Skip to main content

''MSIWAANGUSHIE VIPIGO WAJAWAZITO WATAZAA WATOTO WENYE ULEMAVU''



 NA HAJI NASSOR, PEMBA:::

WANAUME katika wilaya ya Micheweni mkoa wa kaskazini Pemba, wameonywa tabia ya kupiga wake zao, hasa wenye ujauzito, kwani wanaweza kusababisha madhara kadhaa ikiwemo ulemavu kwa watoto tarajiwa.

Kauli hiyo imetolewa na wanaharakati wa haki za watu wenye ulemavu kisiwani Pemba, wakati wakizungumza na mwandishi habari hizi, baada ya kumaliza ziara ya kuishajihisha jamii, utekelezaji wa haki za watu, wenye ulemavu.

Walisema wakati mwengine, watoto huanza kuupata ulemavu tokea wakiwa tumboni mwa wazazi wao, inayosabishwa na madharaka mengi, ikiwemo vipigo.

Mwanaharakati Aisha Hilai Hassan alisema, baadhi ya wanaume wamekuwa wakiwageuza ngoma wake zao, kwa kuwashushia vipigo hata kama wanaujauzito.

Alisema, katika wilaya walizozipitia, wamegundua kuwa Micheweni kuna malalamiko mengi, ambayo wanawake waliwaeleza wakati walipokuwa, wanazungumza nao.

‘’Inawezekana wanaume wanadhani kila aina ya ulemavu mtoto huzaliwa nao kwa asili yake, kumbe upo mwengine husababishwa kwa wanawake, kupigwa wakiwa wajawazito,’’alisema.

Nae Mwanaidi Iliyasa Hassan alisema, wakati wanawake wanazungumza nao, walisema wapo ambao sio kuzaa mtoto mwenye ulemavu pekee, wengine wameharibu pia ujauzito.

‘’Mwanamke anakuambia anapigwa wakati mwengine kwa kuchelewa kupika, au kuongeza ama kupunguza chumvi kwenye chakula huku akiwa na ujauzito,’’alifafanua.

Mmoja kati ya wanawake ambae alizaa mtoto mwenye ulemavu wa akili, akidai ilitokana na kipigo mkaazi wa Shumba mjini, alisema kesi hiyo aliifikisha kituo cha Polisi Micheweni.

Alisema, alipigwa na mume wake kwa sababu ya kuchelewa kurudi kwa mama wake mkwe, huku akiwa na ujauzito wa miezi minne, na hadi leo mtoto wake anaulemavu wa akili.

‘’Madaktari walisema sio rahisi kuwa ningeweza kujifungua salama, ingawa nilifanikiwa hivyo, lakini hadi sasa mtoto anamiaka 11 anaonekana na ulemavu wa akili,’’alieleza.

Kwa upande wake Mwanakhamis Yakouti Juma, aliwataka wanawake wenzake, ni vyema kuisamehe ndoa, lakini wanapopigwa wapeleke taarifa vituo vya sheria.

‘’Wapo wanawake wanapigwa, na kisha hukaa kimnya na wakati wa kujifungua hupata shida hadi wengine kupoteza mtoto au kuzaa akiwa na ulemavu,’’alisema.

Mkuu wa wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya, amekuwa akirejea kauli yake ya kuwataka wanawake kutoa taarifa wanaponyanyaswa ama kudhalilishwa.

‘’Kama mwanamke unapata madhila na kisha unakaa kimnya, itakuwa huipendi afya yako, njooni hata ofisini kwangu mtoe taarifa,’’alisema.



 Mjumbe wa kamati tendaji ya Jumuiya ya wanawake wenye ulemavu Zanzibar ‘JUWAUZA’ Hidaya Mjaka Ali, alisema pamoja na kwamba ulemavu ni kudura ya Muumba, lakini kama yupo anayechangia, lazima sheria ichukue mkondo wake.

Mjumbe wa baraza la taifa la watu wenye Ulemavu Zanzibar Mashavu Juma Mabrouk, amewataka wanawake kisiwani Pemba, wanaopata madhila kuhakikisha wanatoa taarifa maeneo husika.

Taarifa ya kihalifu Jeshi la Polisi Tanzania ya mwaka 2020, imeibua wanawake 636 waliopigwa na watu mbali mbali, na wengine 1,963 waliojeruhiwa katika matukio mbali mbali nchini kote.

 

                                  Mwisho    

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch