Skip to main content

HIVI NDIVYO KILIMO MSITU KINAVYOKUWA RAFIKI WA KARIBU KWA UCHUMI WA WANAWAKE

 


HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@

‘UKIMUELIMISHA mwanamke umeielimisha jamii nzima'

Kutokana na msemo huo, inadhihirika kuwa mwanamke ni muhimili mkubwa, katika dunia hasa pale anapoonekana kuwa na nafasi kubwa ya ulezi ndani ya familia.

Ingawa haimaanishi kwamba, baba si muhimu hapana nae ana umuhimu wake mkubwa tu, lakini kwa upande wa mama anaechukuwa nafasi ya ulezi wa familia ni jambo kubwa.

Na ndio maana, inafahamika kuwa dunia isingeweza kuendelea mbele bila ya uwepo wa wanawake, kwani kuwekeza kwa wanawake na wasichana kunaleta matokeo makubwa. 

Wanawake wanahitaji kuwa na nyenzo madhubuti zitakazowawezesha kuyamudu maisha yao na kuondokana na utegemezi, ambao unaweza kuwa kikwazo katika kuendeleza mbele maisha yao.

Pamoja na kuwepo mafanikio na juhudi za wanawake katika sehemu mbalimbali ikiwemo za kiuchumi, na kijamii bado inaonekana suala la mabadiliko ya tabianchi, linaendelea kuwa na madhara makubwa kwa wanawake. 

Wanawake wanazidi kuonekana kama watu walio katika hatari zaidi ya kuathirika na mabadiliko ya tabianchi, kuliko wanaume, kwani wengi wao ndio wategemezi.

Kwa mujibu wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), wanawake pia ni watu wa kwanza kuhisi madhara ya mabadiliko ya tabianchi.

Mathalan nchini Kenya, baadhi ya wanawakewanalazimika kutembea zaidi ya kilomita 10, kutafuta kile wanachohitaji, ili kulisha familia zao pamoja na kutafuta maji. 

Matumaini ya wanawake wa kisiwa cha Pemba shehia ya Chwale Wilaya ya Wete ni kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi, kwa kujikita katika kilimo msitu. 

Wanawake hawa, wameweka matumaini makubwa juu ya umuhimu wa kilimo msitu huku wakiamini ndio mkombozi mkubwa wa maisha yao.

Ingawa wanawake hao ni wale waliomo kwenye mradi unaoendeshwa na Jumuiya ya Uhifadhi wa misitu Pemba ‘CFI’ na ‘CFP’ wanaofanyakazi kwa karibu na TAMWA Zanzibar, na hasa baada ya serikali ya Canada kutoa fedha na Serikali ya Zanzibar kuridhia. 

Pamoja na kwamba mradi huo imeanza kwa shehia nane  kwa Unguja na Pemba, ikiwemo wanawake wa shehia za Mchanga mdogo, Kambini, Kiuyu minungwini na Chwale kwa Pemba. 

 

Sasa wanawake wa maeneo hayo wameshaamka na kujikita katika harakati za kilimo hicho, ambacho wanasema iwapo watakiendeleza watakuwa na uhakika wa kuyamudu maisha yao.

Kilimo msitu amabacho ni mchanaganyiko wa mazao mbalimbali kama migomba, minanasi, mbazi, michikichi, njugu, mahindi na miembe. 

 WANAWAKE WANUFAIKA

Rehema Salim Issa wa Chwale Weete anasema, kilimo msitu kinawapa uhakika wa chakula katika maisha yake. 

Ingawa kilimo hicho kimekabiliwa na athari kubwa ya mabadiliko ya tabianchi bado wanaendelea nacho.

Anaona pamoja na kuonesha juhudi, kubwa katika kilimo hicho bado mabadiliko ya tabianchi yanawaathiri, ikiwemo jua kali na kupelekea kilimo chao kuharibika.

Anasema suala la jua kali limechangia kutokuwa na maji na vipando kupotea kwa haraka, jambo ambalo hukabiliwa na ongezeko la umaskini. 

"Kilimo hichi tunakitegemea kujikwamua na umaskini kwani tunapata chakula, ila jua kali limetukosesha kupata maji na imechangiwa miti kufa,’’anasema.

 


 Mkulima kiongozi Hadia Omar Haji wa kijijini hapo, anasema kilimo hicho kinawanufaisha kwa muda tofauti ikiwemo muda mfupi, kati na mrefu.

Kumbe, ili waweze kunufaika kama ilivyo maumbile ya kilimo hicho, huduma ya maji ya kumwagilia ni muhimu.

“Kusema kweli tatizo la mabadiliko ya tabianchi yanatuweka katika hali ngumu, kwani sasa ni jua hatujui ikija mvua itakuwaje,’’anaeleza.

Kwa vile wanawake ndio wakaaji wa nyumbani kuliko wanaume, hutumia muda mkubwa kuwashughulikia watoto kwenye mambo mengi, ikiwemo kula.

"Wenzetu wanaume si sana kuteswa na njaa kwani wao si wakaaji wa nyumbani, kama tulivyo wanawake na watoto wetu yeye akitoka hupata cha kujitafunia,"anasema.  

Bikombo Khamis Hamad anasema kuwekeza kwa wanawake na wasichana, kunaleta matokeo makubwa ambayo yanaigusa jamii, na maarifa waliyonayo wanawake yanahitajika sasa kuliko wakati mwingine.

 FAIDA YA KILIMO MSITU

Kilimo msitu ni mfumo wa kilimo  unaohusisha upandaji  wa miti , mazao  na wanyama, kwa lengo la kuongeza tija katika uzalishaji wa kilimo.

Pamoja na kuwa rafiki kwa kupata chakula, kuzuwia ukame kilimo hichi pia kinaleta kivuli na kuzuwia upepo makali.

 
Mkulima anaweza kunufaika na kilimo msitu kwa kumpatia mahitaji yake ya msingi kama vile kuni, matunda, kurutubisha udongo malisho ya mifugo, dawa za asili.

Nyingine ni usindikaji wa bidhaa zitokanazo na mazao ya misitu kama vile juisi, jamu na asali.

Mkurugenzi wa Jumuiya ya uhifadhi wa misitu  Pemba Mbarouk Mussa, anasema  kutopatikana kwa mvua, kukata miti ni jambo jingine linaloendelea kuathiri.

Anasema athari mbalimbali za ukataji wa miti kwa shughuli za kijamii, zimekuwa zikijitokeza  katika maeneo tofauti,  huku jumuiya hiyo  ikiendelea kutoa elimu.

Afisa kilimo kutoka CFP Saada Juma,  anasema kupitia mradi huo haujabaguwa, ingawa lengo ni kuwainuwa wanawake  katika shughuli za kujitafutia kipato. 

Afisa mdhamini Wizara ya kilimo, umwagiliaji  Maliasili  na Mifugo  Muhandisi  Idriss Hassan Abdulla, anafafanuwa kuwa,  wameandaa mpango maalum wa kuhakikisha  wanazalisha kupitia kilimo msitu.

WANAUME WANASEMAJE

Hamad Ali Suleiman, anasema wanatambua mchango mkubwa wa wanawake, katika kukiendesha kilimo msitu kwani hawako nyuma katika kuhakikisha kinaendelea. 

 


Rubea Mwadin, anawashauri wanaume kuwaruhusu wanawake, kujiingiza katika kilimo hicho na ili waweze kujikwamua na maisha.

TAMWA ZANZIBAR

Chama cha waandishi wa Habari wanawake TAMWA Zanzibar, nao husimamia kidete  haki za upatikanaji wa usawa wa kijinsia na kuwashirikisha wanawake. 

Mkuu wa mawasiliano na Habari TAMWA Sofia Ngalapi anawataka wakulima hao, wasikae kimya, katika kueleza changamoto zinazowakwaza katika kilimo chao. 



KumbeTAMWA imewapa elimu ya kuzungumza na waandishi wa habari, sasa wawatumie hapo ndio yatakaposikika . 

 

“Tunapaswa kufahamu kwamba kuwekeza kwa wanawake na wasichana kunaleta matokeo makubwa ambayo yanaigusa jamii, na maarifa waliyonayo wanawake yanahitajika sasa kuliko wakati mwingine,”anasema.



 Katika mwaka wa 2013 Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar ilifanya marekebisho ya sera ya mazingira  ya mwaka 1992 na kuingiza katika sera hiyo mpya, masuala ya mabadiliko ya tabianchi.

Sera hiyo ya mwaka 2013, imetoa muongozo juu ya usimamizi wa masuala ya kimazingira, lengo ikiwa ni kuweka rasilimali za mazingira za Zanzibar, kwa maendeleo endelevu na usimamizi bora wa mazingira kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho.    

Kwa mujibu wa utafiti mdogo uliofaywa mwaka 2013/2014, mkuu wa Kitengo cha Tabianchi katika Idara ya Mazingira Pemba, Ali Abdi Mohamed anasema kuna maeneo 123 ya mashamba yaliyoathirika na mabadiliko ya tabianchi.

Mradi wa kupambana na mabadiliko tabia nchi umetowa miche 178,268 ya aina mbalimbali ikiwemo migomba 7,000, minanasi 117,054.

Miti  ingine ambayo imetolewa kwa mfumo wa miche kwa walengwa hao wa mradi ni midalasini 39,968, miparachichi 5,950,  miembe 3,682, midimu 523, michungwa 534.

Mradi wa ZANADAPT unaoendeshwa na  jumuiya ya uhifadhi wa misitu wenye lengo la kuwafikia wajasiriamali 4,000 amabao asilimia 80 wakiwa ni wanawake  amabao utasaidia  uzalisahi wa chakula  na mazao  pamoja na kupunguza umasikini wa kipato.

Mwisho 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...