Skip to main content

LUGHA CHAFU ZA WAZAZI KWA WATOTO, ZINAVYOWARUGIA MIFUMO YAO YA MAISHA

 


NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

MALEZI bora na makuzi ya mtoto, ni jambo  muhimu kwa maendeleo yake,kimwili na kiakili.

Hili linajumuisha huduma zote muhimu anazostahili kupewa mtoto, kuanzia miaka 0 hadi 8, ili kumuwezesha kukuwa na kufikia utimilifu wake.

Ikiwa ni kimwili, kiakili, kijamii, kihisia na kimaadili, ilikushiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa na kuyamudu mazingirayake.

Mara nyingi ni rahisi kupata haya yote, kutoka kwa wazazi au walezi,lakini wengi wao husahau kwamba matumizi ya lugha nzuri kwa watoto,inamchango mkubwa katika ustawi wao.

Na zipo sheria zinazopinga ukatili wa aina zote dhidi ya watoto, kwamsingi kwamba malezi bora kwa mtoto, ndio msingi imara kwa makuzi yake.

Mfano, Mkataba wa kimataifa wa haki za watoto duniani (Conventionoftherightsofthechildren) wa mwaka 1989, ambao umeanza kutumikarasmi mwaka 1990.

Ibara yake ya 19 inasisitiza, kuwa‘nchi wanachama kuhakikishawanakuwa na sheria nzuri zitakazo mlinda mtoto juu ya aina zote zaudhalilishaji’.

“Nchi wanachama zihakikishe zinakuwa na sheria nzuri zitakazo mlindamtoto juu ya aina zote za udhalilishaji, uwe wa kimwili au kiakili,kujeruhiwa, kudharauliwa, kutengwa au kudhulumiwa” inaeleza sehemu yamkataba huo.

Mkataba  wa haki na Ustawi wa watoto wa Afrika  wa mwaka 1999,kifungu cha 19 kinasisitiza kila mtoto anayo haki ya kufurahia nakunufaika na malezi bora ya wazazi, na ana haki ya kulindwa.



Na Sheria ya Watoto Zanzibar , namba  6 ya  2011, kifungu cha 15kinasisitiza kuwa, ‘mtu yeyote ambaeanamlea mtoto, mwangalizi wa mtoto asimfanyie au kuruhusu mtu yeyotekumfanyia mtoto matendo mabaya”.

Hii ni pamoja na kutomdharau, kumtelekeza kwa namna ambayoitasababisha kumuathiri mtoto huyo kimwili au kiakili, na atakaefanyahivyo, atakuwa amefanya kosa.

Bado wapo wazazi au walezi, hutumialugha na maneno mabaya na yenye kuumiza wakati wa kufundisha aukukanya.

Muda mwingine hufanya hivyo bila kujua kwamba ni tatizo katika ukuaji wa mtoto.

Eneo jingine, ni kuwa utafiti uliofanywa na taasisi ya ‘Words Matter Charity ya UK’,mwaka 2023unaonyesha kwamba, sentensi tano mbaya na zenye athari za muda mrefuzinazotumiwa mara kwa mara na wazazi na walezi.

Ukaonesha maneno kama “hunamaana hutumiwa na wazazi na walezi kwa watoto wao kwa asilimu 59, maneno mingine utafiti ukaeleza kuwa, “wewe ni mjinga kwa asilimia 56”.



Ukaenda mabali zaidi utafiti huo na kulitaja maneno “huwezi kufanya kituchochote vizuri kwa asilimia 52, ‘’hunathamani yeyote kwa asilinmi 48 na ‘naona aibu kwaajili yako huwa kwa asilimia 48.

Huku utafiti ukisisitiza kwamba,  maneno yanaweza kujenga au kubomoamaisha ya mtoto, kwa kiasi kikubwa.

SIMULIZI ZA WATOTO

Salum (13 sio jina lake rasmi) anahadithia, wakati yupo darasa la tano, mwenyekiti wa kamati ya skuli yao, alimsimamisha mbele ya darasa kwa ajili ya  kumfahamisha, ingawa maneno alioitumia hayakua mazuri.

Anasema japo miaka miwili imepita sasa, lakini ni maneno yanayomuumiza kama alitamkiwa jana.

Fatma (15 si jana halisi) anaeleza aliwahi kutamkiwa maneno mabaya, makali na yenye kuumiza na  babayake mzazi, ambayo wamebaki akilini mwake hadi leo,kwa kosa la kutokwenda skuli moja.



Watu watatu kati ya watano waliozungumza na mwandishi wa habari hizi, walionyesha kuguswa moja kwa moja, na matukio haya, na kuonyesha watu wao wa karibu ndio wanaohusika katika hili.

DINI ZINASEMAJE?

Sheikh Said Ahmed anasema katika dini ya Kiislamu matumizi ya maneno ya busara, upole na hekima ni msingi mkuu wa malezi na makuzi ya mtoto.

Anafahamisha, hili limo katika Qur-an tukufu sura ya 31:12-19, kupitia kisa cha Luqman alipomshauri mwanawe, ambapo alitumia maneno ya upendo na yenye kuelimisha, yakionyesha umuhimu wa mazungumzo ya busara ili mtoto aelewe kwanini jambo fulani ni baya.

Hata Mchungaji Samuel Maganga anasema Bibilia inafundisha kua, maneno ya upole na busara hujenga tabia njema na kuondoa chuki na maneno makali yanaweza kuumiza na kuleta uasi.

Akinukuu mstari wa bibilia anasema “Neno lolote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, isipokua linalofaa”.

JE SABABU NI ZIPI?

Salum Abdallah Suleiman mzazi miaka 70, anasema, mila, tamaduni nadesturi zilizopo katika jamii ni miongoni mwa sababu, zinazopelekeahali hiyo.

Anasema, jamii imejengeka kwamba mzazi, mlezi au yeyote mwenye umrikumzidi mwingine, anahaki ya kuzungumza nae kwa namna yeyote, aitakayo isiyo umiiza akili au mwili.



Jokha Ame Makame mzazi miaka 24 anasema, mzazi kukosa elimu ya malezibora, inaweza kuwa ni miongoni mwa sababu ya hiyo.

Hata Mohamed Amour (67) anasema, historia ya ukuaji wa mzazi ni moja yasababu, zinazopelekea hali hiyo.

Anaeleza kwamba, wengi wa wazazi wenye tabia hiyo, walikulia mazingirahayo hayo, hivyo wamekuwa wakiamini kwamba, maneno mabaya ndio malezi.

Nae Salama Abdallah Othman Mratibu wanawake na watoto shehia yaMjimbini anaeleza, kutokujuwa athari za matumizi ya maneno mabaya kwawatoto, ndio sababu ya hayo.

MITANDAO YA KIJAMII IMERIPOTI NINI

Kwa mujibu wa mitandao ya kijamii takriban asilimia 33 hadi 40 ya watoto duniani kote hukabiliwa na ukatili wa maneno.

Aidha mitandao inaeleza kua watoto wa rika zote kuanzia wachanga hadi vijana baleghe , wanaathiriwa na waneno machafu, ingawa namna wanavyoyapokea hutofautiana kulingana na umri wao.

Aidha mitandao imeripoti uwepo wa athari za kisaikolojia kwa watoto wanaokulia mazingira ya kutolewa maneno machafu, ambapo kuna asilimia 64 ya uwezekano wa kupata afya duni ya akili ukubwani.

ATHARI ZAKE NI ZIPI?

Mtaalamu wa saikolojia Ahmada Salum Juma anasema, zipo athari kazaa, ikiwa ni pamoja na kutokujiaminikwa mtoto.

Anasisitiza kua inaweza kupelekea kujitenga pamoja na kupunguzaukaribu baina yake na mzazi au mlezi, kwani maneno hayo, humfanya akatetamaa.

Afisa ustawi wa jamii wilaya ya Wete Salma Saleh Hamad anasema,hali hiyo inaweza kuathiri ustawi wa jamii wa mtoto hadu utuuzima wake.

"Mtoto ambaye anajisikia kukataliwa au kudharauliwa, anaweza kuanzakuonyesha hasira au kitendo chochote, kwa njia isiyofaa ili ajilinde mwenyewe", anafafanua.

NINI KIFANYIKE?

Mzazi Salim Abdallah Suleiman anawasihi wazazi wenzake, kuhakikishawanatumia maneno chanya wakati wa kukanya au kuelekeza watoto wao.

Afisa ustawi wa jamii wilaya ya Wete, Salma Saleh Hamad anasema, ni vizuri wazazi nawalezi kutumia elimu ya malezi bora, hekima na busara hasa katikakauli zao.

Mwenyekiti wa watoto Bodi ya ushauri Taifa Khamis Abdallah Mbaroukanasema, wazazi na walezi wanapaswa kuepuka matumizi ya maneno na sentensi zisizofaa.



Naibu waziri wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na WatotoZawadi Amour Nassor anasema, malezi mazuri kwa mtoto, ndio msingiimara kwa maisha yake ya baadae.

TAMWA-Zanzibar ni asasi ya kiraia inayopambana na aina zote za ukatilidhidi ya wanawake na watoto, afisa programu ya kupambana na matukiohayo Asia Hakim Makame, anawasisitiza waandishi wa habari kuelimisha jamii athari za ainazote za udhalilishaji.

Anasema kuwa anaona hatua hiyo itawasaidia kuongeza uwelewa wakupambana na matukio hayo.

MWISHO.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...