Skip to main content

UKWELI WA DK. MWINYI BAADA YA KUINGIA IKULU, SASA WANAFUNZI 1,236 KONDE WATELEZA KWENTE '''TAIZ' WAKIWA GHOROFANI

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

KWA sasa wazanzibar wote, wamo katika shamra shamra za miaka sita ya uongozi war ais kipendwa Dk. Hussein Ali Mwinyi, tokea alipowasili Ikulu ya Zanzibara mwaka 2020.

Lengo kuu la yeye kuingia Ikulu, ilikuwa ni kumboa mzalendo wa Zanzibar, ili azidi kuwaletea neemaa, baada ya kupokea kijiti za uongozi kutoka kwa mtangulizi wake Dk. Ali Mohamed Shein.

Si unajua ndani ya Chama cha Mapinduzi CCM, iko demokrasia iliyokomaa, kwa kuhakikisha viongozi wanapishana, ili kuomba ridhaa kwa wananchi, kila baada ya miaka mitano.

Mwenye Dk. Mwinyi tokea awamu yake ya kwanza n ahata hii ya pili, ambapo sasa ameshatimiza miaka sita ya uongozi, alipita kwa wananchiu kuwaomba ridhaa.

Nakumbuka vyema, alipokuwa ndani ya Jimbo la Konde, aliwaomba wananchi kwanza kumpa ridhaa, ili azidi kunogesha maendeleo ya kielimu, ikiwemo ujenzi wa skuli za kisasa.

‘’Nawaombeni kura, nikifika Ikulu miongoni mwa ahadi zangu moja wapo ni kuwajengea skuli ya ghorofa hapa Konde, ili kuweka mazingira rafiki ya elimu,’’alisisitiza.

Maneno hayo Dk. Mwinyi aliwahi kuyarejea alipokuwa jimbo la Gando, kwamba anahamu kuona Unguja na Pemba, imejaa maghorofa na vifaa kamili vya kujifunzia na kufundishia.

Ahada hizi za Dk. Mwinyi kwa wakati ule, zilisisitizwa kwa mkazo na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdalla, kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Makombeni.

‘’Dk. Mwinyi amekuwa ni muungwa, na anapoahidi suala la kutekeleza huwa ni jambi rahisi, naamini kule Konde, Kiwani, Mwambe, Kengeja na Michakani maghorofa yanakuja,’’alisema.

Hata aliyekuwa mgombea uwakilishi Jimbo la Konde Zawadi Amour Nassor, nae aliwakumbusha wananchi kuwa, wapo viongozi kadha waliopita walishafanya makubwa,  ingawa na Dk. Mwinyi ataongeza.

‘’Wakati ameshaahidi ujenzi wa skuli wa ghorofa ya Konde, naamini tumpeni kura, ataijenga, maana huyu amekuwa na maneno kidogo na vitendo ndio vingi,’’alisisitiza.

BAADA YA KUINGIA IKULU DK. MWINYI

Sasa ni miaka sita, tokea mpendwa huyo arejee tena kuwaongoza wananchi wa Zanzibar, na tayari wanafunzi wa skuli ya sekondari Konde wanajipatia haki yao ya elimu wakiwa ndani ya skuli ya ghorofa tatu.

Kumbuka sasa, wazanzibari hao, sasa wanasherehekea miaka sita ya Dk. Mwingi kuwaongoza, tokea alipopewa ridhaa pale mwaka 2020.

Yeye anaendeleza yale aliyoachiwa na watangulizi wake, ingawa kila mmoja ni shahidi miaka yake sita ya uongozi, utadhania miaka 600, kutokana na utekelezaji wa Ilani uliotukuka.

Na ndio maana, kwenye moja ya tunda la miaka yake sita hii, ni upatikanaji wa skuli ya ghorofa tatu ya sekondari Konde wilaya ya Micheweni.

Kazi ya kuifungua skuli hii, ilifanywa na mwenyewe Novemba 1, mwaka jana, ambae kisha aliwahutubia wananchi wanaccm wa mikoa miwili ya Pemba.

Hafla hiyo, ilifanyika uwanja wa mpira Konde, ambae aliwaeleza wananchi namna alivyofanikiwa kuitekeleza Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025 kwa vitendo kwa wakati huo.



‘Leo ndani ya uongozi wa serikali ya awamu ya nane, nimeshayatekeleza kwa vitendo, aliyowaaahidi wananchi, ikiwemo ujenzi wa madarasa 2,773 katika skuli zote za Unguja na Pemba,’’alianza hivyo.

Akasema, Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025 iliitaka serikali ya awamu ya nane, kujenga madarasa 1,500 ingawa wameshavuuka lengo hilo, kwa asilimia 184, na bado kazi inaendelea.

Kumbe hata hivyo anasema, serikali imepanga hadi kufikia mwakani, iwe imeshajenga vyumba 2,000 vya madarasa katika skuli zote za Unguja na Pemba, ili kuondoa mikondo miwili.

‘’Ndani ya miaka sita ya madarakani, ya serikali ya awamu ya nane, anawaeleza wale wengine kuwa, kama wanapiga porojo na kusema, uongo waangalie takwimu kutoka wizara ya Elimu, zitadhihirisha ahadi zangu ,’’anasema.

Kumbe Dk. Mwinyi ndani ya miaka hii sita ya kuwaongoza kwa utulivu wazanzibar, mwenyewe anataja mafanikio mingine kuwa, ni kuongezeka kwa bajeti ya mikopo ya elimu ya juu.

Hapa ukiwa mtundu wa kufuatilia hutuba za Dk. Mwinyi utagundua kuwa, bajeti hiyo imeongezeka, kutoka shilingi bilioni 11.5 hadi shilingi bilioni 33.4 mwaka 2024.

‘’Haya hayahitaji porojo, maana nambari siku zote zinasema ukweli, na waje waangalie mafanikio haya, sasa wanaopita pita wakisema hovyo, wapuuzeni,’’anaeleza.

 Dk. Mwinyi akasema,  kwa vile nia ya serikali ni pia kuondoa unyonge wa ajira hasa za waalimu, anasema kwanza wapo waliokwisha ajira wafikao 3,384 na mwaka jana na wingine 1,239 wataajiriwa baadae.

Hapa akitaja skuli mpya za ghorofa, ikiwemo ya Konde kwamba nao watafika na jira hizo, ili kuongeza idadi ya waalimu kutoka 24 wa sasa.

‘’Bado tuna nia ya kuongeza idadi ya waalimu katika uajiri, ili kuhakikisha hakuna skuli yenye upungufu wa waalimu, kwani kwenye samani na majengo, tuko vizuri,’’anafafanua.



Hapa akadakia kuwa, kila skuli mpya inayojengwa kwa sasa, suala la miundombinu ya samani, maktaba na maabara ya masomo ya sayansi ni lazima.

Tena akasema hayo yanafikishwa, kutokana na kuimarika kwa bajeti ya mendeleo ya wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, kwa kufikia shilingi blioni 518 sawa na ongezeko la asilimia 552.

‘’Ndani ya miaka sita ya serikali ya awamu ya nane, bajeti ya maendeleo ya wizara ya elimu imekuwa, kwani kabla, ilikuwa ni shilingi bilioni 83,’’anasema.

WEMA

Katibu Mkuu, wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Khamis Abdalla Said, anasema miaka hii sita ya Dk. Mwinyi madarakani, ndani ya wizara wanayomingi ya kujivuania, likiwemo ujenzi wa skuli ya ghofora ya Konde.

‘’Kwa mfano leo ukienda shehia ya Konde, ipo skuli ya ghorofa tatu, na tayari kuanzia Janauri, 2025 wanafunzi 1,236 wameshaanza kuitumia, haya sio matunda madogo,’’anasema.

Tena akafafanua kuwa, ujenzi huo unakwenda sambamba na azma ya kweli, ya Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, ya kutaka kuoandoa mikondo miwili.

‘’Sisi wizara ya Elimu, tunashukuru mno kwa jitihada zako maalum kwetu, ambazo zinachangia kwa kiwango kikubwa, kuimarisha miundombinu ya elimu nchini,’’anaeleza.

MKOA KASKAZINI PEMBA

Mkuu wa Mkoa wa kaskazini Pemba, Mgeni Khatib Yahya, kubwa zaidi anakumbushia kuwa, awali wanafunzi walikuwa wakiingia mikondo mitatu, ingawa kwa ufunguzi wa skuli hiyo, hilo sasa limeondoka.

Anasema miaka sita ya Dk. Mwinyi kwa wananchi wa Konde, na hasa baada ya kumalizika kwa skuli ya ghorofa tatu, wanalo la kujivunia.



‘’Sasa wanafunzi wa skuli ya sekondari ya Konde, naamini wanasoma kwa utulivu, na hakuna tena mikondo miwili hapa, tunakushukuru,’’anafafanua.

Hata Mwakilishi wa Jimbo la Konde Zawadi Amour Nassor, anasema sasa Konde, inag’ara kwa kuwepo skuli tatu za ghorofa, ikiwemo Kifundi, Makangale na Konde.

‘’Leo ndani ya miaka sita ya Dk. Mwinyi Konde inang’ara kama ilivyo majimbo mingine ya Zanzibar, na mfano ni skuli hii ya Konde,’’anasema.

WANANCHI

Haji Ali Haji anasema yapo mazuri yaliyofanywa na Dk. Hussein katika mkoa huo, ikiwemo ujenzi wa skuli tatu za ghorofa, ndani ya Jimbo la Konde.

‘’Sisi wananchi wa Konde na mkoa kwa ujumla, tunakushukuru sana, kwa jitihada zako, na tunakuomba kuendelea kutuunga mkono,’’anafafanua.

Zuhura Khatib Mwadini, anasema sasa watoto wao, wanasoma ndani ya skuli ya ghorofa, ambayo miaka 62 iliyopita, haikujengwa.

‘’Kwa hakika Dk. Mwinyi ni mtekelezaji kweli wa ahadi zake, maana wakati atuaomba kura na kutoa ahadi ya ujenzi wa skuli ya ghorofa, kwa hakika sikuamini na leo nampa tano,’’anasema.

Aisha Juma Nassor, anasema yeye alisoma miaka 46 iliyopita, ingawa mazingira hayakuwa rafiki kama leo, ikiwemo samani na vifaa vya kujifunzia.

MWALIMU/WANAFUNZI

Msaidizi Mwalimu mkuu wakuli ya sekondari ya Konde Saleh Mbaroku Hemed, asema tunda kubwa la miaka sita ya Dk. Mwiyi ni kupatiwa skuli ya kisasa.

‘’Kuanzia mwezi na Januari mwaka jana, tumeshahamia rasmi, maana samani zote na vifaa vya sayansi navyo viemshawekwa, kilichobakia ni kufanyakazi kwa bidii,’’anasema.

Maana idadi ya vyumba walivyonavyo, sasa kila chumba kimoja ni wastani wa anafunzi 45, kama inavyotaka sera za kimataifa.

Juma Ramadhan Haji ni mwanafunzi wanaosoma skuli ya Konde, wanasema sasa wamefurahia kuingia ndani skuli ya kisasa.

‘’Tunayafurahia mno matunda ya Dk. Mwinyi kwetu, sasa kilichobakia ni kuongezea idadi ya waalimu wa sayansi tu,’’anasema.

UJENZI WA SKULI HIYO

Skuli hiyo yenye ghorofa tatu, ina madarasa 42, yenye uwezo wa kusomewa na wanafunzi 1,890 wastani wa wanafunzi 45 kwa kila darasa moja.

Inazo ofisi nne za waalimu, ofisi ya Mwalimu Mkuu, ukumbi wa mkutano, vyoo 52, maabara mbili za sayansi, chumba cha TEHAMA, ushauri nasaha pamoja na maktaba moja na kugharimu shilingi bilioni 6.2.

              Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...