Skip to main content

MWAKILISHI CHAMBANI, APIGIA CHAPUO KILIMO MATANGO BAHARI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MWAKILISHI wa Jimbo la Chambani wilaya ya Mkoani Pemba, Bahati Khamis Kombo, amewasisitiza vijana kuchangamkia kilimo cha matango bahari, kwani bei yake iko juu kuliko kilimo cha karafuu.

Alisema, kama Katibu mkuu wa wizara ya Uvuvi na Uchumi wa Buluu, alivyosema kuhusu soko na bei, ni fursa kwa vijana wa jimbo la Chambani kuekeza kwenye kilimo hicho.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mara baada ya kuwekwa kwa jiwe la msingI la kituo cha kutotoleshea vifaranga vya matango bahari eneo la Dodo Pujini hivi karibuni, alisema sasa vijana washindwe wao.

Alisema, kama kilo matangao (majongoo) bahari ni shilingi 100,000 ni wakati vijana kwenda kujikomboa kupitia sekta ya bahari.

Alieleza kuwa, awali upatikanaji vifaranga ilikuwa ni changamoto kwa wakulima hao kuagizisia kisiwani Unguja, ingawa kwa sasa kituo cha uzalishaji kipo kisiwani Pemba.

‘’Changamoto kubwa ya kilimo cha matango bahari ilikuwa ni upatikanaji wa vifaranga, lakini sasa kituo cha kisasa kipo na tumearifiwa kina uwezo mkubwa wa kutoa 5000 kwa mwezi,’’alieleza.

Katika hatua nyingine Mwakilishi huyo wa Jimbo la Chambani Bahati Khamis Kombo, alisema maono ya Dk. Mwinyi ni kutaka kuhakikisha, anakikomboa kisiwa cha Pemba, kwa vitendo.

‘’Kila mmoja ni shahidi kwenye sekta za maji, hospotali, elimu na sasa ameongeza kasi kawenye uchumi wa buluu kwa kugawa boti na mashine yote ni kutaka kuongeza kipato kwa wananchi,’’alifafanua.




Hata hivyo ameikumbusha wizara husika, kuhakikisha wanaongeza idadi ya mashamba yay a ufugaji wa matango bahari, kutoka 50 yaliopo Pemba na kuongeza walau kufikia 200.

Wakulima wa kilimo hicho kutoka Gando, Asia Mwalimu Omar na mwenzake Mtumwa Budi Pandu, walisema kilimo hicho licha ya kukabiliwa na changamoto wakati wa kuanza, lakini kina tija mno.

‘’Pale mwanzo wa kupokea vifaranga panahitajika umakini wa hali ya juu, lakini ikimalizika miezi mitatu, hawana shidna tena wewe subiri upate fedha zao tu,’’walisema.

Nae Himdi Mjaka Himid wa Pujini, alisema uwepo wa kituo hicho kitasaidia kupanua wigo wa kujiajiri kwa vijana na wanawake, ambao ndio waliojiekeza baharini.

Kwa upande wake, Katibu mkuu wizara ya Uchumi wa Bulu una Uvuvi Zanzibar Aboud Suleiman Jumbe, aliwataka wananchi wa Zanzibar, kuchangamkia kilimo hicho haraka, kwani kwa sasa thamani nzima ya soko kwa bidhaa hiyo duniani inafikia Dola za Marekani Bilioni 10.

Alieleza kuwa, kwa nchi za Afrika, 80 kila 100 zilizopakana na ukanda wa pwani zinajishughulisha, kilimo, uuzaji usafirishaji wa matanga bahari na theluthi moja ya zao hilo ni kutoka nchi za Afrika kwenda kwenye masoko ya nchi za China, Japan, Hong kong, Taiwan na Korea.

 inatoka magharibi wa ukanda wa hari ya hindi inapopatikana Zanzibar,’’alifafanua.

Alieleza kuwa, mara baada ya Zanzibar kujenga kituo cha kwanza cha kuzalishia matango bahari mwaka 2017, na kuanza ufugaji, uzalishaji na usafirishaji nje ya nchi, mwaka 2019 ulikuwa ni tani 30.

Alifahamisha kuwa, kisha usafirishaji huo, ulisita kwa ujio wa janga la Covid 19, mwaka 2020 hadi 2021 na kufikia tani 5.58, ingawa mwaka 2022 usafishaji huo uliongezeka na kufikia tani 15, zenye thamani ya shilingi milioni 492.4.

Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch