Skip to main content

MAJIMBO YA UCHAGUZI CHINA HAYASHIKIKI KWA WANAWAKE, RAIS WAO AENDELEA KUWEKA MAZINGIRA RAFIKI

 


NA HAJI NASSOR

NIPO, jiji la Beijing linalopatikana takriban saa 12, kutoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Zanzibar, kwa usafiri wa anga.

Jiji hili ni moja kati ya majiji manne yayounda taifa la China, likiwemo pia lile la Shanghai, ingawa Beijing ndio mji mkuu.

Lenyewe limezungurukwa na milima mikubwa kwa upande wa magaribi, ingawa kusini mashariki na kaskazini mwa jiji hilo, linaujirani na bahari iitwayo Bohai.

Jiji hili, lina ukubwa wa skweya kilomita 16,410, ambapo hadi mwishoni mwa mwaka 2023, lilikuwa na wakaazi milioni 21.858.

Kati yao hao, wanaoishi ndani ya mji husika wa kudumu ni watu milioni 19.198, sawa na asilimia 87.8, huku ambao sio wa waakzi wa kudumu ni milioni 8.204 sawa na asilimia 12.2.

Mpaka mwezi April 2023, Beijing pekee inazo wilaya 16 ‘municipal districs’ ikiwemo ya Xichenga, Chaoyang, Fengatai, Shijingshan, Hiaidian, Miyun pamoja na wilaya ya Yanging.  

Ukingia ndani ya jiji la Beijing, mara zote utakaribishwa na mazingira mazuri ya kijani kibichi kinachotawala pembezoni mwa barabara kuu, inayotokea uwanja wa ndege wa kimataifa wa China.

Uwingi wa watu na gari, serikali ya China iliamua kuzijenga kama njugu barabara za juu ‘fly over’, kusudi kupunguza kama sio kuondosha kabisa, foleni.

Ingawa kwa taifa lenyewe la China, linaundwa na maeneo makubwa maalum  mawili ‘special administration’ likwemo la mji wa Macao.

ELIMU KWA MATOTO WA KIKE CHINA

Kwa mujibu wa msomi nguli wa historia ya China Dk. Sun Jiwen, anasema serikali ya rais wa sasa wa taifa hilo Xi Jinping, amefanikiwa kuweka mazingira ya kielimu yanayowawezesha watoto kusoma.

Akasema, watoto wa wakike wamekuwa mastari wa mbele kuliko wa kiume, kuanzia ngazi ya elimu ya msingi hadi ile ya vyuo vikuu.

Akatoa mfano kuwa, kila mwaka kila wanafunzi 100, wanaomaliza elimu ya vyuo vikuu, kwa shahada ya kwanza watoto wa kike huwa na 52, na 48 huwa ni wanaume.



Vivyo hivyo kwa elimu digree ya kwanza na kuendelea, kwa mwaka watoto wa kike huwa 48, idadi ambayo wamepitwa kidogo mno na wale wa kiume.

HALI IKOJE KWENYE BUNGE LA CHINA

Kwenye taifa la china, linaloundwa na majimbo makubwa 23 yanayobeba wapiga kura zaidi ya bilioni 1.5, ingawa bado wanawake wanaogombea, huangushwa.



Dk. Sun Jiwen nilipomuuliza sababu ya idadi ya wanawake kuwahi kumaliza kwa wingi vyuo vikuu, ingawa Bungeni kuwa wachache, anasema bado hawajaaminika.

‘’Bado wapiga kura wanaume hawajawaamini wagombea wanawake, na ndio maana kila wabunge 100, wanawake ni sawa na 26 pekee,’’anasema.

JUHUDI ZA SERIKALI YA CHINA

Profesa He Wenping, anasema moja ni kwa rais aliyepo sasa kuandaa mazingira ya kuwainua wanawake, ili waweze kugombea na kuchukua nafasi ndani ya Bunge la china.

‘’Kwa mfano wanawezeshwa kielimu, mikopo ya kukukuza pato lao, wafikirie kugombea na kupambana na wanaume majimboni,’’anasema.

Jingine ipo mikopo ya kujiendeleza elimu ya juu, maana imegundulika wengi wanaogombea wamekosa kujiamini sababu, ikiwa ni kukosa elimu ya juu.

Akifungua mafunzo ya siku 20 kwa waandishi wa habari wa Zambia, Gambia, Ethiopia, Tanzania, Kenya na China, Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Mawasiliano ‘CICG’ Han Likiang, anasema bado vyombo vya habari vinakazi ya ziada.



‘’Wanawake ni sehemu ya taifa, ni sehemu ya nguvu kazi, ni sehemu ya familia ni sehemu ya viongozi, haya yanahitajika kufafanuliwa na waandishi wa habari,’’anasema.

WANAWAKE WENYEWE WA CHINA

Young Jujian, anasema wamekuwa wakifanyavyema kushiriki kampeni, chaguzi mbali mbali na kuwaunga mkono wagombea wanaume, ingawa inapofika wakati wao kuomba nafasi, huangushwa.

Hei Ujun anasema, wamekuwa wachache ndani ya bunge la China, kwani wapo wanawake wamekuwa wakiwafanyia uadui wa kidemokrasia wakati mwingine.

‘’Lakini hii tabua ipo duniani kote, kuanzia nchi zilizoendelea na hata zilizoendelea, maana wanawake hutiwa sumu na baadhi ya wanaume na kukosa kura,’’anasema.

WANAUME WA CHINA

Hu Iyain anasema, histori ya taifa lao tokea utawala wa rais wa kwanza Mwenyekiti Mao Dzodung, iliwasahaulisha wanaume kuwapa nafasi wanawake.



‘’Kwa sasa hali inaendelea kupanda juu, maa asilimia 26 ndani ya Bunge la China ni wanawake, hali ambayo kabla haikuwa ikiridhisha,’’anasema.

Hey Idong, anasema kidogo kidogo wapiga kura wameanza kuwazoea wagombea wanawake, jambo ambalo awali lililonekana kama kituko.

Sun Lyu, anakiri kuwa wapo baadhi ya wapiga kura wamekuwa na uwelewa taofauti wanapoona mgombea mwanamke, na ndio maana, wapo wanaoangushwa hata kabla ya uchaguzi mkuu.

UZOEFU KATIKA MAENEO MINGINE

Zanzibar, kwa mfano katika kisiwa cha Pemba yapo majimbo 18 ya uchaguzi, ingawa wanawake wameng’ara katika majimbo manne.

Ni jimbo la Chambani, Gando, Wete na pamoja na jimbo Konde wote kwa nafasi ya Uwakilishi huku wanaume wakiendelea kushikilia majimbo 14, ingawa kwa nafasi ya ubunge ni yote.

WANAHARAKATI

Dk. Mzuri Issa Ali anayekiongoza Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar anasema, wanategemea mno, kuona uchaguzi wa mwaka huu, wanawake wanachukua hatamu ya uongozi.

‘’Tunaendelea kuendesha mradi wa kuwahamasisha wanawake na uongozi, kupitia vyombo vya habari na wapo zaidi ya 20 kwa Unguja na Pemba, waliokwisha onesha nia, sasa ni kazi ya wapiga kura kuwaamini,’’anasema.

Sifuni Ali Haji kutoka Mtandao wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’, analalamikia vyama kutowaunga mkono wanawake, wanapoonesha azma ya kugombea.

VYAMA VYA SIASA

Mwenyekiti wa chama cha ACT-Wazalendo Othman Massoud, anasema wanawake ndio jeshi kubwa ndani vyama, hivyo ni wakati na wao kugombea, badala ya kutegemea viti maalum.

‘’Viti vya wanawake vinaweza kuondoka siku moja, hivyo lazima wanawake wajipange kisaikolojia na kuingia majimboni, maana katiba haijawakataa,’’anasema.

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa kusini Pemba, Yussuf Ali Juma, anasema chama hicho, kimekuwa na utaratibu wa kuwajenga wanawake kiuongozi, kuanzia ngazi ya shina hadi taifa.

‘’Ndio maana hata wawakilishi hao wanne waliofuzu majimboni ni kutoka CCM, ni baada ya kuwawezesha ngazi ya shina na sasa wako taifa,’’anasema.

Rais wa sasa Jamhri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan, anasema lazima vikwazo viondolewe na wanaume na kuwaachia wanawake kupata uongozi.

Wakati akiadhimisha miaka mwili ya uongozi wake ndani ya ukumbi wa zamani wa baraza la Wawakilishi Wete Pemba, Rais wa Zanzibar Dk. Mwinyi, aliahidi kuendelea kuwapa nafasi wanawake.

‘’Ijapokuwa mawaziri na makatibu wakuu wote niliowateua wanafanya vuzri, lakini ukweli ni kwamba wanawake wako juu  zaidi ya wanaume,’’alisema.

Mwisho 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...