Skip to main content

SPIKA ZUBEIR AWEKA JIWE LA MSINGI SKULI YA GHOROFA MWAMBE KISHA AACHA UJUMBE

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

SPIKA wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Zubeir Ali Maulid, amewataka wananchi wa Mwambe wilaya ya Mkoani, kuyaenzi na kuyalinda mapinduzi ya Zanzibar, kwani ndio mkombozi wa upatikanaji wa huduma mbali mbali, ikiwemo elimu.

Spika Zubeir, aliyasema hayo leo Disemba 28, 2023 Mwambe wilaya ya Mkoani, mara baada ya uwekaji wa jiwe la msingi la skuli ya ghorofa mbili iliyopo Chanjaani, ikiwa ni shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Alisema kabla ya Mapinduzi hayo, watawala walitoa huduma hizo kwa matabaka na kuwafanya watoto wa wanyonge, kukosa huduma mbali mbali ikiwemo elimu na matibabu.

Alieleza kuwa, madhila hayo na mingine ndio yaliyowafanya waasisi wa Mapinduzi hayo, kuamua kufanya kila juhudi ili kuhakikisha wanauondoa utawala uliokuwepo, ili kuwarejeshea heshima wazalendo.




‘’Leo tukiwa ndani ya miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar wananchi wa Mwambe na maeneo mingine, tunayokila sababu ya kuyalinda, kuyaenzi mapinduzi hayo, maana ndio ambayo sasa matunda yake tunayatumia,’’alieleza.

Akizungumza uwepo wa skuli hiyo ya ghorofa mbili, aliwataka wananchi na waalimu, kushirikiana ili itowe wataalamu wa fani mbali mbali, kwa ajili ya taifa lao.

Alieleza kuwa, serikali imetumia fedha nyingi katika ujenzi wa skuli hiyo, sasa ili matunda yake yarudi serikali ni kuongeza ufaulu ambao utasababisha upatikanaji wa wataalamu hapo baadae.

Alieleza kuwa, kumalizika kwa ujenzi wa skuli hiyo mwanzoni mwa mwaka ujao, utakwenda kuondoa moja kwa moja mikondo mitatu, ambayo hapo awali ilikuwa katika maeneo hayo ya Mwambe.

‘’Naelezwa kuwa, ndani ya miaka hii mitatu ya uongozi wa Dk. Mwinyi, samba mba na miaka 60 ya mapinduzi, ndani ya jimbo hili la Kiwani, tumeshajenga skuli tatu za ghorofa, ikiwemo za Mwambe na ile ya Kiwani,’’alieleza.

Hata hivyo, Spika huyo wa Baraza la Wawakilishi, aliwataka wananchi wa Mwambe, kuitunza skuli hiyo mara itakapomalizika, ili iweze kutumiwa na vizazi vijavyo.

Mapema Naibu Katibu Mkuu wizara ya Elim una Mafunzo ya Amali Zanzibar, Mwanakhamis Adam Ameir, alisema ujenzi wa skuli hiyo, ni miongoni mwa mikakati ya serikali, katika kuweka elimu kipaumbele cha pekee.




Alisema, serikali ya awamu na nane, tokea ilipoingia madarakani imeweka mikakati ya kuimarisha miundombinu ya elimu, ikiwemo ujenzi wa skuli za ghorofa, ili kupunguza msongamano wa wanafunzi

Naibu Katibu mkuu huyo alieleza kuwa, ujenzi wa skuli kama hizo unamawanda mapana ya kuondoa mikondo mwili kwa skuli zote za Unguja na Pemba, ili kuwapa waalimu nafasi nzuri zaidi za kufundisha.

‘’Kwa mfano hapa Mwambe, tulikuwa na mikondo mitatu, lakini mwanzoni mwaka huu, tulishafungua skuli moja ya ghorofa na leo, tunaweka jiwe la msingi skuli hii, iliyopo Chanjaani, haya yote ni kuona wanafunzi wanapata muda wa kujifunza,’’alieleza.

Aliongeza kuwa, eneo la Mwambe kwa sasa lina skuli tatu za msingi, ambazo zinajumla ya wawanafunzi wa msingi na maandalizi 4,658, wakiwa na vyumba 68 vya kusomea.

“Lengo la serikali ni kuongeza vyumba zaidi vya kusomea, ili kufikia lengo la serikali, la kuwa na wanafunzi 45 kwa kila darasa moja,’’alifafanua.   

Kwa upande wake Naibu Waziri wizara ya Elim na Mafunzo ya Amali, Ali Abdull-ghulam Hussein alisema ujenzi wa skuli hiyo, ni utekelezaji wa vitendo, wa maana ya mapinduzi daima.






Alieleza kuwa, Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi wakati akilihutubia Baraza la Wawakilishi, alieleza kutotaka hadithi ya Mapinduzi, bali sasa ni kuwaonesha wananchi matunda yake.

‘’Ujenzi wa skuli kama hii ya Mwambe, tayari sisi wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, wakati tukiadhimisha miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, tumeshazijenga 21 kwa Unguja na Pemba, lengo ni kuondoa msongamano mdarasani,’’alifafanua.

Mapema Mkuu wa wilaya ya Mkoani Khatib Juma Mjaja, alisema Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, yalifanyika ili kuwakomboa wananchi na kupata haki zao.

Alieleza kuwa, sasa ndani ya miaka 60, watoto wa kinyonge wanapata haki ya elimu, matibabu, maji safi na salama na hata miundombinu ya barabara.



Ujenzi wa skuli hiyo ya ghorofa, ulianza Mei, 2023 na unatarajiwa kukamilika mwanzoni mwa mwezi Januari 2024, ambapo inajengwa na kampuni ya Mwinyi Bulding na kusimamiwa na wakala wa majengo Zanzibar ‘ZBA’ na sasa umefikia asilimia 60.

Skuli hiyo yenye vyumba vya kusomea 29, vyoo 25, ofisi nne za waalimu, ukumbi mmoja wa mitihani, maabara, chumba cha kompyuta na maktba moja, hadi kukamilika kwake itagharimu shilingi bilioni 4.6.

                    Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch