Skip to main content

OTHMAN AWEKA JIWE LA MSINGI SKULI YA GHOROFA KOJANI, ASEMA HIZO NI RASHA RASHA ZA MAPINDUZI



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@

MAKAMU wa Kwanza wa Rais Zanzibar Othman Massoud Othman, amesema Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, ndio yaliotengeneza mwanga, na kisha kufungua milango ya fursa sawa kwa wote, ikiwemo elimu bila ya ubaguzi.

Alisema, Mapinduzi hayo ndio yaliyojenga ngome ya uhakika kwa kila mzanzibari, katika kupata elimu, matibabu na huduma nyingine za kijamii bila ya ubaguzi wowote.

Makamu huyo wa Kwanza, aliyasema hayo leo Disemba 30, 2023 Kisiwa cha Kojani wilaya ya Wete Pemba, mara baada ya uwekaji wa jiwe la msingi la skuli ya ghorofa ya msingi ya Kojani, ikiwa ni shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Alisema, ujenzi wa skuli hiyo pamoja na nyingine, ni mkakati endelevu wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, wa kuhakikisha inawapatia wananchi wake haki ya elimu, waliyoikosa kabla ya Mapinduzi.

Alieleza kuwa, elimu ndio msingi wa uhakika wa maendeleo ya mwanadamu, na ndio maana hata Muumba katika kuwaumba wanaadamu, kuliambatana na tendo la kupewa elimu.






Alisema msingi wa elimu, kama inavyofanya serikali kwa kuwekeza miundombinu ya kisasa, ndio inayomtofautisha mwanaadamu na viumbe vyingine duniani.

‘’Kuimarika kwa sekta ya elimu na miundombinu yake, kumekuwa kukishuhudia kukua mwaka hadi mwaka, na haya hasa ndio azma na malengo ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964,’’alieleza.

Aidha Makamu huyo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Othman Massoud Othman, alisema kuwa, kwa kule serikali kutambua umuhimu wa haki ya elimu, imeweka kwenye dira yake ya 2050, ikiwa na dhima ya kujenga nguvu kazi, yenye ujuzi, ubunifu na uwezo wa kuchangia katika uchumi wa taifa.

Alifahamisha kuwa, moja ya vipaumbele vya kwanza ndani ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ni elimu na ndio maana, imemshapitisha mpango mkubwa wa mageuzi ya elimu, hapa visiwani.

‘’Mpango huo unazo nguzo kadhaa, ikiwemo kuimarishwa kwa miundombinu ya elimu, ambayo yatamuwezesha mwanafunzi kusoma kwa mujibu wa mahitaji ya kisasa,’’alifafanua.

Hivyo Makamu huyo wa Kwanza, alifahamisha kuwa, ujenzi wa skuli hiyo, unakwenda samba mba na mipango na mikakati ya muda mrefu ya serikali, katika mageuzi ya elimu.

‘’Uwekaji wa jiwe la msingi la skuli hii, ni kielelezo tosha, cha dhamira thabiti ya serikali, kupitia wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, katika kutekeleza kwa vitendo, mageuzi ya elimu,’’alieleza.




  Aidha alisema skuli hiyo ya Kojani ni moja, lakini tayari serikali kupitia wizara husika, inaendelea na ujenzi wa skuli nyingine 25, katika mwaka huu, tano kati ya hizo zikiwa mkoa wa kaskazini Pemba.

Alieleza kuwa skuli hizo ambazo ni za kisasa ni pamoja na Kojani, Konde, Kifundi, Utaani pamoja na ile ya Maziwang’ombe , ambazo zinatarajiwa kuanza kutumiwa, kuanzia mwakani.

‘’Kumbukeni kuwa, ujenzi wa skuli hizi za kisasa kwa Unguja na Pemba, serikali imeshajiwekea shabaha, ili kuona kila darasa halizidi wanafunzi 45, pamoja na kuwa na mkondo mmoja wa wanafunzi,’’alisema.

Alisema, licha ya ongezeko la idadi ya watu wa Zanzibar kutoka milioni 1.3 hadi kufikia watu milioni 1.8, sawa na ongezeko la wananchi wa Kojani, waliokuwa 4,536 kwenye sensa ya mwaka 2012 hadi kufikia 8, 475 kwa sensa ya mwaka 2022.

Wakati huo huo Makamu huyo wa Kwanza, amewataka wazazi na walezi, kuhakikisha hakuna mtoto, ambae amefikia umri wa kuandikishwa masomo na kubakia nyumbani.

Mapema Katibu mkuu wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Khamis Abdalla Said, alisema skuli hiyo inajengwa kwa fedha za serikali na hadi kukamilika kwake, itagharimu shilingi bilioni 3.382.



Alieleza kuwa, skuli hiyo itakuwa na madarasa ya chini ‘ground floor’ kisha ghorofa mbili za juu, pamoja na kuwekewa miundombinu yote ya kisasa, kwa ajili ya wanafunzi.

Katibu mkuu huyo alifafanua kuwa, ndani ya skuli hiyo kutakuwa na vyumba 34, ofisi tatu za waalimu, ukumbi wa mitihani, maabara, ofisi ya TEHAMA, maktaba na stoo.

‘’Shabaha ya ujenzi wa skuli kama hizi za ghorofa, kwanza ni kuongeza kiwango cha elimu, kuondoa mikondo miwili pamoja na wanafunzi kuwepo 45 kwa darasa moja,’’alieleza.

Alifamisha kuwa, skuli ya sasa ya Kojani inayotumika, inavyo vyumba 19, yenye wanafunzi 2,802 ambapo kati ya hivyo, vyumba vitano vinatumiwa na wanafunzi 430, wastani wa wanafunzi 86 kwa darasa moja.

‘’Vyumba vya msingi ni 14 vinavyotumiwa na wanafunzi 1,942 sawa na wanafunzi 139 kwa darasa moja, jambo linalosababisha kuingia mikondo miwili,’’alieleza.

Kwa upande wake, Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba, Salama Mbarouk Khatib, amewataka wananchi wa Kojani, kuthamini juhudi za serikali, katika kuitunza miundombini ya elimu.





Hata hivyo, amepongeza Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, kwa kueteleza kwa vitendo, ahadi yake kwa wananchi wa Kojani, juu ya ufinyu wa nafasi za kusomea kwa watoto wao.

                                   Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch