Skip to main content

MAKAMU WA KWANZA AIZINDUA BARABARA KIPAPO-MGELEMA, AWAKUMBUSHA JAMBO WANANCHI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MAKAMU wa Kwanza wa Rais Zanzibar Othman Massoud Othman, amesema maono ya muasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar, mzee Abeid Amani Karume, yanaendelea kutekelezwa kwa vitendo, ndani ya awamu ya nane, inyoongozwa na Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi.

Makamu huyo wa Kwanza, aliyasema hayo leo Disemba 29, 2023 shehia ya Mgelema wilaya ya Chake chake Pemba, mara baada ya uzinduzi wa barabara ya Kipapo- Mgelema, ikiwa ni shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Alisema, ujenzi wa barabara za kisasa, skuli, miundombinu ya maji safi na salama na matayarisho ya ujenzi wa viwanja vya ndege na utanuzi wa bandari, yanayotekelezwa sasa, ndio azma na maono ya wasisi wa Mapinduzi.




Aleleza kuwa, kila mmoja anayosababu ya kufurahia na kushangilia yanayofanywa sasa, na yale yaliokuwepo kabla, kwani yanalenga moja moja kutatua changamoto za wananchi.

Alifafanua kuwa, ujenzi wa bara bara ya Kipapo– Mgelema na nyingine, ni mifano mizuri ya jitihada za serikali ya awamu ya nane, ambayo yanakwenda sambamba na shabaha ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.

‘’Leo tukiadhimisha miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, kila mmoja anayofuraha, maana yapo mingi yameshatekelezwa, kwa mfano barabara hii ya Mgelema, kila mmoja alikuwa shahidi jinsi ilivyokuwa hapo kabla’’alifafanua.

Aidha Makamu huyo wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Othman Massoud Othman, amewataka wananchi wanaotumia barabara hiyo, kuilinda na kuienzi, ili itumike kwa muda mrefu ujao.

Alieleza kuwa, barabara ndio kichecheo pekee cha kukuza na kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja na serikali kuu, hivyo ni wajibu, kuilinda miundombinu yake.

Hata hivyo, amewakumbusha wananchi wa Pemba, kuwa tayari serikali imeshasaini mikataba mbali mbali na kampuni tofauti, juu ya ujenzi wa bara bara kuu na zile za ndani.

‘’Hapa nichukue nafasi ya kuipongeza wizara husika, kwa juhudi zao mbali mbali, ambazo zinaonekana kwa vitendo, katika kuwakwamua wananchi, na sio tu kwa usafiri, bali hata kwa usafirishaji wa mazao yao na bidhaa nyingine,’’alieleza.

Wakati huo huo, Makamu huyo wa Kwanza, ameitaka jamii kuendelea kupanda miti na kukirejeshea uasili wake, kisiwa cha Pemba, ambacho kilikuwa kimezungumkwa na miti mikubwa.

Aidha ameitaka jamii, kutokuwa sehemu ya kuendeleza na kukuza vitendo vya udhalilishaji na ukatili kwa wanawake na watoto, kwani nao wanahitaji kulindwa, ili wawe viongozi wema hapo baadae.




Katibu Mkuu wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar Khadija Khamis Rajabu, alisema ujenzi wa barabara hiyo ya Kipapo- Mgelema yenye urefu wa kilomita 5.3, ujenzi wake uligawika katika awamu mbili, ambapo moja wapo ni ujenzi wa Kipapo –Mgelema na kisha Mgelema- Wambaa yenye urefu wa kilomita 4.

Alieleza kuwa, ujenzi huo ulianza mwezi Novemba mwaka 2020, na ukitarajiwa, kukamilika mwaka mmoja baadae, ingawa kutokana na sababu za mbali mbali, umekamilika Disemba mwaka huu.

Aidha Katibu Mkuu huyo alieleza kuwa, barabara hiyo ina upana wa mita sita, na mabega {road shoulder} yenye upana wa 0.5 kwa kila upande, na ujenzi wake umetumia mfumo wa lami moto.

‘’Kwa sasa bara bara hii, inazo daraja ndogo {culvert} sita na daraja moja kubwa, na imeshawekewa alama za barabarani, kwa ajili ya vyombo vya moto, watembea kwa miguu na ina uwezo wa kupitisha gari zenye uzito usiozidi tani 10,’’alifafanua.

Alieleza kuwa, kama barabara hiyo ya Kipapo- Mgelema itatunzwa inaweza kuishi kwa wastani wa miaka 10, bila ya kuharibika, wala kufanyiwa matengenezo yoyote.

Katibu Mkuu huyo aliongeza kuwa, ujenzi wa barabara hiyo, hadi kukamilika kwake, umeshatumia zaidi ya shilingi bilioni 2.109, fedha zilitolewa na serikali ya Mapinduzi, kupitia Mfuko wa Bara bara na imejengwa na Wakala wa Barabara Zanzibar.

Akizungumzia fidia za vipando na makaazi ya wananchi, alisema miti ya wananchi 63 na majengo ya watu 17, yalilazimika kuondolewa, na sasa shilingi milioni mia 500.723 zimeshatumika.

‘’Kati ya fedha hizo, zaidi ya shilingi milioni 134.6 zimetumika kulipa majengo ya makaazi na shilingi milioni 437.434 zimeshatumika kuwalipa wananchi 63 walioharibiwa miti yao,’’alieleza.

Mapema Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar Dk. Khalid Salum Mohamed, alisema ujenzi wa barabara hiyo, umechukuwa muda mrefu hadithi yake, bila ya kutekelezwa.

Hata hivyo Dk. Khalid alisema katika kipindi kifupi tayari wizara inaendelea na ujenzi wa kilomita 854 kwa Zanzibar, ambapo kwa Pemba zipo wastani wa kilomita 300 zinazoendelezwa ujenzi katika maenoe mbali mbali.

Alisema, kwa upande wa mkoa wa kaskazini Pemba, zipo wastani wa kilomita 81.35 wakati mkoa wa kusini kukiwa na kilomita 53.6 kwa barabara za vijijini pekee, zinazoendelea na ujenzi.

‘’Lakini kwa upande wa wilaya ya Chake chake, wizara wakati wowote itaanza na ujenzi wa barabara ya Wesha- Mkumbuu yenye urefu wa kilomita 10, Wawi- Mesi kupitia Mzambarau -Boko yenye urefu wa kilomita 6.4, Mkoroshoni- Ndugu kitu hadi Machomane kilomita 2 pamoja na Mchanga wa Kwale- Kichuwani yenye urefu wa kilomita 2.7,’’alifafanua.

Aidha Waziri huyo aliwaeleza wananchi kuwa, barabara nyingine ambazo zitajengwa kwa kiwango cha lami ni Chanjaani- Pujini, Chanjamjawiri- Tundaua, Mizingani -Wambaa, Mtambile -Kangani na Mtambile -Mwambe, ambazo awali barabara hizo zilijengwa kwa lami baridi.

Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba, Mattar Zahor Massoud, amewataka wananchi wa Mgelema, kuwawalinzi na barabara hiyo, ili iweze kudumu kwa muda mrefu.

Hata hivyo amepongeza Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, kwa usikivu wake wa vilio vya wananchi, hali inayosababisha kuimbua miradi mkubwa na yenye tija.

                                   Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch