Skip to main content

MAHAKAMA KUU YAMLAZA CHUO CHA MAFUNZO MIAKA 30 FARIDI KWA ULAWITI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA

MAHAKAMA kuu Zanzibar kanda ya Pemba, imempeleka chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka 30, mshitakiwa Farid Abdalla Omar mika (35) wa Chambani wilaya ya Mkoani, baada ya kutiwa hatiani kwa makosa mawili, likiwemo la kumlawiti mtoto wa miaka 6.

Jaji Mahakama hiyo Ibrahim Mzee Ibrahim, alilipokea jalada la kesi hiyo, likitokea mahakama maalum ya makosa ya udhalilishaji mkoa wa kusini Pemba, kwa ajili ya kupangiwa hukumu.

Kesi hiyo awali ilianzia kwenye mahakama hiyo na kuanza kusikilizwa mashahidi wa pande zote mbili, na baada ya mahakama hiyo kumtia hatiani, jalada la kesi yake, lilifikishwa mahakama kuu kwa ajili ya kupangiwa hukumu.

Hayo yalifanyikwa, kwa vile kosa la mshtakiwa huyo linaanzia miaka isiyopungua 30 ama kifungo cha maisha, ambapo mahakama ya Mkoa, haina uwezo huo kisheria.

Ndipo wiki iliyopita, jalada hilo lilifikishwa mikononi mwa Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim wa Mahakama kuu, na kuamza kulipitia kwa umakini, hadi ilipofika Novemba 21, mwaka huu, akamua kumsomea hukumu.

‘’Mshitakiwa kutokana na kutiwa hatiani kwa kosa la kwanza la kutorosha, mahakama hii kuu inakupa miaka 10, na kosa la pili la kulawiti nalo utatumikia miaka 20 chuo cha mafunzo, ‘’alisema Jaji Ibrahim.

Aidha Jaji huyo akisoma hukumu hiyo, mbele ya waendesha mashtaka wa serikali Seif Mohamed Khamis na Asiya Ibrahim, alisema kifungo hicho cha mshitakiwa huyo, cha miaka 30 kitakwenda sambamba.

‘‘Mshtakiwa, ushahidi uliotolewa na mashahidi wa upande wa mashataka, ulitosha wewe kukutia hatiani maana haukuacha chembe ya shaka, kuanzia wa mtoto mwenyewe hadi mpelelezi,’’alisema Jaji huyo.

Kabla ya kusoma kwa hukumu hiyo, mawakili hao wa serikali, waliiomba mahakama hiyo kuu, kutoa dhabu kwali kwa mshitakiwa, ili iwe fundisho kwake na wengine wenye tabia kama hiyo.

Kosa la kumtorosha mtoto huyo, ilithibiti kuwa alilitenda April 30, mwaka huu majira ya saa 9:30 jioni, eneo la Tumbini Chambani wilaya ya Mkoani, kwa kumtorosha mtoto huyo kutoka nyumbani kwao, na kumpeleka nyuma ya hospitali ya Tumbini.

Kosa la pili, ni kumlawiti mtoto huyo siku hiyo hiyo majira ya saa 9:35 jioni, ambapo ni kosa kinyume na kifungu cha 115 (1) sheria nambari 6 ya mwaka 2018 sheria Zanzibar.

                               Mwisho  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...