Skip to main content

WAZIRI SHAABAN ASIFIA MATUNDA YA MAPINDUZI MIAKA 60




NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WAZIRI wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar Omar Said Shaaban, amesema tayari serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, imeshatekeleza mambo makubwa kwa wananchi, ikiwemo miradi mbali mbali, yenye tija ya moja kwa moja.

Alisema, ndani ya shamra shamra hizi za kuelekea miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, ni wakati kwa viongozi na wananchi kuyatangaaza mema yaliokwishafanywa, ikiwemo ujenzi wa miundo mbinu ya barabara, afya elimu na huduma za maji safi na salama.

Waziri Shaaban, aliyasema hayo leo Disemba 24, 2023 kwenye hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la mradi wa utotoleshaji wa vifanga vya matango bahari, ikiwa ni sehemu ya shamra shamra, za kuelekea miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, iliyofanyika shehia ya Dodo Pujini, wilaya ya Mkoani Pemba.

Alisema, kwa mfano ndani ya wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, wametafsiri kwa vitendo, maana ya Mapinduzi pamoja na yale maono ya Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, la kuweka mkakati maalum katika uwekezaji wa bahari.





Alieleza kuwa, hivyo kila mmoja na kwa nafasi yake, anaowajibu wa kusherehekea mafanikio ya Mapinduzi ya Zanzibar, ya mwaka 1964, kwani yapo mafanikio ya wazi wazi, kwenye sekta mbali mbali ikiwemo uchumi na kijamii.

‘’Leo tukisherehekea miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, moja ya wizara iliyofanya vizuri kwa muda mfupi, ni hii iliyokuja kuanzishwa na Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, ya Uvuvi na Uchumi wa Buluu, ambao sasa wananchi wananeemeka,’’alieleza.

Alifafanua kuwa, Mapinduzi hayo ndio msingi wa utu, heshima, mafanikio na maendeleo ya kila mmoja, hivyo ni wajibu wa kila mmoja, kuyalinda na kuyaenzi, ili yazidi kuwakomboa wananchi.

Akizungumzia mikakati ya serikali, katika kuwandeleza wananchi kupitia uchumi wa buluu na uvuvi, alisema ni pamoja na ufugaji wa mazao ya baharini kama vile kaa, samaki na matango bahari.




‘’Ndio maana, ushirikiano wa serikali na wawekezaji wa kituo hichi cha kutotoleshea vifaranga vya matango bahari wanaoitwa Mwambao MCC, ni hatua kubwa na inahitajika kuendelezwa, kwa maslahi mapana zaidi,’’alifafanua.

Alisema serikali imejidhatiti kuendeleza wananchi kupitia dira yake ya maendeleo ya mwaka 2050, pamoja na mipango ya maendeleo, ambapo vituo kama hivyo, ni sehemu ndogo katika hilo.

Alifafanua kuwa, tayari serikali katika kutekeleza dira hiyo kwa vitendo, imechimba mabwawa 100 ya ufugaji wa mtango bahari (majongoo bahari), kwa idadi sawa, kati ya Unguja na Pemba.

Alieleza kuwa, sasa ndio mwisho kwa wafugaji wa matango bahari waliopo Pemba, kuagizishia vifaranga hivyo kutoka Unguja, baada ya kuzinduliwa kwa kituo cha Pujini Dodo, wilaya ya Mkoani.

‘’Unguja kipo Bet-elrass ambacho kilikuwa kikihudumia Unguja na Pemba, kwa kuzalisha vifaranga vya matango bahari, lakini kilichopo Pujini, sasa kitasidia wakulima zaidi ya 500 walipo Pemba,’’alifafanua.

Mapema Katibu mkuu wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar Aboud Suleiman Jumbe, alisema vitango baharini, ni bidhaa adimu na dhahabu ya bahari, kwani soko lake ni katika nchi za China, Japan na Korea.




Hivyo aliwataka wananchi wa Zanzibar, kuchangamkia kilimo hicho, kwani kwa sasa, thamani ya soko kwa bidhaa hiyo duniani, inafikia dola za Marekani bilioni 10, ambapo kwa nchi za Afrika, 80 kila 100 zinazopakana na ukanda wa pwani, zinajishughulisha na kilimo, uuzaji usafirishaji wa matango bahari.

‘’Theluthi moja ya zao la matango bahari, kutoka nchi za Afrika kwenda masoko ya nchi za China, Japan, Hong kong, Taiwan na Korea inatoka magharibi wa ukanda wa hari ya hindi, inapopatikana pia Zanzibar,’’alifafanua.

Katibu Mkuu huyo alieleza kuwa, mara baada ya Zanzibar kujenga kituo cha kwanza cha kuzalishia vifaranga vya matango bahari mwaka 2017, na kuanza ufugaji, uzalishaji na usafirishaji nje ya nchi, kisha mwaka 2019 kulisafirishwa na tani 30 pekee.

‘’Usafirishaji huo, ulisita kwa ujio wa janga la Covid 19, mwaka 2020 hadi 2021 na kufikia tani 5.58, ingawa mwaka 2022 usafishaji uliongezeka na kufikia tani 15, zenye thamani ya shilingi milioni 492.4,’’alieleza.



Aliongeza kuwa, uwepo wa mashamba 100 ya matango bahari kwa Unguja na Pemba, kunatarajiwa kuongeza usafirishaji tani 45 hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 2024.

Nae Mkurugenzi Mtandaji wa shirika la MCC-Mwambao Said Khalifa, alisema, wanatamani kuona jamii ya pwani, wanakuwa wasimamizi wazuri wa rasilimali bahari, kwa maendeleo endelevu.

‘’Lengo la mradi huu ni kuisadia serikali kuu, katika uchumi wa buluu, kwani ndio ambao kwa sasa, umepewa kipaumbela kama sekta kiongozi,’’alifafanua.



Alieleza kuwa, kituo hicho kina mpango wa kuzalisha vifaranga zaidi ya 5,000 kwa mwezi, sawa na mashamba matano, ambapo tayari kwa awamu ya kwanza, walizalisha mayai milioni 1, na kukuza vifaranga 4,000, na kisha kupata 1,035 na 1,1500 ndio wamefakiwa kuviuza.

‘’Kwa awamu ya pili, tunavyo vului lui wastani wa milioni 2.1, vilivyozalishwa, ambavyo kwa sasa viko hatua ya kulelewa, na kisha vitawekwa kwenye eneo maalum, kabla ya kuwa vifaranga kamili kwa ajili ya kuuzwa,’’alifafanua.

Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, alisema uwepo wa kituo hicho, ni ishara ya utekelezwaji wa kwa vitendo, maana halisi ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Ujenzi wa kituo wa kutotolea matango bahari, umeanza mwezi Machi mwaka huu na kumalika mwaka huu, ambapo jumla shilingi milioni 55, kutoka shirika la moja lililoko Marekani, ndio zilizotumika.




Kisha uwekaji mitambo maalum na ya kisasa ulifuatia, na kugharimu  shilingi milioni 90, uwepo wa mashine za kuvutia maji baharini, ujenzi wa barabara ya kuingia kituoni hapo kwa njia ya kifusi.

Ufunguzi wa miradi ya Mapinduzi ya Zanzibar, utasita kwa siku mbili na kuendelea tena Disemba 27, kwa ufunguzi wa miradi miwili ukiwemo wa soko la samaki na mboga Machonne Chake chake na Ufunguzi wa ghala la la chakula na vifaa vya ujenzi Kinyasini wilaya ya Wete.

    Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch