NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@
MAMLAKA ya Mapato Zanzibar 'ZRA' imesma, imezifanyia mabadiliko sheria saba za kodi kwa mwaka wa fedha
2026/2027, yanalenga kuleta ufanisi katika makusanyo na kuwapa ahuweni wananchi.
Hayo yameelezwa leo August 28, 2026 na Mkuu wa Kitengo cha Habari Makame Khamis Mohamed wakati akiwailisha mabadiliko ya sheria hizo kwa wahariri na waandishi wa habari wa
vyombo mbalimbali kisiwani Pemba, katika ukumbi wa mikutano wa Mamlaka hiyo
Gombani Chake chake Pemba.
Alisema
kua mabadiliko hayo, yanalenga kuleta ufanisi kwa mlipa kodi na serikali, kwani
yamezingatia kupunguza kasoro mbalimbali, zinazojitokeza pande zote mbili
wakati wa kulipa na kukusanya kodi hizo.
Alieleza
kua mabadiliko ya sheria hizo pia
yamezingatia mabadiliko na mwenendo wa sayansi na teknolojia, pamoja na kuzingatia unafuu kwa walipakodi na
kuongeza mapato kwa serikali kuu.
"Sababu
ya madiliko ya sheria mbalimbali za kodi kwa mwaka wa fedha 2026/2027 ni
kuongeza ufanisi zaidi katika ukusanyaji na ulipaji wa kodi, kwa kuondoa vikwazo
vilivyokuwepo, kasi ya sayansi na teknolojia, kuleta unafuu kwa walipakodi na
kuongeza mapato ya serikali" alieleza.
Akizungumzia sheria zilizofanyiwa mabadiliko, alisema ni pamoja na Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani, inaeleza kuondoshwa kwa kodi, ambayo kwa sasa inatoa fursa kwa wawekezaji wa viwanda vidogo na vya kati, ambao hawajasajiliwa ZIPA, hawatolipa kodi ya 'VAT' katika uingizaji wa malighafi.
Alisema sheria nyengine iliofanyiwa mabadiliko ni sheria ya Fedha ya Kodi za Miundombinu, ambapo marekebisho yake yanaruhusu uingizaji wa vifaa saidizi vya watu wenye mahitaji maalum, kutotozwa kodi ya miundombinu, jambo litakalosaidia ustawi wao.
Alieleza
vifaa hivyo ni pamoja na viti mwendo, viungo bandia, visaidizi vya kuona na
kusomea, fimbo nyeupe na mashine za kutolea hati nundu, na vyoo vinavyotumiwa
na watu wenye ulemavu.
Alieleza
sheria ya tatu iliofanyiwa mabadiliko, ni sheria ya Ushuru wa Stempu, ambapo kwa sasa hati ya usajili kwa wafanyabiashara wanaolipa ushuru wa Stempu itamaliza muda wake ifikapo miezi 12 baada ya tarehe ya kutolewa.
Aidha alieleza sheria hii, imekuja kupunguza kiwango cha ushuru wa stempu kwa asilimia 25, kwa gari za biashara, jambo litakalorahisisha utoaji huduma bora kwa wananchi.
Alifafanua kuwa, sheria nyengine iliofanyiwa mabadiliko ni Sheria ya Ada za Bandari, ambayo inaeleza ada ya huduma za bandari, kwa wageni wanaosafiri ndani
ya Zanzibar (Pemba/ Unguja) na kutoka
Zanzibar kwenda Tanzania Bara imeongezwa
kutoka Zanzibar kwenda Tanzania Bara dola 2 hadi dola 3; na kutoka Unguja kwenda Pemba dola moja hadi mbili 2.
Mkuu huyo wa Kitengo cha Habari, kutoka ZRA alifahamisha sheria nyengine iliofanyiwa mabadiliko ni
sheria ya Ushuru wa Bidhaa kinachoeleza, uingizaji wa bidhaa
kutoka Tanzania Bara, hazitotozwa kiwango cha ushuru wa bidhaa, ikiwa
zitahamishiwa kwa matumizi ya Zanzibar, ikiwa kiwango cha ushuru wake ni sawa au
kikubwa kama kiwango cha Zanzibar.
Inaeleza
, ikiwa ushuru wa bidhaa unaotumika Zanzibar ni mkubwa kuliko Tanzania Bara, tofauti
ya ushuru huo itachukuliwa kuwa haijalipwa na itakusanywa Zanzibar wakati wa
kuingizwa bidhaa hiyo Zanzibar.
Sheria
hii inaeleza Ushuru wa bidhaa kwa kampuni zinazorusha matangazo ya Televisheni
(Cable Television Company) umeongezwa na kuwa Asilimia saba (7%) pamoja na kutoza Ushuru wa Bidhaa kwa kiwango
cha asilimia kumi (10%) kwenye tiketi za kiingilio katika Viwanja vya Michezo,
Kumbi za Starehe na Maeneo ya Burudani.
Sheria nyengine iliofanyiwa mabadiliko ni sheria ya Usimamizi wa Kodi, ambapo
kwa sasa cheti cha usajili wa mlipakodi, kitapaswa kuoneshwa hata kwa njia ya kidijitali, katika eneo la biashara.
''Sheria hii imeainisha kua adhabu ya faini kwa
mlipakodi atakeshindwa kutoa risiti ya kielektroniki imeanzia kiasi
kisichopungua shilingi 200,000 na kisichozidi shilingi milioni 2.
Aidha
imeainisha mlipakodi aliyekuwa nje ya Zanzibar anaweza kuomba kuongezewa muda
wa kulipakodi kwa maandishi kwa Kamishna. Baada ya kiogozi huyo, kujiridhisha kwa sababu za
kutokuwepo kwake Zanzibar, au maradhi au sababu nyingine za msingi.
Imeainisha
kua ugomboaji wa deni kwa njia ya mtu wa tatu kupitia matumizi ya kadi za
malipo za kielektroniki kutoka kwa watoa huduma za malipo ya kielektroniki.
Akizungumzia kuhusu makiso ya makusanyo yao, Makame
alissema , kua 'ZRA' kwa mwaka wa fedha 2026/2027
imekadiria kukusanya shillingi Tirrion 1.726 kupitia vyanzo mbalimbali vya
makusanyo, hivyo amesisitiza wananchi kulipakodi kwa hiari ili kufanikisha
hilo.
Akizungumza
kwa niaba ya waandishi wa habari walishiriki mafunzo hayo Mkurugenzi uratibu
shirika la Magazeti ya serikali Pemba Haji Nassor Mohamed aliipongeza ZRA kwa
kuwaogezea maarifa waandishi juu ya sheria mbali mbali za kodi huku akiwasihi
kuendeleza utaratibu huo.
MWISHO

Comments
Post a Comment