Skip to main content

Posts

MAHAKAMA KUU YAMLAZA CHUO CHA MAFUNZO MIAKA 30 FARIDI KWA ULAWITI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MAHAKAMA kuu Zanzibar kanda ya Pemba, imempeleka chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka 30, mshitakiwa Farid Abdalla Omar mika (35) wa Chambani wilaya ya Mkoani, baada ya kutiwa hatiani kwa makosa mawili, likiwemo la kumlawiti mtoto wa miaka 6. Jaji Mahakama hiyo Ibrahim Mzee Ibrahim, alilipokea jalada la kesi hiyo, likitokea mahakama maalum ya makosa ya udhalilishaji mkoa wa kusini Pemba, kwa ajili ya kupangiwa hukumu. Kesi hiyo awali ilianzia kwenye mahakama hiyo na kuanza kusikilizwa mashahidi wa pande zote mbili, na baada ya mahakama hiyo kumtia hatiani, jalada la kesi yake, lilifikishwa mahakama kuu kwa ajili ya kupangiwa hukumu. Hayo yalifanyikwa, kwa vile kosa la mshtakiwa huyo linaanzia miaka isiyopungua 30 ama kifungo cha maisha, ambapo mahakama ya Mkoa, haina uwezo huo kisheria. Ndipo wiki iliyopita, jalada hilo lilifikishwa mikononi mwa Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim wa Mahakama kuu, na kuamza kulipitia kwa umakini, hadi ilipofika Novemba 21, mwa...

HUKUMU YA MZEE SODA TUHMA ZA UBAKAJI LEO PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: SHAHIDI nambari nne, Said Massoud ambae ni jirani wa mtuhumiwa wa ubakaji, Khamis Juma Chumu ‘ soda ’ (76) mkaazi wa Mtoni, amesema, mzee huyo hahusiki na tuhuma za ubakaji, kama zilivyowasilishwa mahakamani hapo.   Alidai kuwa, mzee ‘ soda’ ana mfahamu vyema, kwa ujirani na ni mkarimu mno, hivyo amekuwa akizungumza na kila mmoja, na shauri lililopo mahakamani, ni la kupangwa, ili kumachafua.   Shahidi huyo alidai kuwa, amekuwa nae karibu mno mzee ‘soda’ na hata siku ya tukio alikuwa hayupo kisiwani Pemba, na sio kweli kuwa, alikimbia baada ya kuwepo kwa tuhuma hizo.   Aliendelea kudai kuwa, mtoto aliyedai kubakwa na mzee ‘ soda ’ hamfahamu jina lake wala apoishi, na anayemjua yeye ni mzee huyo pekee.   ‘’Mheshimiwa Hakimu, mzee huyi ni mtu wangu na karibu, kila mmoja mtaani anamuheshimu, sasa leo nikisikia amebaka nishangaa sana’’,alidai shahidi huyo.   Kabla ya shahidi huyo kutoa ushahidi wake, akiongozwa n...

''MSIWAANGUSHIE VIPIGO WAJAWAZITO WATAZAA WATOTO WENYE ULEMAVU''

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: WANAUME katika wilaya ya Micheweni mkoa wa kaskazini Pemba, wameonywa tabia ya kupiga wake zao, hasa wenye ujauzito, kwani wanaweza kusababisha madhara kadhaa ikiwemo ulemavu kwa watoto tarajiwa. Kauli hiyo imetolewa na wanaharakati wa haki za watu wenye ulemavu kisiwani Pemba, wakati wakizungumza na mwandishi habari hizi, baada ya kumaliza ziara ya kuishajihisha jamii, utekelezaji wa haki za watu, wenye ulemavu. Walisema wakati mwengine, watoto huanza kuupata ulemavu tokea wakiwa tumboni mwa wazazi wao, inayosabishwa na madharaka mengi, ikiwemo vipigo. Mwanaharakati Aisha Hilai Hassan alisema, baadhi ya wanaume wamekuwa wakiwageuza ngoma wake zao, kwa kuwashushia vipigo hata kama wanaujauzito. Alisema, katika wilaya walizozipitia, wamegundua kuwa Micheweni kuna malalamiko mengi, ambayo wanawake waliwaeleza wakati walipokuwa, wanazungumza nao. ‘’Inawezekana wanaume wanadhani kila aina ya ulemavu mtoto huzaliwa nao kwa asili yake, kumbe upo mwe...

WAZIRI RAHMA ASITISHA UJENZI KITUO CHA 'WATER SPORTS' ZANZIBAR

    Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar Rahma Kassim Ali amesitisha ujenzi wa michezo ya baharini (Water Sports) unaojengwa na Muekezaji NJ Water sports eneo la fukwe za bahari Matemwe Wilaya ya Kaskakazini ‘A’’ kwa madai ya kukiuka kanuni na sheria ya Ardhi. Agizo hilo amelitoa mara baada ya kufanya ziara katika eneo hilo ambalo linadaiwa kuwa na mgogoro wa ardhi baina ya Muekezaji NJ Water Sports na Matemwe Bangaloes ambapo kesi ya mgogoro huo imeshafikishwa Mahakama ya Ardhi Gamba Wilaya ya Kaskazini “A” Unguja. “Nimelazimika kusitisha ujenzi unaoendelea ili kuweza kuutafutia ufumbuzi mgogoro huo ikiwa ni msimamizi mkuu wa masuala ya ardhi" sitoweza kuacha ujenzi uendele wakati kesi iko mahamani alisema Waziri huyo.   Alisema Mahakama ya Ardhi Gamba imeshatoa   maamuzi ya kusimamisha ujenzi wa muekezaji NJ Water Spots   ambae anadaiwa kuingia eneo la mwekezaji mwenzake huko Matemwe. Alifahamishwa kwamba Wizara ya Ard...

VIONGOZI WA DINI PEMBA 'WAFOK'A WATOTO WENYE ULEMAVU KUFUNGIWA NDANI

  HAJI NASSOR, PEMBA::: VIONGOZI wa dini kisiwani Pemba, wamewakumbusha wazazi na walezi, kuwafichua na kuwasajili watoto wao wenye ulemavu, ili wajiunge na wenzao, kama njia ya rahisi ya kupata haki zao za msingi ikiwemo elimu. Walisema, wazazi na walezi wanaowajibu wa kuhakikisha watoto wao wote wanapata haki za msingi kama elimu, matibabu bora, haki ya kucheza ili kutanua upeo wa ufahamu wao. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, juu ya mchango wa viongozi wa dini, katika kuihamasisha jamii ili kundi la watu wenye ulemavu, kupata haki zao, walisema kwanza ni kuwatoa nje. Mmoja kati ya viongozi hao sheikh Issa Hassan Maalim wa Chake chake alisema, kumfungia ndani mtoto kwa sababu ya ulemavu wake, ni kosa. ‘’Suala la ulemavu ni kudura ya Muumba, sasa kama mzazi anaichukulia kama ni kosa na kuamua kumfungia ndani, anamdhalilisha mtoto wake,’’alieleza. Nae kiongozi wa kidini nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Aisha Hasnuu Omar, alisema wazazi wote wanalojukum...

KISA CHA MWAKA PEMBA ''MUME WANGU HAJAMBAKA MTOTO WANGU WA KAMBO''

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: SHEMSA Hakim Khamis wa Chanjamjawiri wilaya ya Chake chake, ameiambia mahakama maalum ya makosa ya udhalilishaji ya mkoa wa kusini Pemba kuwa, mume wake hajambaka mtoto wao wa kumlea, bali ni uongo alioutengeneza mtoto huyo.   Alidai kuwa, mtoto huyo amekuwa muongo mzoefu na mzushi, maana siku ambayo, alidai amebakwa na mumewake, alikuwa safarini kikazi kisiwani Unguja.   Shemsa ambae ni shahidi nambari nne kwenye shauri linalomkabili mumewake (mtuhumiwa Said Abdalla Issa ), alidai kuwa mumewa alikuwa kisiwani Unguja kikazi siku hiyo aliyodaiwa kubaka.   Alidai kuwa, mtoto huyo ambae ni wa kulea, amekuwa muongo na alishawahi kumsingizia jirani wao mwanamme, kuwa alishawahi kumvulia nguo na kumuonesha sehemu zake za siri, ingawa walipofuatilia, haikuwa sahihi.   Mke huyo wa mtuhumiwa, alidai kuwa mtoto huyo pia alishawahi kukamatwa na barua ya mahaba, ndani ya mkoba wake wa mabuku ya skuli, akiashiria kuwa mtoto huyo a...

BILALI WA VITONGOJI RUMADE TUHUMA ZA UBAKAJI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA:::: MTUHUMIWA Bilali Hamad Kombo miaka 19, mkaazi wa Vitongoji wilaya ya Chake chake mkao wa kusini Pemba, ameanza kuhemea rumande, akikabiliwa na tuhma za kumbaka mtoto wa miaka 14.   Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha mashataka kutoka Afisi ya Mkurugenzi wa mashataka Ali Amour Makame kuwa, mtuhumiwa huyo bila ya halali na bila ya ridhaa ya wazazi wake, alimtorosha na kisha kumbaka mtoto huyo.   Alidai kuwa, tukio la kwanza la utoroshaji lilitokea Oktoba 29, mwaka huu, majira ya saa 1:40 asubuhi ambapo, mtuhumiwa anadaiwa kumtorosha mtoto huyo kutoka nyumbani kwao na kumpeleka nyumbani kwake Vitongoji wilaya ya Chake chake.   Kufanya hivyo ni kosa kinyume na kifungu cha 113 (1) (a) cha sheria Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, sheria ya Zanzibar.   Kosa la pili linalomkabili mtuhumiwa huyo, ni la ubakaji, kwa mtoto huyo huyo, alilodaiwa kulitenda pia Oktoba 29, mwaka huu, majira ya saa 2:00 asubuhi, wakati akiwa ...

WAZAZI WA WATOTO WENYE ULEMAVU PEMBA WANAKIU YA POSA.....

  HAJI NASSOR, PEMBA:: WAZAZI na walezi wa watoto wenye ulemavu shehia ya Vitongoji wilaya ya Chake chake Pemba, wameitaka jamii kutowabagua vijana wao, kwani wana haki ya kuchagua na kuchaguliwa, ili kuanzisha familia. Walisema, bado baadhi ya familia zimekuwa haziwachagua watoto wao kike, kwa sababu ya ulemavu wao, jambo ambalo wanasema ni kuwanyima haki zao masingi. Wakizungumza kwenye mkutano wa kuihamasisha jamii kutiii sheria na kufanyika Vitongoji, walisema wamekuwa na watoto wa kike kwa muda mrefu, bila ya kugongewa mlango. Mmoja kati ya wazazi hao Omar Khamis Omar, alisema jamii haiwaoni vijana wenye ulemavu kama sehemu ya kuanzisha familia, jambo ambalo linawatia unyonge. Alisema imekuwa ni adimu kuona mtu mwenye ulemavu anaolewa au wakati mwengine kukubaliwa posa yake, jambo ambalo, linawazidishia kujiona wanyonge. ‘’Mimi nna mwanangu ana ulemavu wa viungo, basi tulienda kupeleka posa baba mzazi akakubali, ingawa baada ya familia kukutana, tukirejeshwa kwa sa...

ALIYEMLAWITI MTOTO WA MIAKA 9, AFUNGWA MIAKA 20 PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:: KIJANA Massoud Khamis Mussa wa Vitongoji wilaya ya Chake chake, kuanzia Novemba 15 mwaka huu, ataendesha maisha yake akiwa chuo cha mafunzo, kwa muda wa miaka 20, baada ya mahakama maalum ya makosa ya udhalilishaji mkoa wa kusini Pemba, kumtia hatiani, kwa kosa la kumlawiti mtoto wa miaka 9. Mahakama hiyo chini ya Hakimu wake Muumini Ali Juma, ilisema imefikia uamuzi huo, baada ya mashahidi watano waliowasilishwa mahakamani kutoa ushahidi, ambao uilikidhi vigezo husika. Hakimu Muumini alitumia dakika 35 kumsomea hukumu mshitakiwa huyo, ambapo alisema ushahidi nambari moja ambao umetia hatiani mshitakiwa huyo, ni ule uliotolewa na mtoto wa miaka 9. Alisema mtoto huyo, wakati anatoa ushahidi wake, aliithibitishia mahakama kuwa, mshitakiwa Massoud Khamis Mussa, ndie mtu pekee ambae alishawahi kumlawiti akiwa bandani kwake. ‘’Mtoto alisema kuwa, siku ya kwanza kabla ya kulawitiwa, mshitakiwa alitumia mafuta ya nazi, kuupaka uume wake na kisha nae kum...

WANAFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUM PEMBA WAIPA NENO SERIKALI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: WANAFUNZI wenye mahitajia maalum katika skuli mbali mbali kisiwani Pemba, wameikumbusha serikali kuzidi kuimarisha miundo mbinu ya kielimu, ili watimize haki yao ya kupata elimu kwa ufanisi.     Walisema, bado serikali imekuwa ikiweka mikakati zaidi kwenye maandishi, ingawa hawaoni utekelezaji wake hasa kwa baadhi ya skuli, na kuendelea kuwaacha wao wakiwa kwenye mazingira magumu.   Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi   kwa nyakati tofauti, wasema wameshaitikia wito wa kwenda skuli kuungana na wenzao kutafuta elimu, ingawa bado wamezungurukwa na cgangamoto.   Mmoja katia ya wanafunzi Abdalla Hussein skuli ya Tumbe, alisema ukosefu wa vitabu vya nukta nundu, waalimu wenye utaalamu ni moja ya changamoto zinazowakabili.   ‘’Bado mazingira ya sisi wenye mahitaji maalum katika skuli skuli zetu hayajakuwa rafiki kwa sisi wenye ulembu wa aina mbali mbali, ni wakati wa serikali kuimarisha,’’alil...