Skip to main content

WAZIRI RAHMA ASITISHA UJENZI KITUO CHA 'WATER SPORTS' ZANZIBAR

 


 

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar Rahma Kassim Ali amesitisha ujenzi wa michezo ya baharini (Water Sports) unaojengwa na Muekezaji NJ Water sports eneo la fukwe za bahari Matemwe Wilaya ya Kaskakazini ‘A’’ kwa madai ya kukiuka kanuni na sheria ya Ardhi.

Agizo hilo amelitoa mara baada ya kufanya ziara katika eneo hilo ambalo linadaiwa kuwa na mgogoro wa ardhi baina ya Muekezaji NJ Water Sports na Matemwe Bangaloes ambapo kesi ya mgogoro huo imeshafikishwa Mahakama ya Ardhi Gamba Wilaya ya Kaskazini “A” Unguja.

“Nimelazimika kusitisha ujenzi unaoendelea ili kuweza kuutafutia ufumbuzi mgogoro huo ikiwa ni msimamizi mkuu wa masuala ya ardhi" sitoweza kuacha ujenzi uendele wakati kesi iko mahamani alisema Waziri huyo.

 Alisema Mahakama ya Ardhi Gamba imeshatoa  maamuzi ya kusimamisha ujenzi wa muekezaji NJ Water Spots  ambae anadaiwa kuingia eneo la mwekezaji mwenzake huko Matemwe.

Alifahamishwa kwamba Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi haina nia mbaya ya kumuonea mtu bali inahitaji wananchi wafuate sheria ili kuepusha migogoro ya Ardhi inayojitokeza katika maeneo mbali mbali ya Zanzibar.

 Aidha Waziri huyo alitoa wito kwa wageni na wenyeji ambao wanaohitaji kuekeza ujenzi wa aina yeyote kuhakikisha wanafuata sheria na taratibu zilizowekwa ikiwemo kupata kibali cha ujenzi kutoka Taasisi ya  Utoaji wa vibali vya Ujenzi(DCU) kabla ya kuanza hatua ya ujenzi huo.

Naye  Mkurugenzi Mipango Miji na Vijiji Kutoka Kamisheni ya Ardhi Muchi Juma Ameir alifahamisha kua lengo la kuwepo kwaTaasisi hiyo ni kuepusha migogoro ya ardhi isiyo na ulazima kwani inarudisha nyuma jitihada za kuleta maendeleo ya nchi yetu.  

‘’Kibali ambacho kinatolewa na DCU huwa kinaonesha michoro ya ujenzi katika eneo husika  na mipaka, hivyo vibali vya  wawekezaji hao vitaonesha mpaka wa kila mmoja” Alisema Muchi.

Naye Muekezaji Matemwe Bangaloes alisema Mwekezaji NJ Water Sports amejenga ukuta katika eneo lake baada ya kutofahamina kauli yangu ya kumtaka avunje ukuta huo  kwa muda wa miezi sita ndipo alipoamua kwenda Mahakamani kumshtaki ili apate haki yake.

Kwa upande wake Muekezaji NJ Water Sports alisema kua alifuata taratibu zote kabla ya kuanza ujenzi huo na yuko tayari Serikali ichukuwe hatua za kupima tena michoro ya ujenzi na endapo atakua ameingia katika eneo la muekezaji mwenzake basi yuko tayari kuliachia eneo ambalo limeingia upande wake au kulinunua ili aendelee na ujenzi  wa michezo ya baharini.

Mgogoro huo  ulianza mwezi wa June, 2022 baada ya NJ water kujenga ukuta katika eneo linalodaiwa sio la kwake hali ambayo imepelekea viongozi wa Serikali akiwemo Waziri wa Ardhi, Rahma, Mkuu wa Mkoa Kaskazini, Ayoub, Mkuu wa wilaya Sadifa, watendaji wa wizara mbali mbali kuingilia kati na mahakama kusimamisha ujenzi huo.

  Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch