Skip to main content

KATIBU MKUU ABEDA ATOA DARSA KWA WAZAZI ULINZI WA WATOTO

 



Na Muandishi Wetu

Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto bi Abeida Rashid Abdallah amewataka Wazazi na Walezi Wanawake kuwachunguza watoto wao sehemu za siri katika miili yao ili kuhakikishwa kwamba mtoto hao wako salama na hawajafanyiwa vitendo vya udhalilishaji vya aina ya ngono.

Kauli hiyo ameitowa katika mafunzo ya kuwajengea uweza kikundi cha Banaty yaliyofanyika Michenzani Mall Unguja mara baada ya mtaalam wa Afya Dkt Ummulkulthum Omar kuwasilishaji mada ya afya ya mfumo wa uzazi pamoja na kueleza kwamba katika utekelezaji wa majukumu yake anakutana na kesi za watoto wachanga  wa miezi minane wameingiliwa kinyume na maumbile na kuharibiwa.

Bi Abeida amesema kwa vile Wazazi na Walezi Wanawake hawana vibakio ni vyema kuwa karibu na watoto hasa watoto wa kiume waliyofikia umri wa balegh kwa kuwauliza masuali bila ya kuona haya pamoja na kuwaangalia sehemu zao za siri kama ziko salama na hazijafanyiwa udhalilishaji wa aina ya ngono.

“Tuwe karibu nao hasa watoto wa kiume sisi wanawake hatuna vibakio kwahiyo lazima tuwe karibu na watoto wetu tuwahoji Je hakuna mtu aliyeguza sehemu za siri? Na tusiishie kuwauliza tu. Pia kuwaangalia hasa huko sehemu ya siri  tujue kama kuko salama, tusisuniria azoeshe mchezo mchafu ”. Alisema Abeida.



Alieleza kwamba ripoti ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeonesha matukio ya udhalilishaji 199 yameripotiwa kwa mwezi wa Oktoba, 2023 kati ya idadi hiyo asilimia 78.9 ni watoto na wanawake ni asimia 16.2 hivyo ni vyema Wazazi na Walezi Wanawake kila mara wawe karibu na watoto wao.

Aidha katibu Mkuu huyo alitoa wito kwa  washiriki wa mafunzo hayo  na wanawake wote waliyopata mafunzo ya ujasiriamali  kutumia ipasavyo  elimu hiyo kwani Serikali ya Mapinduzi inatoa fursa ya mikopo kwaajili ya kuwawezesha  kiuchumi  ili waweze kujiongezea kipato na kujikwamua na umasikinini. Alisema kwani umasikini pia unachangia matendo ya udhalilishaji kutokea kwa watoto.

Naye Mtaalum wa Afya bi Dkt Ummulkulthum Omar kutoka Hospital ya Rufaa ya Mnazimmoja Zanzibar katika mada ya mfumo wa uzazi aliyowasilisha alieleza matatizo  mbali mbali yanayowatokea wanawake katika mfumo wa uzazi ikiwemo kutoshika mimba, kutokwa na uchafu usiokuwa wa kawaida katika sehemu za siri, n.k. hivyo amewataka wanawake kukimbilia hospitali endapo wataona dalili yeyote ambayo sio ya kawaida kutokana na elimu aliyofundisha ili kuwahia kutimbiwa.

Aidha katika uwasilishaji wa mada hiyo aliezea kwamba anakutana na kesi ya watoto wa umri tofauti ambao wameingiliwa kinyume na maumbile ikiwemo watoto wa miezi minane, hali ambayo inasikitisha hasa ukiangalia matendo hayo yanafanywa na mtu wa karibu.

Mapema Mratibu wa mafunzo hayo ambaye ni Mkurugeni wa Raha online TV bi Raya Hamadi Mchele amesema lengo la kunadaa mafunzo hayo ni kuwapa elimu kundi la Banaty ikiwemo elimu ya afya, kujitambua na elimu ya ujasiriamali ili waweze kujikwamua kimaisha.

Kikundi cha Banaty kimeanzishwa kwa lengo la kusaidiana katika shughuli mbali mbali za kijamii ikiwemo harusi na msiba. Hivyo kikundi hicho kinamuda wa miaka minane na mfuko wao wafedha una pesa zaidi ya shilingi za Tanzania milioni ishirini.

Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch