Skip to main content

NAIBU SPIKA ZANZIBAR KUFUNGUA MIRADI MIWILI ASUBUHI HII PEMBA

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

SHAMRA shamra za kuelekea miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, yaliofanyika mwaka 1964, zinatarajiwa kuendelea tena asubuhi hii, katika wilaya za Chake chake na Wete, kwa ufunguzi wa miradi miwili.

Shamra shamra hizo, zitaanzia kwa wilaya ya Chake chake, ambapo Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mgeni Hassan Juma, anatarajiwa kufungua soko la samaki na mboga eneo la Machomane wilayani humo.

Shughuli hiyo inatarajiwa kuanza majira ya saa 2:00 asubuhi, kwa kuwasili wananchi na wageni wingine mashuhuri, kabla ya Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za ‘SMZ’ Issa Mahafudhi, kumpokea mgeni rasmi.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa kwa vyombo vya habari, na Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba, Mattar Zahor Massoud, alisema tayari kila kitu kilichopangwa kwa ajili ya hafla hiyo, kimekaa sawa.

Alisema, tayari mgeni rasmi wa ufunguzi wa soko hilo, alishapatikana mapema, na kilichobakia ni kwa wananchi na wafanyabiashara kushiriki katika hafla hiyo.

‘’Ni kweli asubuhi hii ya Disemba 27, mwaka huu Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Mgeni Hassan Juma, anatarajiwa kulifungua soko jipya la na kisasa la Samaki na mboga, ndani ya shamra shamra za kuelekea miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar,’’alisema.

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, aliwaeleza waandishi wa habari kuwa, mradi ambao unatarajiwa kufunguliwa jioni ya leo, ni ule wa ghala la chakula na vifaa vya ujenzi, lililopo Kinyasini wilaya ya Wete.

Alieleza kuwa, kuelekea shughuli hiyo, tayari mambo kadhaa yameshakaa sawa, ikiwa ni pamoja utenzi, wimbo maalum wa mapinduzi na ngoma nyingine za utamaduni.

Aidha alieleza kuwa, Katib Mkuu wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar ndie mwenyeji wa shughuli hiyo kwa upande mmoja, kwa ndio wizara husika.

Wakuu hao wa mikoa wakielezea umuhimu wa kufanyika kwa mapinduzi hayo, walisema yalikuwa na lengo zuri la kumkomboa mzalendo wa nchi hii, ambae alikuwa hana thamani.

Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, alisema hakukuwa na mwananchi aliyekuwa akifikiria namna ya kulima na kupata tija, au kufanyakazi na kupata malipo mazuri.

‘’Leo tukiwa ndani ya miaka 60 ya Mapinduzi, kila mmoja ni shahidi kuwa, sasa tumekomboka na kila mmoja anafanyashughuli zake kwa mujibu wa uwezo wake, haya ndio maana na mapinduzi daima,’’alisema.

Hata hivyo amewakumbusha wananchi hao, kuendelea kushiriki katika hafla za uwekaji mawe ya msingi na ufunguzi wa miradi mbali mbali, kwani serikali, inafanya kwa ajili yao.

Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, alisema maana ya mapinduzi, ni kuendeleza mbele ujenzi wa miradi mbali inayowahusu wananchi na yenye tija katika maisha yao.

‘’Kila mmoja ni shahidi kupitia serikali ya awamu ya nane, imeshafanya miradi kadhaa hasa ndani ya mkoa huu, tena ndani ya muda mfupi ukiwemo kituo cha Vijana, bara bara ya uwekezaji, skuli ya msingi kisiwa cha Kojani pamo na skuli ya Ole,’’alifafanua.

Miradi ambayo itafunguliwa kesho ni pamoja na ofisi ya elimu Wete, uwekaji jiwe la msingi skuli ya msingi Mwambe pamoja na mradi wa vijana uliopo Weni wilaya ya Wete.

                                    Mwisho    

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch