya mtaji, wa kuwaomba omba, mtegemezi wa familia na kuonekana mazigo,’’anasema.

 

Katija ni mchesi, mchangamfu na mwenye ulemavu wa viungo, ni mweusi wa wastani, na uso wake saa 24 huwa ni wenye bashasha.

 

Hadi sasa anaamini, iko siku atakuwa mtetezi wa kweli kwa wanawake, jamii na kundi la wenzake wenye ulemavu, akiwa ndani ya chombo cha kutunga sheria.

 

Kumbe anaumia ndani ya moyo, kuona kundi la wanawake na watu wenye ulemavu, kudhalilika kwa kukosa mitaji ya kujiendesha.

 

‘’Unajua mwandishi, mimi na uongozi, mimi na sisasa sasa ni watoto pacha, na tunaorithi pamoja, na sifanyi haya kwa ajili ya tumbo langu, lahashaa,’’anasimulia.

 

KATIJA NA UONGOZI

Kumbe, baada ya kuiva akitokea mjumbe wa mkutano wa wadi wa tawi la Kiuyu Minungwini, sasa ikwa ni mwendo wa kugombea.

 

Maana kuanzia mwaka 2017 hadi 2019, aliwahi kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa tawi la CCM Kiuyu Minungwini, inagawa kwa mshangao alikabidhiwa nafasi ya ujumbe.

 


‘’Hapo nilianza kuulizwa maswali, na wasionitakia mema wala chama changu, eti wapi na wapi mlemavu kugombea,’’walihoji watu.

 

Katija, ambae familia inamuita shujaa asiyekumbuka kovu za kukatishwa tamaa, kudharauliwa, aligombea tena nafasi ya Mwenyekiti wa tawi.

 

‘’Mara iliyofuata mwaka 2017, niligombea Mwenyekiti tena wa tawi la CCM Kiuyu Minguwini, ingawa nilipewa nafasi zile tano za kupitia wilaya,’’anasema.

 

Walishasema wahenga kuwa, zimwi likujualo halikuli likakumaliza, ndivyo ulivyosadifu msemo huu kwa shujaa Katija.

 

Ilipofika mwaka 2020, aliibuka tena kiana na kumuliika bahati yake kwenye viti maalum, tena kwa watu wenye ulemavu.

 

‘’Hapa tulikuwa wanawake wanne (4), ingawa pia haikuwa bahati yangu, lakini sikununa wala sikumlau mtu,’’anasema.

 

Maisha ya Katija na kuusaka uongozi, ili kuwatumikia wananchi, uliamka tena mwaka 2025.

 

Si unajua kwa anapoishi Katija, jimbo lake ni Kojani, hapo dada huyo alijichanga kwa miaka mitano, na kufundika shilingi 500,000 kibindoni.

 

Anamueleza mwandishi wa makala, kuwa, siku ilipofika aliianga familia yake, na kutaka dua na ridhaa hadi wilaya ya Wete, yalipo makao makuu ya CCM.

 

‘’Nilizitoa shilingi 500,000 kuchukua fomu ya kugombea Uwakilishi wa Jimbo la Kojani, huku nikiangalia huruma za wajumbe,’’anasema.

 

Hapa alipambana na watia nia 23, wakiwemo wanawake wanne, ingawa mwenye ulemavu alikuwa peke yake.

 

Kwa hakika, msuguano wa kukutana na wajumbe, kwa Katija hakukutana nao, akiamini kama sehemu ya njama ya kumkosesha nafasi.

 

Aliona madudu kadhaa, kuanzia kwa wanachama wa kawaida, wagombea wenzake na watu wingine wa karibu, wakiashiria maumivu kwake.

 


‘’Wapo walioniita mlemvau sio kiongozi, mbona umeacha nafasi za watu wenye ulemavu umekuja jimboni, pesa zako hazina kazi,’’nadio maneno aliyokumbana nayo.

 

Anasema akikumbuka tokea, alipokuwa akiomba nafasi za kugombea Mwenyekiti wa tawi, zaidi ya miaka 10 na haya ya mwaka 2025, hakutetereka.

 

‘’Unajua ukishatafunwa na simba, mbwa, kima, paka na kuku, huwa ni jambo la kawaida,’’anasema.

 

Kwenye kinyang’anyiro hicho, mtia nia Katija, alifanikiwa kupenya, kuanzia ngazi ya jimbo, wilaya, mkoa na taifa.

 

‘’Kama binaadamu na mwanamke mwenye ulemavu, kwa hakika nafasi ya uwakilishi wa Jimbo la Kojani, nilishaanza kuifikiria,’’anasema.

 

‘’Siogopi kupambana na wanaume kwenye kupiga kura, naopa kwenye riadha, kuvuta kamba, kutupa mkuki ama kucheza mpira, kwa sababu ya ulemavu wangu tu,’’anasema.

 

Kumbe jasiri huyo anaetamani kuingia tena jimboni mwaka 2030, kwa nafasi ya ubunge, anachojenga hofu ni kubezwa na kudhalilishwa kwa maneno.

 

Mana anasema, baada ya watia 23, na kisha vikao vya chama taifa kuwarejesha saba, na akiwa mwanamke pekee, anasema huo ulikuwa mtihani kwa wajumbe.

 

‘’Tunasema kila siku mwanamke mbele na hasa mwenye ulemavu, lakini duuuu….wajumbe hawakuliona hilo na leo hii sikufanikiwa kuwa mwakilishi mteule Kojani,’’anasema.

 

AKIWA NJE YA SIASA

Katija, ni mjasiriamali wa kutembeza bidhaa kama kanga, madira na manukato mingine katika shehia ya Kiuyu Minungwini na vijiji jirani.

 


Anasema, hapendi hata kidogo kuonekana mzingo kwa wazazi wake, ingawa hajabahatika ndoa, lakini ndio msaada mkubwa kwa familia yake kwa sasa.

 

Alishaanzisha vikundi kadhaa vya wajasiriamali vya watu wenye ulemavu, ingawa bado hajafanikiwa kutoboa kimaisha.

 

‘’Unajua, katika kutafuta fursa, inafika wakati nasema kama vile kushirikiana na watu, ni mbaya maana nia zetu hazifanani,’’anasema.

 

Kumbe anakumbuka machungu, baada ya kuwezeshwa kwa cherhani zaidi ya sita, na aliyekuwa Mwakilishi wa watu wenye ulemavu Raya Suleiman, ingawa kwa utunzaji mbovu wamerudi tena kwenye umaskini.

 

Anasema, kama wengikuwa na moyo unaofanana na tamaa ya kutafuta maisha, leo hii wengekusha kuwa wameshaajiri wenzao.

  



 FAMILIA YA KATIJA

Mwanache Mkadamu Juma ni mama mzazi wa Katija, anasema juhudi za kutafuta fursa za uongozi kwa mtoo wake, zimezungurukwa na changamoto za kiroho.

 

‘’Hata mimi hufuatwa na kupewa lugha za kumvunja moyo, mara…..ooooni mlemavu, mara oooo…ataka poteza pesa zake,’’anaelezea anavyovunjwa moyo mtoto wake.

 

Anasema, anapokaa au wakati mwingine kusikilzia redio, hulalamika na kuguna, jinsi wanawake na watu wenye ulemavu, wanavyoishi kwenye changamoto za kimaisha.

 

‘’Utaskia, nikipata nafasi ya kuwa Mwakilishi wa jimbo au viti maalum, ntahakikisha napunguza changamoto za watu wenye ulemavu,’’anasema.

 

Fatma Mbarouk Ali ni ndugu wa Katija, anasema dada yake, anasema bado hapati usingizi wa fofo, hasa anapoona watu wenye ulemavu wanadhalilishwa.

 

Ukikakaa nae hadithi zake ni kuwasaidia wanawake, watu wenye ulemavu na wale maskini, akisema kuwa, inawezekanaje mtoto kushindwa kwenda skuli, kwa kukosa kiti mwendo.

 

Anasema, wakati mwingine anaporudi kwenye mikutano, huandika orodha ya watu wenye ulemavu, ukimuuliza, anasema ana mpango mkakati.

 

CCM JIMBO LA KOJANI 

Tamimu Omar ni Katibu wa CCM jimbo la Kojani, anasema, juhudi za kumuunga mkono na kumpa moyo, zinafanyika kila wakati.

 

‘’Kwa mfano, tunamuelekeza njia za kufanya, ili afanikiwe, na kwa hakika ni mwanachama anayepitia changamoto na hasa akionesha nia tu ya kugombea,’’anasema.

 

Hilo anasema huchangiwa na mambo kadhaa, maana Katija ni kijana wa misimamo, hayumbishwi na visenti na ana maadili ya kijamii na kichama.

 

Akigusia juu ya watu wenye ulemavu, anasema CCM katika kuwajali, imeanzisha viti maalum, kwa ajili yao.

 

‘’Fursa iliyopo, anaweza kugombea, jimbo, vitu vyao maalum au nafasi ya wanawake au nafasi ya vijana, hayo ndio mahaba ya CCM kwa makundi ya jamii,’’anafafanua.

 

 

WANAHARAKATI

Hidaya Mjaka Ali ni Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wenye Ulemavu Zanzibar ‘JUWAUZA’, anasema bado watu wenye ulemavu wanakabiliwa na vikwazo kadhaa ushiriki katika uongozi.

 

Anasema, jamii haijawaamini hata chembe, kama wanaweza kuwa watetezi wao, maana kama hivyo sivyo, Katija kwa mwaka huu engefanikiwa.

 

Amina Ahmed Mohamed ni Kaimu Mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania- TAMWA Zanzibar ofisi ya Pemba, anasema kazi yao ni kuwawezesha wanawake kugombea.

 

Kwa mfano tulikuwa na mradi maalum wa kuwawezesha kushika nafasi, na huyo Katija alikuwa mshiriki, lakini bado jamii haijawaamini.

 

‘’Na tulianzisha kamati maalum na wanaume wa mabadiliko, na ilipita vijijini na vitongoji vyote vya Pemba, lakini bado mfupa ni mgumu,’’anasema.

 

Kwenye majimbo ambayo tulitarajia CCM wengemsimamisha mwanake mwenye ulemavu kwa nafasi ya Uwakilishi, tulihisi ni Kojani, lakini imekuwa tofauti.

 

Ijapokuwa wapo wanawake kadhaa kwa sasa waliopitishwa na vyama vyao kugombea nafasi za majimbo kama Wawi, Chake chake, Chambani, Wete, Konde, Gando bado takwimu ni ndogo.

 

‘’Maana Pemba, tu tunayomajimbo 18, ambapo ni sawa na wagombea 36, kwa kila jimbo kwa nafasi ya ubunge na uwakilishi, takwimu bado haziridhishi kwa wanawake,’’anasema.

 

 

Ijapokuwa taarifa za Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC, imabainisha, kuwa, wapo wapiga kura wenye ulemavu mchanganyiko 8,021 bado wanaowania majimbo hawajapewa kipaumbele.

 

JAMII NA WAPIGA KURA

Omar Haji Msanifu wa Kojani, anasema ngarambe ya kulipata jimbo, bado mazingira yanatawaliwa na mambo kadhaa, ikiwemo rushwa na umaarufu.

 

Mwanaisha Hilali Khamis, anasema wanawake wenyewe, hutengenezwa kuwa maadui kwa wanawake wenzao, na kusabisha ugumu kufingia jimboni.

 

NYARAKA ZINASEMA JE HAKI YA KISIASA

Hadithi ya kusikitisha ya Katija, haibebwi na Sheria ya watu wenye Ulemavu nambari 8 ya mwaka 2022, maana kifungu cha 28 (1) (e) chenyewe kimetamka haki ya kushiriki, katika shughuli za kijamii, ikiwemo siasa.

 

Hata Mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu mwaka 2006, Ibara ya 29 (b) (i), kwamba watu wenye ulemavu, wana haki ya kujumuishwa kisiasa.

 

‘’Kushiriki katika asasi za kiraia na zile zinazojihusisha na masuala ya umma na siasa za nchi, na katika shughuli na uongozi wa vyama vya siasa, ni haki kwa watu wenye ulemavu,’’umefafanua mkataba.

 

Mkataba wa kimataifa wa haki za kiraia na kisiasa wa mwaka 1976, ukitaja moja ya haki za kila mmoja ni kushiriki, siasa bila ya ubaguzi.

 

Tena hata mkataba wa kimataifa wa kutokomeza aina zote za ubaguzi dhidi ya wanawake ‘CEDW’ wa mwaka 1979, ukasisitiza  Ibara ya 7, kwamba lazima hatua zichukuliwe, kuhakikisha wanawake wanakuwa na ushiriki sawa kwenye ulingo wa siasa.

 

Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kifungu cha 21(1), kinasisitiza kuwa, watu wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki bila ya ubaguzi, kupata haki mbele ya sheria.

 

Katija Mbarouk Ali, ambae hayuko kwenye ndoa ni mkaazi wa shehia ya Kiuyu Minungwini yenye wakaazi 60,23 wanaume 29,14 wanawake 31,09.

 

Akiwa ni mtoto wa tatu kuzaliwa, katika familia ya Mbarouk Ali Suleiman yenye watoto wanne, ameshatimiza miaka 35, tokea alipofika hapa ulimwenguni.

 

                    Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...