Skip to main content

MWAKILISHI CHAMBANI, APIGIA CHAPUO KILIMO MATANGO BAHARI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MWAKILISHI wa Jimbo la Chambani wilaya ya Mkoani Pemba, Bahati Khamis Kombo, amewasisitiza vijana kuchangamkia kilimo cha matango bahari, kwani bei yake iko juu kuliko kilimo cha karafuu.

Alisema, kama Katibu mkuu wa wizara ya Uvuvi na Uchumi wa Buluu, alivyosema kuhusu soko na bei, ni fursa kwa vijana wa jimbo la Chambani kuekeza kwenye kilimo hicho.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mara baada ya kuwekwa kwa jiwe la msingI la kituo cha kutotoleshea vifaranga vya matango bahari eneo la Dodo Pujini hivi karibuni, alisema sasa vijana washindwe wao.

Alisema, kama kilo matangao (majongoo) bahari ni shilingi 100,000 ni wakati vijana kwenda kujikomboa kupitia sekta ya bahari.

Alieleza kuwa, awali upatikanaji vifaranga ilikuwa ni changamoto kwa wakulima hao kuagizisia kisiwani Unguja, ingawa kwa sasa kituo cha uzalishaji kipo kisiwani Pemba.

‘’Changamoto kubwa ya kilimo cha matango bahari ilikuwa ni upatikanaji wa vifaranga, lakini sasa kituo cha kisasa kipo na tumearifiwa kina uwezo mkubwa wa kutoa 5000 kwa mwezi,’’alieleza.

Katika hatua nyingine Mwakilishi huyo wa Jimbo la Chambani Bahati Khamis Kombo, alisema maono ya Dk. Mwinyi ni kutaka kuhakikisha, anakikomboa kisiwa cha Pemba, kwa vitendo.

‘’Kila mmoja ni shahidi kwenye sekta za maji, hospotali, elimu na sasa ameongeza kasi kawenye uchumi wa buluu kwa kugawa boti na mashine yote ni kutaka kuongeza kipato kwa wananchi,’’alifafanua.




Hata hivyo ameikumbusha wizara husika, kuhakikisha wanaongeza idadi ya mashamba yay a ufugaji wa matango bahari, kutoka 50 yaliopo Pemba na kuongeza walau kufikia 200.

Wakulima wa kilimo hicho kutoka Gando, Asia Mwalimu Omar na mwenzake Mtumwa Budi Pandu, walisema kilimo hicho licha ya kukabiliwa na changamoto wakati wa kuanza, lakini kina tija mno.

‘’Pale mwanzo wa kupokea vifaranga panahitajika umakini wa hali ya juu, lakini ikimalizika miezi mitatu, hawana shidna tena wewe subiri upate fedha zao tu,’’walisema.

Nae Himdi Mjaka Himid wa Pujini, alisema uwepo wa kituo hicho kitasaidia kupanua wigo wa kujiajiri kwa vijana na wanawake, ambao ndio waliojiekeza baharini.

Kwa upande wake, Katibu mkuu wizara ya Uchumi wa Bulu una Uvuvi Zanzibar Aboud Suleiman Jumbe, aliwataka wananchi wa Zanzibar, kuchangamkia kilimo hicho haraka, kwani kwa sasa thamani nzima ya soko kwa bidhaa hiyo duniani inafikia Dola za Marekani Bilioni 10.

Alieleza kuwa, kwa nchi za Afrika, 80 kila 100 zilizopakana na ukanda wa pwani zinajishughulisha, kilimo, uuzaji usafirishaji wa matanga bahari na theluthi moja ya zao hilo ni kutoka nchi za Afrika kwenda kwenye masoko ya nchi za China, Japan, Hong kong, Taiwan na Korea.

 inatoka magharibi wa ukanda wa hari ya hindi inapopatikana Zanzibar,’’alifafanua.

Alieleza kuwa, mara baada ya Zanzibar kujenga kituo cha kwanza cha kuzalishia matango bahari mwaka 2017, na kuanza ufugaji, uzalishaji na usafirishaji nje ya nchi, mwaka 2019 ulikuwa ni tani 30.

Alifahamisha kuwa, kisha usafirishaji huo, ulisita kwa ujio wa janga la Covid 19, mwaka 2020 hadi 2021 na kufikia tani 5.58, ingawa mwaka 2022 usafishaji huo uliongezeka na kufikia tani 15, zenye thamani ya shilingi milioni 492.4.

Mwisho

Comments