Skip to main content

NAOMBA: MKULIMA ALIYEJIKITA NA KILIMO MSITU, AELEZEA KILICHOMVUTIA



HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@

NI majira ya saa 4:00 asubuhi, nilipofika katika bonde la Kigawani kijiji cha Chwale Wilaya ya Wete Pemba, nikitokea Mkoani. 

Katika safari  hiyo niliyochukuwa muda usiopunguwa saa 1:30 kwa usafiri wa umma, nikiwa na lengo la kutaka kujuwa changamoto na maendeleo ya kilimo msitu ambacho kinalimwa shehiani humo.  

Ilikuwa ni safari yenye kheri kubwa, kwani kukutana na wakulima  wa kilimo msitu, ambao wameamuwa kujikita na kilimo hicho wakiwa na malengo ya kujikwamua kimaisha.

Pamoja na wakulima wengine kuzungumza nao  nilipata hamu na shauku kubwa ya kuzungumza na mkulima Naomba Shaaban Mbarouk, baada ya kumsikia kuwa alikotokea  hakuwa na hamu ya kujiingiza katika kilimo hicho. 

 Wala sikufanya ajizi nilimvuta pembeni, chini ya muembe huku upepo ukitupepea taratibu akiielezea makala haya, kinaga ubaga kuhusu kilimo hicho kilichomvutia hadi kujiingiza.  

Alijiingiza katika kilimo hicho, baada ya kupata mafunzo kutoka  jumuiya ya uhifadhi wa misitu, yaliyomuonesha njia na kumpa uhakika wa kuendesha maisha. 

Anasema ni faraja kubwa aliyonayo kwa kuweza kuingia katika kilimo msitu, kwani ana uhakika wa kuendesha maisha yake, na kuacha utegemezi. 

 "Huko nilikotokea sikuwa nikilima na hata lengo la kuanza kulima sikuwa nalo, ila sasa siwezi kukiacha.

Anasema  na TAMWA – Zanzibar  nao walimzidisha hamasa ya kujikita na kilimo hicho, baada ya kuwapa mafunzo ya kuwajengea uwezo.

 Anasema TAMWA imefanya jambo moja zuri, kuwapa wakulima elimu na kuwawezesha kuzungumza na vyombo vya  habari, kwani sasa wataweza kutowa changamoto na mategemeo yao.

Kumbe Naomna kabla ya kuingia katika kilimo hicho, maisha yake yalikuwa magumu, ila  baada ya kuanza kilimo na  kujivunia matunda mengine kula na mengine kuuza kupata pesa za kujikimu anafurahia maisha.  

"Nilipojuwa umuhimu wa kilimo msitu, kinavoweza kuniinuwa kimaisha sikujibweteka niliingia shambani na kuanza kufanya kazi za kilimo hichi,"anasimulia.

HATUA ALIZOCHUKUWA KUIMRISHA KILIMO HICHO 

Baada baada ya kuingia kwenye kilimo hicho, alishirikiana na wenzake wakachimba mashimo, kwa ajili ya kupata maji na wakafanikiwa na wakawa wanamwagilia vizuri na kilimo chao kilinawiri.

Hali hiyo iliendelea akaendeleza kilimo hicho ingawa kila siku zinapoendelea hali ya juwa kali inaendelea na kukiifanya kilimo hicho kudhoofika na kisha kufa. 



"Pamoja na faida zinazopatikana kupitia kilimo msitu, lakini, kuna changamoto zinazokikabili kilimo hicho,,"anasema.

Anasimulia moja ya changamoto ni ukosefu wa maji kwa kuwepo kwa jua kali  linalosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi.  

Hali hiyo, imeathiri kilimo hicho na kufanya baadhi ya miche kukosa afya na mingine kufa kabisa, kilichosababisha kufa kwa baadhi ya miche.

Kilimo msitu ni chenye kukomboa maisha ya waliowengi kwani ni mchanganyiko wa miti na matunda hivyo ndani ya miezi mitatu unavuna na kula ama kuuza.

Mimi nimepanda migomba, minanasi, miparachichi miembe, midimu, mikungu India, kunde, njugu na mchicha. 

 KITAMSAIDIAJE 

Naomba anasema kwa vile kilimo hicho ni cha mchanaganyiko kati ya miti na matunda na hakichukuwi muda mkubwa, kati ya kupanda na kuvuna kitawasaidia kuondokana na njaa na kukuza uchumi.

Akizungumza kwa furaha anasema kilimo msitu kinampa uhakika wa kuyamudu maisha yake na kujisikia  furaha kila siku ziendapo.



Kumbe hapo awali, hakuwa na uhakika hata wa shilingi 5000 kwa mwezi, maana hakuwa mwenye kujishughulisha na kazi yoyote, alikuwa ni wa kukaa ndani na kusubiria kuletewa tu.

Shughuli za kilimo cha mihogo na mpunga ambacho alikuwa analima mwenza wake hakikumtosheleza hata kidogo yeye na familia yake.

Ndani ya shamba lake la kilimo msitu, Naomba sasa atakuwa na uhakika wa chakula kwa muda wakati, kwa kuvuna minanasi miezi sita ijayo.

Wakati anavuna manasi kwa ajili ya chakukala na biashara fedha, zitamuwezesha kuanzisha miradi mingine aliyokwishaibuni ikiwemo wa kuuza sabuni.

‘’Hivi sasa nimeanza kuona mwanga, maana nna uhakika wa kuingiza lakini 300,000 hadi shilingi 500,000 kwa mwezi, ntakapovuna mananasi ndani ya miezi sita ingawa nimo mbioni kupanda mabamia na matango,’’anasema.

MATARAJIO YAKE

Ni kuwa mkulima mkubwam kujiendeleza kimaisha na kufikia kwenye uchumi mkubwa wenye manufaa na kuongeza pato lake.



Ingawa matarajio mengine ni kuwapa wenzake elimu upandaji, kama alivyoipata yeye pamoja na kutowa elimu kwa jamii iliyomzunguka.

“Nataka niwe mkulima mkubwa katika kilimo hichi na  niwafikie wengine wote wenye hamu ya kulima kilimo hichi,”anafafanua.

 WATU WA KARIBU WA NAOMBA

Bikombo Khamis Hamad ni mmoja wa wakulima wenzake amabao wanalima kilimo msitu katika bonde la Chwale, anasema wamefurahia baada ya kumuona Naomba, amejiongeza na amejikita na kilimo hicho. 

Anasema alikuwa ni mmoja amabae hataki kujishirikisha na kilimo hicho, lakini kwa sasa amekuwa wa kwanza kushajihisha wenzake.

“Ama kweli mafunzo yanamtowa mtu sehemu moja kumpeleka kwengine, kwani mwenzetu huyu baada ya kupata mafunzo ameshajihika kweli na kilimo hichi”,alisema.

Khatib Juma Mbarouk ni mume wa Naomba, anasema hapo awali, hakuwa tayari mkewake kutoka toka na kujishirikisha na kilimo, ingawa kwa sasa amebadilika. 

Anasema hali ya maisha kuwa ngumu na kuona faida wanayoipata wanawake wengine ikiwemo kujihudumia angalau kwa baadhi ya mahitaji na watoto ndio akaona, amruhusu.

“Faida ya kilimo msitu ipo kwa sababu tumekuwa tofauti baada ya kujiingiza na kilimo hichi tunapata mazao ya kula na kuuza pia”,anasema.

 Saada Hamad Alawi ni mama wa Naomba anasema alichukuwa jitihada kubwa ya kumshajihisha mwanawe kuhusu kujiingiza na kilimo mtoto wake, ingawa hakuwa tayari.

“Baada ya kupata mafunzo ya umuhimu wa kilimo sasa ameridhia na anaiona faida, kwani hataki tena kukiacha kilimo hichi,”anaeleza. 

Mkuu wa Mawasiliano na Habari chama cha waandishi wa Habari Tanzania TAMWA Zanzibar Safia Ngalapi akawataka wakulima hao akiwemo Naomba, wasikate tamaa na wasikae kimya badala yake wazisemee chanagamoto zinazowakwaza.

Akawanasihi kuwa pamoja na misaada kuelekezwa katika mambo mengine ikiwemo mipira, badala yake itazamwe na kwa wakulima ili nao waweze kujikomboa katika kilimo chao. 

Ili wakulima waweze kuendeleza kilimo chao na kuondokana na changamoto zinzowakumba, ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha anatupia nguvu zake, katika kutowa msaada wa hali na mali.

 Mwisho 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...