Skip to main content

ZAWA WASAKENI MAFUNDI WA MAJI MITAANI - KADUARA

 



Na Salma Lusangi

WAZIRI wa Maji, Nishati na Madini Zanzibar Shaibu Hassan Kaduara ameagiza Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) kuwatafuta na kuwachukulia hatua mafundi wa maji wa mitaani ambao wanaunga maji kwa wananchi kinyume na Sheria zilizoekwa na Wizara yake.

Akizungumza katika kikao na uongozi pamoja na wafanyakazi wa ZAWA huko Gombani, Pemba mwishoni mwa wiki aliwataka watendaji hao kuwatambua  wateja wao pamoja na kuwasaka mafundi wa maji wa mitaani ambao wanaunga maji kwa watu kinyume na Sheria.

Alisema Wizara ya Maji, Nishati na Madini kupitia taasisi yake ZAWA imeshatoa muongozo kwamba watu wanaohitaji kuungiwa maji wafike katika ofisi hiyo kwaajili ya kujisajili.

“ ZAWA hamuwajui wateja wenu, hamuwatambui mafundi wa mitaani! Mapato ya maji yanapotea kwasababu hamjawajibika ipasavyo. ZAWA watambueni wateja wenu, mafundi wa mitaani wanaowaungia watu maji kinyume na sheria ”. Alisema kaduara

Pia alisisitiza umuhimu wa ZAWA kujipanga katika kukusanya mapato ya maji. Alisema endapo taasisi hiyo itajipanga vizuri katika ukusanyaji wa mapato basi wataweza kujilipa mishara mizuri sana na fedha zingine zitabakia.

“Mkisimamia mapato vizuri basi mnaweza kujilipa mishara na pesa ya chenji zitabaki, simamieni mapato vizuri, kwani siku za nyuma makusanyo yalikua yanaenda vizuri, Mji wa Wete tu, mkisimamia vizuri basi mapato yataongezeka” Alielezea Kaduara.

Aidha Waziri huyo alikemea tatizo la uwepo wa makundi ndani ya ofisi, ununuzi wa vifaa ambavyo sio sahihi kwa maana ya kutokua na vigezo vinavyotakiwa. Pamoja na kuwataka watendaji hao kusameheana endapo mtu amekwanzana na mtumishi mwenzake. Alisema kwani bila ya kusameheana watendaji hao hawataweza kufanya kazi kwa pamoja na kufikia malengo yaliyokusudiwa.



 Naye Katibu Mkuu wa wizara hiyo Joseph Kilangi aliwakumbusha watendaji hao nidhamu ya kazi, lugha nzuri kwa wateja  wao, umuhimu wa kusimamia matumizi sahihi ya fedha kwa kufuata mfumo uliyowekwa na Serikali, pamoja  na kuwahimiza kujibu hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) haraka.

Aidha aliwataka watendaji hao kuwa wabunifu wa kubuni miradi ya maendeleo ambayo italeta tija kwa Serikali na wananchi. Alielezea kwamba kuna baadhi ya Idara/Taasisi hazina miradi.

Aidha Katibu Mkuu huyo aliwataka mafundi wa ZAWA wasifunge mota za maji bila ya kushirikiana na wataalamu wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) kwa sababu mota zinaungua, hivyo Serikali inapata hasara zaidi ya milioni mia tano.

“Wizara yetu inamgusa kila mtu tujitahidi kuzuia malalamiko na kuzuia malalamiko hayo  ni kuwajibika, nidhamu, sisi tuliyopo ofisini tunatakiwa tutowe ripoti ya miaka miwili ya uongozi wa Rais Zanzibar Dk. Hussein kwa kuangalia ilani, hivyo timu iliyopo chini ya Afisa Mdhamini Pemba itekeleze wajibu wao” Alisema Kilangi.

                            Mwisho

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch