Skip to main content

WADAU UANDAAJI MALIPO 'ZSSF' PEMBA TUMIENI MIFUMO KURAHISISHA TAARIFA

 


NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

AFISA Mdhamini Wizara ya Fedha na Mipango Pemba, Abdulwahab Said Abuu-bakar aliwataka wadau wanaohusika na uandaaji wa malipo ya michango katika mifumo ya Mfuko wa hifadhi ya jamii (ZSSF) kutumia mifumo hiyo kwa usahihi ili kurahisisha upatikanaji wa taarifa kwa wanachama wake.

Aliyasema hayo April 15, 2025 katika mkutano wa kuwajengea uwezo wadau hao uliofanyika katika ukumbi wa (ZSSF) Tibirinzi Chake Chake Pemba.

Alisema kumekua na malalamiko ya ucheleweshwaji wa upatikanaji wa mafao ya ustaafu kutoka kwa wanachama, yanayosababishwa na taasisi kushindwa kuweka kumbukumbu vizuri, katika mifumo hiyo.

Hivyo alisema ni vyema kwakila taasisi kuhakikisha inatimiza majukumu yake vizuri ili kupunguza malalamiko hayo kwa wastaafu wa serikali na taasisi binafsi.

"Ni vyema  taasisi zihakikishe  zinatimiza majukumu yake vizuri ili kupunguza malalamiko kutoka kwa wastaafu wa serikali na taasisi binafsi" alisema.

Alieleza kua  serikali imeandaa utaratibu wa kuwalipa wastaafu mafao yao ndani ya wiki mbili baada ya kustaafu, hivyo amewataka wadau hao kutumia vizuri  mifumo ya habari na mawasiliano ili kulifanikisha hilo.

Alisema mfuko wa hifadhi ya jamii Zanzibar (ZSSF) inatumia mitandao ya kijamii ili kurahisisha upatikanaji wa taarifa, hivyo amewaomba wadau hao kutumia mitandao hiyo pamoja na kushajihisha wengine kuitumia ili kuondoa changamoto ya ucheleweshwaji wa mafao kwa wanufaika.

Aidha aliipongeza (ZSSF) kwa kua na utaratibu wa kukutana na wadau hao mara kwa mara, ambayo ni hatua muhimu katika kuchochea maendeleo, huku akiwasihi kuendeleza utaratibu huo.



Akiwasilisha mada kuhusu umuhimu wa hifadhi ya jamii Afisa hifadhi ya jamii Pemba Said Omar Juma alisema,  Mfuko wa hifadhi ya jamii ni kwaajili ya watu wote wenye ajira rasmi na zisizo rasmi.

Alieleza kua hifadhi ya jamii inaumuhimu mkubwa kwa jamii kwani inamuhakikishia kipato mwanachama baada ya kustaafu pamoja na kutoa ulinzi wa kifedha kwa wanufaika.

Alisema ingawa kunachangamoto ya uelewa mdogo kwa wananchi, pamoja na uhaba wa mashirikiano kutoka kwa wananchi, lakini wamekua wakifanyajitihada mbali mbali ikiwemo kutoa elimu kwao.

Alisisitiza kua hifadhi ya jamii ni nguzo muhimu kwa maendeleo ya Taifa, hivyo ni wajibu wa serikali, taasisi binafsi na wananchi kuungamkono ili kuzidi kuimarika.

"Hifadhi ya jamii ni nguzo muhimu kwa maendeleo ya Taifa, hivyo ni wajibu wa kila mmoja wetu kuanzia  serikali, taasisi binafsi na wananchi kuungamkono ili uzidi kuimarika" alieleza.

Nae Afisa tehama wa ZSSF Pemba Madi Jafar Khamis alisema matumizi ya mifumo katika ukusanyaji wa taarifa itasaidia kuweka sawa kumbukumbu za fedha pamoja na kuhifadhi taarifa kwa usahihi na kwa wakati.

Akiwasilisha mada kuhusu fidia ya ajalikazini inayotolewa na( ZSSF) Ali Mtemani Hussen Afisa hifadhi ya jamii Pemba alisema, fidia hio ni haki ya msingi ya kila mwanachama atakaepata kadhia hii,  huku akisisitiza kua (ZSSF) ipo kwa ajili ya kustawisha jamii.

Kwaupande wake Kaimu Mkurugenzi ZSSF Pemba Msabah Massoud Msabah aliwataka wadau walioshiriki mafunzo hayo kuendelea kutumia mitandao ya mfuko huo kwa kutoa maoni na ushauri ili kuongeza ufanisi katika utendaji wao wa kazi.




Hatahivyo alitoa shukrani kwa wadau walioshiriki mafunzo hayo huku akiwaomba kuripoti changamoto zao ili kupatiwa ufumbuzi wa haraka.

Nae mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo Ali Talib Bakkar kutoka wizara ya Fedha na mipango, alitoa pongezi kwa  mfuko wa hifadhi ya jamii kwa kuwapatia mafunzo hayo, huku akiwataka wadau wengine kurahisisha upatikanaji wa taarifa muhimu ili wanachama wapate mafao yao kwa haraka.

   MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...