Skip to main content

WAZAZI WA WATOTO WENYE ULEMAVU PEMBA WANAKIU YA POSA.....

 




HAJI NASSOR, PEMBA::

WAZAZI na walezi wa watoto wenye ulemavu shehia ya Vitongoji wilaya ya Chake chake Pemba, wameitaka jamii kutowabagua vijana wao, kwani wana haki ya kuchagua na kuchaguliwa, ili kuanzisha familia.

Walisema, bado baadhi ya familia zimekuwa haziwachagua watoto wao kike, kwa sababu ya ulemavu wao, jambo ambalo wanasema ni kuwanyima haki zao masingi.

Wakizungumza kwenye mkutano wa kuihamasisha jamii kutiii sheria na kufanyika Vitongoji, walisema wamekuwa na watoto wa kike kwa muda mrefu, bila ya kugongewa mlango.

Mmoja kati ya wazazi hao Omar Khamis Omar, alisema jamii haiwaoni vijana wenye ulemavu kama sehemu ya kuanzisha familia, jambo ambalo linawatia unyonge.

Alisema imekuwa ni adimu kuona mtu mwenye ulemavu anaolewa au wakati mwengine kukubaliwa posa yake, jambo ambalo, linawazidishia kujiona wanyonge.

‘’Mimi nna mwanangu ana ulemavu wa viungo, basi tulienda kupeleka posa baba mzazi akakubali, ingawa baada ya familia kukutana, tukirejeshwa kwa sababu ya ulemavu,’’alisema.

Nae Maimuna Hamad Mjaka, alisema mtoto wake mwenye uziwi alishapokea posa mara mbili, lakini inapokaribia wakati wa kufanya maandalizi ya harusi, wahusika hukimbia.

‘’Mwaka jana tulishapokea fedha za awali za mahari, na wakati wanakwenda hospitali kuchunguuza afya zao, wakamgundua ana tataizo ya usikivu hafifu, walikataa,’’alieleza.



Aidha mzazi Mayasa Haji Issa ‘da maa’ alisema pamoja na vijana wa kike na kiume wenye ulemavu kuwa wastahamilivu hasa wanapoingia kwenye ndao, lakini bado kundi kubwa la watu hao wanawapiga chenga.

Mmoja kati ya vijana miaka 26 ambao aliposwa mara mbili kwa miaka miwili tofauti, alisema kwa sasa ameshakata tamaa, juu ya kuanzisha familia.

‘’Maana wanaonikataa wanasema kwa sababu ya kuburura kwangu mguu, sasa hili mimi sikuliomba ni kazi yake Allah, sasa kama wachumba wananikataa kwa hili, ni milele tena,’’alieleza.

Hata hivyo alisema hajakata tamaa, kwa vile wenzake wawili wenye ulemavu kama wa kwakwe, aliosomanao chuoni mwaka 2017, wameshaolewa.

Mratibu wa wanawake na watoto shehia ya Kangagani Awena Salim Kombo, alisema suala la ndoa na mtu na ulemavu wake halina uhusiano wowote.

‘’Ulemavu wakati mwengine unatokana na matukio ya hapa na pale mfano ajali, kuungua moto sasa kila mmoja anaweza kupata, isiwe jambo wengine kukosa haki za ndoa,’’alishauri.

Akizungumza kwenye moja ya mikutano ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari, Mkurugenzi wa Baraza la taifa la watu wenye ulemavu Zanzibar Ussi Khamis Debe, alisema kukataa kufanda ndoa kwa sababu ya ulemavu wa mtu aliyonao ni changamoto.

‘’Hata mimi wakati sijakuwa na kazi yangu, nilipeleka posa kila kona, lakini mwisho nikapata mchumba na kuoa, sasa ni Mkurugenzi wananijia wenyewe,’’alifafanua.

Kwa upande wake, Mtaribu wa Idara ya watu wenye ulemavu kisiwani Pemba, Mashavu Juma Mabrouk, alisema nguvu za ziada zinahitajika, kuielimisha jamii, mchango wa watu wenye ulemavu.

 Mratibu wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ tawi la Pemba Safia Saleh Sultan, alisema suala la kuwa na mwenza ni la kibinaamu zaidi.

‘’Sio suala la kuangalia aina ya ulemavu wa mtu bali ni haki ya kibinadamu zaidi na ambayo haihitaji manyanyaso wala kero ndani yake,’’alieleza.

Mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulamavu, Ibara ya 18, imezitaka nchi zilizoridhia mkataba huu, kila mtu mwenye ulemavu ana haki na kuheshimiwa kwa ajili ya utu wake kwa misingi sawa na wenzao.

Ibara ya 23 (a) na (b) imesema watu wote waliofikia umri wa kufunga ndoa, na kuanzisha familia na hata suala la kupanga idadi ya watoto wawatakao na ni kosa kufungwa kizazi maana ni haki zao.

                                   MWISHO.



Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch