Skip to main content

MTUHUMIWA, WAKILI WAKE WAINGIA MITINI TUHUMA DAWA ZA KULEVYA

                                                           


NA MARYAM SALIM, PEMBA@@@@

KUTOKUFIKA kwa mtuhumiwa Zaid Mussa Zaid miaka (46) mkaazi wa Machomanne pamoja na wakili wake katika mahakama ya Mkoa ‘C’ Chake Chake Pemba, kumepelekea shauri hilo kuahirishwa mahakamani hapo  na kupangwa tarehe nyengine kwa ajili ya utetezi.

 

Mapema Mwendesha mashitaka akiwakilisha Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka wa serikali, Kheir Hassan Omar, aliieleza mahkama hiyo mbele ya Hakimu Hamisuu Saadun Makanjira kwamba, shauri hilo lilifikishwa katika mahakama hiyo, kwa ajili ya utetezi ingawa mtuhumiwa na wakili wake, hawakuhudhuria.

 

"Mheshimiwa Hakimu, shauri lilimefikishwa mahakamani kwa ajili ya kusikilizwa utetezi, ambalo linamkabili mtuhumiwa Zaid Mussa Zaid, anaedaiwa kupatikana na dawa za kulevya.

 

"Ingawa mtuhumiwa na wakili wake, hawakuja mahakamani na hatuna taarifa zao, hivyo tunaomba mahkama kutokana na shauri hili, liahirishwe na lipangwe tarehe nyingine kwa ajili ya kusikilizwa utetezi," alidai.

 

Baada ya ombi hilo la kuahirishwa kutoka kwa Mwendesha Mashitaka, Hakimu huyo hakuwa na pingamizi, hivyo aliliahirisha shauri hilo na kutaka lirudi tena mahakamani hapo Juni 25 mwaka huu, kwa utetezi.

 

Aidha Hakimu huyo, pamoja na mtuhumiwa huyo alitoa onyo kwa wakili wa matuhumiwa nae aitwe na wafike siku hiyo, ili taratibu nyingine ziendelee, za shauri hilo.

 

Kabla ya kuahirishwa kwa shauri Hati ya mashitaka ya mtuhumiwa inadai kwamba, mtuhumiwa anakabiliwa na kosa la kupatikana na dawa za kulevya.

 

Ilidaiwa kwamba mnamo Agosti 31 mwaka 2024, majira ya saa 6:0 mchana shehia ya Wawi, bila halali, alipatikana na kete 89 zinazosadikiwa kua ni za dawa za kulevya aina ya Heroin, zikiwa na uzito wa gramu 1.0947, jambo ambalo ni kosa kisheria.

 Aidha hati hiyo ya mashitaka ya mtuhumiwa ilielezaa kuwa, kupatikana na dawa za kulevya ni kinyume na kifungu cha 23(1) (a) (3) cha sheria nambari 8 ya mwaka 2021, Sheria ya Mamlaka ya Udhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Zanzibar, sheria ya Zanzibar.

 

                   MWISHO.

Comments