NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@
UTAMADUNI, ni neno
la lugha ya kiswahili, ambalo kwa lugha ya kiingereza ni ‘culture’,
lenyewe likitokana na neneo la kilatini, lenye maana ‘Cultura’.
Mitandao ya kijamii,
inaripoti kuwa, neneo hilo usuli wake ni neno ‘colere’, linalomaanisha
"kulima, kustawisha.
Ikifafanua kuwa, neno
hili linafafanuliwa kwa namna nyingi, ikiwemo tokea mwaka 1952, na Alfred Kroeber na Clyde Kluckhohn, walikusanya
orodha ya vijelezi 164 vya neno hilo, katika kazi yao.
Miongoni mwa vijelezi
hivyo ni ‘culture:a’, critical, Review, ambapo lengo ni kuonesha
mzizi wa neno, utamaduni kwa lugha ya Kiswahili, ama ‘culture’ kwa
lugha ya kiingereza.
KWANINI MATAIFA YAWE
NA UTAMADUNI?
Inafahamika katika
maandishi mbalimbali, kikiwemo kitabu cha ‘ukombozi wa kiutamaduni’ kuwa, utamaduni
ni kielelezo cha uhai wa watu.
Kwa mfano
Tanzania pekee, imeundwa na mchanganyiko wa zaidi ya makabila 120, yenye
mila, lugha na desturi zinazotofautiana.
Ingawa pamoja natofauti
hizo, watanzania, kama alivyowahi kusema Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania hayati Julius Kambarage Nyerere, sio kwa ajili ya kuchukiana.
‘Kweli Tanzania
yapo makabili zaidi ya 120 yenye utamadyni usiofanana na wakati mwingine ambao
haukaribiani, hili lisiwe chanzo la kutugawa,’’alisema.
Kupitia
maandishi kadhaa, inaonesha historia ya utamaduni wa Tanzania, umekuwa
ukiathiriwa na mchanganyiko wa jamii zenye asili ya Kibantu, Waswahili wa
pwani, na athari kutoka kwa waarabu.
Na makabila ya
waajemi, wazunfu na wale waliowahi kutawala sehemu ya Afrika Mashariki kwa
wakati huo.
Aidha, mabaki
ya michoro katika miamba, katika maeneo kama Tendaguru na hifadhi ya Swaga
Swaga, yanaonesha uwepo wa utamaduni tangu enzi za kale, huku baadhi ya michoro
ikikadiriwa kuwa na zaidi ya miaka 500.
TAFSIRI YA SASA YA MAANA YA UTAMADUNI
Ni njia, mwelekezo na jinsi binaadamu
anavyokabili maisha yake ya kila siku,
iwenya kiimani, Sanaa, maadili, sheria na desturi.
Hapa utagundua kuwa, kwa kule
mwanaadamu kuwa na utamaduni, ndio kwa sifa hiyo maalumu, humtofautisha na
wanyama kama Simba na Nyati.
Julai 22, mwaka 2015
aliyekua Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Moghamed
Shein, nae aliwakumbusha wananchi, kuelewa kuwa heshima na tabia njema, walizonazo
ni sehemu muhimu ya utamaduni wao.
Akasema ni muhimu kwa
kila mtu, kuhakikisha anatoa mchango wake katika kulinda, kuukuza na kuutangaza
utamaduni wa mzanzibari, kwa kuzingatia mambo mazuri wanayoyapenda wananchi husika.
Kauli hii aliitoa wakati
akilizindua Tamasha la 20 la Utamaduni wa Mzanzibari, kwenye hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na aliyekuwa
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, ukumbi wa Salama
Hoteli ya Bwawani Unguja.
Akasisitiza kuwa, endapo
mkakati wa makusudi utawekwa wa kuwashawishi wageni kuiga mambo ya asili na
utamaduni wanaoutembelea, bila shaka wageni na watalii hao watavutiwa na
kuyapenda na hatimae yatalipatia sifa taifa.
Hakuacha kuipongeza
Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo kwa kushirikiana na Kamati
Maalum ya Maandalizi na Uendeshaji wa Tamasha la Utamaduni la Mzaznzibari,
kwa kuongeza kasi na ubunifu katika matayarisho.
MATAYARISHO YA
TAMASHA LA 31 YAKOJE PEMBA
August 18, mwaka huu Kaimu
Ofisa Mdhamini Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Pemba,
Sharifa Hamad Shapandu, alizizindua kamatano kwa ajili ya matayarisho hayo.
Hafla hiyo ilifanyika
ofisini kwake Gombani Chakechake Pemba, na kuzitaka kamati za kufanikisha tamasha
hilo la 31 la utamaduni wa mzanzibari, kuhakikisha zinafanyakazi kwa kushirikiana.
Akasema kuwa, kuwepo kwa kamati hizo anataka iwe ni njia rahisi ya
kufanikiwa kwa tamasha hilo, ambalo kwa awamu hii, linatarajiwa kuwa la aina
yake.
Yeye akaona kuwa, njia ya kuzigawa kwa kamati hizo, ni namna ya kuwa na na urahisi
wa ufuatuliaji, ingawa isiwe chanzo cha kukosa kushirikiana.
‘’Najua kuwa zipo kamati tano, zinawajumbe wenye uwezo na
maarifa yasiofanana, lakini hili sasa muwe na ushirikiano kwa pamoja, ili
kulifanikisha hili,’’alifafanua.
Aidha Kaimu Ofisa Mdhamini huyo, amewataka wananchi kushiriki kikamilifu
katika tamasha hilo, tangu kuanza kwa uzinduzi wake wilaya ya Micheweni, ili
kujionea mambo mbalimbali ikiwemo, utamaduni wa kizanzibar, michezo, maigizo na
ngoma za asili.
"Wananchi wote nawaomba mushiriki kikamilifu, katika tamasha hili la utamaduni
wa mzanzibari, ikiwa ni njia moja wapo ya kujionea utamaduni wetu na wingine
kujikumbusha,’’alieleza.
Mapema Mkuu wa Divisheni na Utamaduni Pemba Hamad Ali Haji,
alisema tamasha hilo litakuwa la aina yake kwa mwaka huu, kwa kuvishirikisha
zaidi ya vikundi 10 vya ngoma asili, kutoka Unguja na Pemba.
Alisema, tangu kuanzishwa kwa tamasha hilo, kwa mwaka huu,
ambalo ni 31, kwa wanachi watakaojitokeza wataniufaika na mambo makubwa,
ikiwemo resi za ngalawa, Punda, msewe wa zamani na sasa, taarab asilia na mbio
za baiskeli.
‘’Kwa mwaka huu wizara yetu ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo,
chini Waziri Riziki Pembe Juma Khamis na Katibu Mkuu Matar, tamasha hili,
litakuwa la kuvutia na si la kukosa,’’alisisitiza.
Katika hatua nyingine, alisema tamasha hilo kwa kuanzia, litazinduliwa
Septemba 19 hadi 23 mwaka huu kisiwani Pemba, wilaya ya Micheweni na mgeni
rasmi akitarajiwa kuwa, Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla.
Alifafanua kuwa, kwenye uzinduzi wa tamasha hilo, utafuatiwa na matembezi
ya wajasiriamali, wasanii wa ngoma za asili, utenzi na shamra shamra nyingine
za kulipamba.
Siku ya pili, tamasha litahamia wilaya ya Wete, litanogeshwa na maulidi
ya home, nasheed, dufu na maigizo yanayohusiana na tamaduni wa kiislam na
kizanzibari.
‘’Wananchi wa wilaya ya Wete, wanakaribishwa siku hiyo, ukumbi
wa zamani wa baraza la Wawakilishi, ambapo hakutakuwa na kiingilio,’’alisema.
Aidha Mkuu huyo wa Divisheni ya Utamaduni Pemba, alisema Septemba 21, kutakuwa
na mashindano ya ngalawa, yatakayoambatana na sarakasi na ngoma za asili Mkoani,
na siku inayofuata ni mchezo Ng'ombe uwanja Pujini.
‘’Niwaarifu wananchi wa
Pemba, tamasha hili litahitimishwa Septemba 23, kwa usiku wa sanaa, pamoja na
wajasriliamali, wakionesha shughuli mbalimbali, zikipambwa na kwa taarabu, uwanja
wa Gombani, kabla ya kilele Septemba 25 Unguja,’’alieleza.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya Habari na Burudani Adam Ramadhani
Kombo, ameipongeza wizara, kwa kuendeleza tamasha hilo na kuahidi kamati yake,
itafanyakazi kwa karibu na wizara, ili kufanikisha shughuli hiyo.
Aidha aliwataka wajumbe wa kamati hiyo, kuhakikisha, kazi na
majukumu waliyopewa wanayafanya kwa ufanisi, ili kuhakikisha wananchi wote
wanapata taarifa.
Hili ni tamasha la 31, la utamaduni wa mzanzibari, kufanyika
Unguja na Pemba, ambapo kwa mwaka huu, uzinduzi wake unatarajiwa kufanyika
Micheweni Septemba 19 mwaka huu.
WANANCHI WANASEMAJE
Ali Hamad Mjaka wa Micheweni mjini, anasema wizara imefanya
jambo, jema kuifanya wilaya ya Micheweni kama sehemu ya uzinduzi.
Omar Bashiru Omar wa Mjananza, anasema kilichobaki ni wao kusubiri
siku ifike, ili waungune na watendaji wa wizara ya Habari, katika uzinduzi wa
tamasha hilo la 31 la utamaduni wa mzanzibari.
Mwajuma Haji Othman na mwenzake Aisha Msellem Hassan, walisema
juhudi za serikali za kuutangaaza utamaduni ni kubwa, ingawa sasa kilichobakia
ni juhudi za kuurejesha.
WIZARA YA HABARI INAFANYA NINI
Kwa mwaka 2024/2025 Wizara ilifanikiwa
kufanya Tamasha la 29 la Utamaduni wa Mzanzibari, kwa lengo la kurithisha mila,
silka, desturi na Tamaduni za Mzanzibari. Hayo yalifahamika kwenye hutuba ya
wizara hiyi, ambapo pia shughuli mbalimbali zenye mnasaba na tamasha hilo,
zilifanyika zikiwemo maonyesho ya bidhaa za kitamaduni na dawa za asili na
sanaa za ngoma za asili.
Ikafahamika kuwa, wizara imesaidia
vikundi 78 vya kitamaduni na wasanii 28, kushiriki katika matamasha ya ndani na
nje ya nchi.
Upande mwingine ikaelezwa kuwa, serikali
inaendelea kuchukuwa juhudi kubwa za kuielimisha jamii, juu ya umuhimu wa
kuendeleza sanaa na utamaduni wa kizanzibari.
Kwa mwaka uliopita, wizara ya Habari,
Sanaa, Utamaduni na Michewezo, moja ya vipaumbele vyake, ilikua ni kutoa elimu
kwa jamii, juu ya kulinda mila silka na utamaduni wa mzanzibari.
Ambapo iliwajengea uwezo wajasiriamali wa
22 bidhaa za kiutamaduni, kusimamia shughuli za sanaa na burudani pamoja na
kuwaunganisha wasanii na fursa mbalimbali.
MWISHO.


Comments
Post a Comment