Skip to main content

WANANCHI MJANANZA WATAKA OFISI YA ‘ZLSC’ IHAMIE KWAO

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANANCHI wa shehia ya Wingwi Mjananza wilaya ya Wete Pemba, wamekishauri Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ kuhamishia ofisi kwenye shehia yao, ili kila wanapokuwa na changamoto zao za kisheria wawe karibu nao.

Walisema, huduma walizopewa za ushauri wa kisheria bila ya malipo, zimewavutia na kuona ipo haja kwa sasa, kwa kituo hicho kujenga ofisi shehiani mwao.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi leo April 18, 2025 mara baada ya kufungwa kwa kambi ya siku tatu ya utoaji elimu, ushauri na msaada wa kisheria, walisema wanatamani ZLSC ijenga ofisini eneo la Mjananza.

Walisema kuwa, wengi wao walikuwa hawana uwelewa wa utaratibu wa kufuatilia nyaraka kama za vyeti vya ndoa, talaka, vyeti vya kuzaliwa, vitambulisho jambao ambalo wamelipata ndani ya kambi hiyo.

Mwananchi Salim Hamad Faki, alishauri kuwa, ni vyema kwa ZLSC ikawa na ofisini ngazi ya shehia, ili kupunguzia dhiki za wananchi kuwafuata mjini wanasheria, wanapokuwa na changamoto za kisheria.

Nae Fatma Mussa Iddi, alisema kama ikiwezekana ni vyema kituo cha Huduma za sheria, kikajenga ofisi shehia ya Mjananza, hasa kutokana na aina yake ya huduma inayotoa.

‘’Kwa mfano mimi nilifuata kupata utaratibu wa kupata chti cha ndoa, maana nimeolewa huu sasa ni mwaka wa nane, lakini sijapata cheti,’’alifafanua.

Nae Mwajuma Himid Mjaka, alisema kupitia kambi hiyo ya siku tatu, amepata mwelekeo wa kwenda kuwashawishi kaka zake, kuharakisha mirathi.



Akizungumza katika ufungaji wa kambi hiyo, skuli ya Msingi Mjananza, Afisa Miradi wa ‘ZLSC’ Beny Louis Mlingi, alisema walifanikiwa kuwapata wananchi 304, wakiwemo wanawake 295 na wanaume tisa (9).



Alisema wingi wa wananchi waliowapokea walikuwa wakilalamikia ukosefu wa gharama za vyeti vya kuzaliwa, na baadhi yao wakikosa vyeti vya ndoa kwa zaidi ya miaka 25 sasa.

‘’Kwanza niwashukuru wananchi wa shehi ya Mjananza kwa kufuata wito wetu, na tumeona ipo shida kwa wananchi, ingawa wengi wao wanaliwa na umaskini wa kipato,’’alifafanua..

Nae Afisa Sheria wa ‘ZLSC’ Asha Maulid Khamis, alisema muitikio mkubwa wa wananchi, ni ishara kuwa msaada wa kisheria unahitajika kwa jamii.

‘’Kwa vile kila jimbo na baadhi ya shehia wapo wasaidizi wa sheria, ni dalilili kuwa waongeze kasi ya kuwafikia wananchi, maana bado wanakabiliwa na changamaoto za elimu, ushauri na msaada wa kisheria,’’alifafanua.


Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’, kimeasisiwa mwaka 1992, kwa kutoa huduma za maktaba, kuwasomesha wasaidizi wa sheria na kutoa elimu, msaada na ushauri wa kisheria kwa wananchi bila ya malipo.

Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar, kimemaliza kambi ya siku sita kwa shehia za Uwandani wilaya ya Chake chake na Mjananza wilaya ya Wete, na kuwafikia wananchi 416.

Mwisho  

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...