Skip to main content

MJIMBINI MKOANI MAJI 'FULL KUJIACHIA' WAIPA TANO ZAWA

 



NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

WANANCHI shehia ya Mjimbini wilaya ya Mkoani Pemba, wameipongeza Serikali kupitia Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA), kwa upatikanaji wa maji safi na salama shehiani mwao.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Juni 20, 2025 mwananchi  Saumu Issa Mohamed alisema, huduma ya upatikanaji wa maji safi na salama kijijini hapo, kwa sasa ni yauhakika jambo linalotoa faraja kwao.

Alisema mafanikio hayo ni muhimu kwao, kutokana na umuhimu wa huduma hiyo katika maisha yao ya kila siku, hivyo wameipongeza serikali kwa kuwahakikishia  upatikanaji wa huduma hio saa ishirini na nne.

Mwananchi Suleiman Muhammed Makame kutoka shehiani hapo alisema, kwa miaka zaidi ya saba iliopita,  iliwalazimu kutumia maji ya mito na visima ambayo hayakua safi na salama, kwa matumizi ya binaadamu, hivyo upatikanaji wa huduma hiyo imekua suluhu ya tatizo  hilo.

Nao Zahra Hafidh Juma na Hafidh Khatib Faki, walisema, upatikanaji wa huduma hio ni utekelezaji wa ahadi ya serikali ya awamu ya nane, ya kuwasogezea karibu wananchi wake huduma zote muhimu za kijamii, ikiwemo ya maji safi na salama.

Hivyo waliongeza kwamba ili kuungamkono jitihada hizo watahakikisha wanatunza miundombinu hio kwa maslahi ya sasa na baadae.

"Serikali imefanya jitihada ya kutatua changamoto ya ukosefu wa huduma ya maji safi na salama, iliokua ikitukabili, na kwa  sasa tunapata ipasavyo, hivyo   tutahakikisha tunatunza miundo mbinu hii kwa matumizi ya sasa na baadae," walisema.

Kwa upande wake sheha wa Mjimbini wilayani humo, Faida Haji Khatib, alisema serkali imekua ikichukua jitihada mbalimbali, ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma zote za kijamii.

Alieleza kuwa, hivyo ni muhimu kwa wananchi kuungamkono jitihada hizo, ili kufikia lengo la serikali na wananchi kupata huduma za kuendesha maisha yao.

Alisema kua, niwajibu wa wananchi wa kijiji hicho kutumia maji kwa uangalifu, kwa kuepuka kuyamwaga ovyo, pamoja na kuchangia kwa wakati, ili kuiwezesha huduma hio kudumu kwa mda mrefu.

Hata hivyo aliwaomba viongozi wa jimbo hilo, pamoja  na wadau wingine wa maendeleo, kuwapatia tanki lenye uwezo wa kuhifadhi kiwango kikubwa cha maji, ili kujihakikishia zaidi huduma hiyo hata kipindi ya umeme unapokazimika.

" Kwasasa tunakisima chenye maji mengi, ambayo ni toshelevu kwa shehia yetu, ingawa  bado kuna  hofu  kwa wananchi,  kutokana na kutokua na tenki la kuhifadhia maji,’’alifafanua.

Nae Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Maji ZAWA Pemba Suleiman Anas Massoud  alisema, hatua hiyo ni miongoni mwa mikakati ya serikali, ya kuhakikisha upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi wote.



Shehia ya Mjimbini inawakaazi 3,210 wanaume wakiwa na 1,558 na wanawake 1,652 ikiwa na zaidi ya vitongoji vinne, na ni miongoni mwa shehia zilizonufaika na mradi mkubwa wa uchimbaji wa visima, kupitia mradi wa COVID 19.

 

                                                         MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...