Skip to main content

MICHEWENI WAONYESHWA NJIA KUEPUKA MATUMBO YA KUHARISHA

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANANCHI wa Halmashauri ya wilaya ya Micheweni Pemba, wametakiwa kurejea utamaduni wao wa kuweka mazingira yao safi na salama, ili kujikinga na magonjwa ya kuharisha, ambayo chanzo chake kikuu ni uchafu.

Ushauri huo umetolewa jana na Mwanasheria wa Halmashauri hiyo, Rukia Khamis Haji, alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hii, kufuatia uwepo wa tishio la matumbo ya kuharisha, katika baadhi ya maeneo kisiwani Pemba.

Alisema, suala la usafi haipendezi kuona wananchi wanalifanya kwa shindikizo la Halmshauri, bali wenyewe waamue kujielekeza kwenye usafi, ili kujihakikisha usalama wao.

Alieleza kuwa, utamaduni wa kuweka mazingira safi na salama, ni vyema kwa wananchi wa Halmashauri hiyo, ikawa ndio utamaduni wao endelevu, kwani kinyume chake ni kujiangamiza.

‘’Hichi ni kipindi cha mvua na kinakuwa na changamoto zake, ikiwemo kusambaa kwa uchafu kutoka sehemu moja kwenda nyingine, hivyo suala la usafi lazima liwe kipaumbele chetu,’’alieleza.

Katika hatua nyingine Mwanasheria huyo wa Halmashauri ya wilaya ya Micheweni Rukia Khamis Haji, amewakumbusha wafanyabiashara nao kuzihifadhi vyema biashara zao, ili zisishambuliwe na wadudu.

‘’Tunajua kuwa, biashara kama mandazi, visheti, mikate, samaki wa kukaanga na matunda, huwa ni rahisi kuingiliwa na nzi, ambao kwa njia moja ama nyingine, hubeba vimelea vya magonjwa,’’alifafanua.



Hata hivyo, amewakumbusha wafanyabishara hao, kuendelea kulipa kodi zao kwa wakati, ili kuiwezesha Halmashauri hiyo na serikali kuu, kuendelea kuwaletea maendeleo wananchi.

Baadhi ya wananchi wa wilaya ya Micheweni, akiwemo Huda Hamad Simba, alisema bado wapo baadhi ya wananchi, ambao wamekuwa wakitiririsha maji taka ovyo.

‘’Watu bado elimu haijawafikia na wingine ni wakaidi wa kuchimba mashimo maalum ya kuhifadhia maji taka, kwani yakitiririka huwa chanzo cha magonjwa kusambaa,’’alifafanua.

Aisha Omar Mjaka, alisema ni vyema kukaandaliwa adhabu na faini nyingine, pindi akijitokeza wananchi wenzao, kukaidi amri ya kufanya usafi.

Hidaya Haji Khamis na mwenzake Mwamize Kombo Juma, walisema usafi katika baadhi ya shehia zao, umekuwa ukisua sua, kwakule wananchi kukosa usimamizi.

Juzi, Mkurugenzi wa Manispaa ya Chake chake Shida Kombo Mohamed, alifanya ziara ya kushtukia katika viwanjwa vya sikukuu na kupiga marufuku uuzaji wa juisi.



Hata hivyo, aliwahimiza wafanyabiashara hao, kuzihifadhi vyema biashara zao, kwa kuzitia kwenye masunduku ya vioo, ili kuwakinga wateja wao na uwezekano wa kupata magonjwa.

Afisa Mdhamini wziara ya Afya Khamis Bilali Ali, aliwakumbusha wananchi, kuyasafisha mazingira waliyoyazunguruka, sambamba na kuchemsha maji ya kunywa.

              Mwisho  

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...