NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@
IDARA ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar,
imemkabidhi ripoti ya awali, ya kampeni ya msaada wakisheria ya Mama Samia,
mara baada ya kumalizika kwa kambi ya siku 10 ndani ya mkoa huo.
Kabla ya kukabidhi kwa ripoti hiyo, Mkuu wa Idara hiyo Pemba
Bakari Omar Ali, alipongeza ushirikiano alioupata kutoka kwa maafisa wa taasisi
mbali mbali za serikali, wakati wote wa kampeni hiyo.
Alisema, katika kampeni hiyo, waliwatumia maafisa wa
kamisheni ya wakfu, ardhi, mawakili wa serikali, makadhi, maafisa ustawi,
matukio ya kijamii pamoja na waandishi wa habari.
Alieleza kuwa, maafisa hao walisaidia kwa kiasi kikubwa, kupokea
malalamiko na kuyapatia ufumbuzi papo hapo na mingine kuziandikia barua taasisi
husika.
Alifahamisha kuwa, kampeni hiyo ambayo ilikuwa katika mifumo
miwili, moja ni kuwafuata wanafunzi wa skuli, vyuo vya elimu ya juu pamoja na
mikutano ya jamii.
‘’Tulijigawa timu mbili, moja wilaya ya Micheweni na nyingine
Wete, ambapo maafisa kadhaa walikuwa wanakutana na makundi mbali mbali ndani ya
jamii, na kuyapa elimu na ushauri wa kisheria bure,’’alifafanua.
Aidha Mkuu huyo wa Divisheni ya Idara ya Katiba na Msaada wa
Kisheria Pemba, Bakar Omar Ali alisema, wakati hayo yakifanyika, timu nyingine
iliweka kambi katika eneo la Jamhuri Wete, kwa ajili kutoa huduma papo hapo.
Alisema, wapo wananchi ambao walikuwa hawajapata nyaraka
kama vile vyeti vya kuzaliwa, vitambulisho vya ukaazi, usaliji wa vyeti vya
ndoa na utatuzi wa migogoro mingine.
‘’Mheshimiwa Mkuu wa mkoa, kambi yetu iliwasaidia mno wananchi,
maana hata mawakili, wanasheria, makadhi, watendaji wa mwanasheria mkuu, walitoa
huduma bila ya malipo kwa wananchi,’’alifafanua.
Mapema Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba, Salama Mbarouk
Khatib, alisema ataisoma ripoti hiyo, na kama kuna jambo hajalifahamu, atawasiliana
na Idara hiyo.
Alisema, wazo la Mama Samia kuwa na kampeni hiyo, imeasaidia
kwa kiasi kikubwa, na kuongeza upatikanaji haki zao mbali mbali.
Alieleza kuwa, kampeni hiyo ni sehemu ya maono ya Mama
Samia, katika kuhakikisha wanawake, watoto, watu wenye ulemavu na watu wingine
wasiojiweza wanapata haki zao mbali mbali.
‘’Lakini hata suala la kuwafikia wanafunzi na wanajamii kwa
mikutano ya elimu, ushauri na msaasa wa kisheri iliwaamsha wanajamii, kujua
haki na wajibu wao kisheria,’’alisema.
Mapema Mratibu wa kampeni hiyo wilaya ya Micheweni Khamis
Bakar Aman, wakati akimkabidhi ripoti hiyo Mkuu wa wilaya ya Micheweni Khatiba
Juma Mjaja, alisema changamoto kubwa, walioibua ni utelekezaji wa wanawake na
watoto.
Alisema, walipokea kesi kadhaa ambazo wanawake
wanawalalamikia waume zao, walioko dago nje ya Pemba, wakishindwa, kupeleka
huduma kwa familia zao.
‘’Ijapokuwa tulibaini changamoto nyingine, lakini hili la wanawake
kulilia huduma kwa waume zao, ndio linaongoza, hivyo ni sehemu kwa wilaya kulifanyia
kazi,’’alifafanua.
Mkuu wa wilaya ya Micheweni Khatib Juma Mjaja, alisema kazi
iliyofanywa na Idara hiyo kusimamia kampeni ya Mama Samia, ni nzuri.
Alisema, anaamini sasa wapo wananchi waliopata uwelewa wa
wajibu na haki zao mbalimbali, kama vile umuhimu wa vyeti vya kuzaliwa, usajili
wa vyeti vya ndoa, kifo na haki za wanawake na watoto.
Wakati huo huo Mratibu wa Kampeni hiyo wilaya kwa wilaya ya Wete
Moza Rajab Baraka, alimkabidhi ripoti kama hiyo Mkuu wa wilaya ya Wete na
Mkurugenzi baraza la mji wa Wete, na kuwampa shukran kwa misaada yao.
Alisema, ushauri, maelekezo na mbinu walizotoa zilisaidia
mno kuhakikisha kampeni hiyo ya siku 10, inakwenda vizuri na kumalizika kwa
wakati.
Kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia, kwa mkoa wa
kaskazini Pemba, iliendelea tena kuanzia Mei 31, na kumalizika Juni 9, mwaka
huu.
Mwisho
Comments
Post a Comment