Skip to main content

WAZEE WA ZANZIBAR WASEMA JAMBO

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA

KILA ifika Oktoba 1 ya kila mwaka, dunia huadhimisha siku ya wazee.

 

Siku hii kihistoria, iliaanzishwa na Baraza kuu la Umoja wa Mataifa ‘UN’ kuanzia Disemba 14, ya mwaka 1990.

 

Ambapo maadhimisho haya, ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Vienna wa mwaka 1982, kwa ajili ya wazee duniani,“The Vienna International Plan of Action on Ageing”.

 

Ulioboreshwa tena na Mkakati wa Madrid, Hispania wa mwaka 2002, ili kuweza kupambana na changamoto za wazee katika karne ya 21, na kuendelea mchakato wa maendeleo fungamani ya binadamu kwa ajili ya wote.

 

MWELEKEO NA HISTORIA

Maadhimisho ya siku ya wazee duniani, ni moja kati ya jitihada za Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ‘UN’ katika kutambua na kuihamasisha jamii, kuwalinda na kutetea haki zao msingi za wazee duniani kote.

 

Kwa maadhimisho ya mwaka 2021, yalinogeshwa na kauli mbiu “Matumizi Sahihi ya Kidigitali kwa Ustawi wa Rika Zote.”

 

Inatambuliwa kuwa, takriban watu milioni 700 kwa sasa, wamepindukia umri wa miaka 60, na ifikapo mwaka 2050, watu bilioni 2, ambayo ni zaidi ya asilimia 20 ya idadi jumla ya watu duniani, watafikisha umri wa miaka 60 au zaidi.

 

Kuongezeka kwa idadi ya wazee duniani, litakuwa jambo kubwa na litakalokwenda haraka zaidi katika dunia ya sasa, inayoendelea huku bara la Asia, likiwa na idadi kubwa ya wazee na Afrika nayo ikifuata kuwa na idadi hiyo kubwa ya wazee.

Kwa kuzingatia hayo, wazee wanamahitaji makubwa na kuzeeka au kuwa mkongwe hakuondowi utu na haki zao za msingi za mwanadamu, kama inavyosema ripoti ya Umoja wa Mataifa juu ya kuadhimisha siku kimataifa ya wazee duniani.

 

Umoja huo ulianzisha siku hii, kwa lengo la kutoa ulinzi kwenye masuala ya uhuru, ushiriki, huduma, heshima na utu wao.

 

Ingawa ripoti za utafiti za hivi karibuni zinaonesha kwamba, wanawake na wazee hawapati nafasi sawa wanapohusika masuala ya kidijitali.

 

Kwa sasa watu milioni 125 ni wazee, kuanzia umri wa miaka 80 kwenda juu, na serikali zikiendelea kujipanga, ili kuhakikisha wazee wanaishi maisha mazuri na ya amani.

 

Katika hilo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, anasema wazee ni lazima wapewe kipaumbe katika kukabiliana na ugonjwa, kama vile ukoma, corona, ukimwi na kifua kikuu.

 

Amesema ni lazima watu waangalie namna wanavyowashughulikia wazee, katika maisha yao, ili wabaki salama na kuishi kwa amani kama yalivyomakundi mengine.

 

‘’Kila mkongwe (mzee) anahitaji heshima, na kutambuliwa utu na mchango wake kwa jamii yake na taifa, ili kufikia malengo yake,’’anasema.

Kwa upande wa Tanzania bara, Serikali ipo katika hatua za mwisho za mapitio ya Sera ya Taifa ya Wazee ya mwaka 2003, kwa kushirikiana na wadau na imeendelea kutekeleza afua mbalimbali zinazolenga kutatua changamoto zinazowakabili wazee.

 

Hayo aliyasema waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Dorothy Gwajima, alipotembelea makazi ya wazee wasiojiweza ya Sukamahela kuelekea siku ya wazee duniani.

ZANZIBAR

Wakati dunia ikiadhimisha siku ya wazee hapo Oktoba 1 hapa Zanzibar, ambapo rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi akitarajiwa kuwa mgeni rasmi, wazee wanakumbukwa mno.

Kwa Zanzibar, serikali iliamua wazee kuanzia miaka 70, walipwe pencheni jamii ya shilingi 20, 000 kila mwezi, hata kama wazee hao, hawakuwa watumishi wa umma.

Amekuwa akirejea kauli yake kuwa, azma ya kupunguza umri huo ili kuangalia uwezekano wa miaka 65 walipwe pencheni jamii, linafanyiwa kazi kwa haraka.

‘’Wazee wetu fedha mnazopata za shilingi 20,000 kwa kila aliyefikisha umri wa miaka 70, ni ndogo na tunajua kuwa maisha yamepanda, lakini tunangalia uwezekano wa kuongeza fedha hizo na kupunguza umri,’’alieleza.

KAULI YA WAZEE KUELEKEA SIKU YAO

Ali Haji Ali wa Pujini, anasema yapo mambo mazuri ya kujivunia, ambayo, yanatokana na matayarisho na kuweka mazingira rafiki na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

‘’Hata kupewa pencheni jamii za shilingi 20,000 ni eneo moja, lakini hata kuwepo kwa madirisha maalum ya kutokewa dawa kwenye hospitali za serikali, nalo ni zuri,’’anasema.

Mwanajuma Issa Haji ‘Mwaju’ anasema, wazee wote wanakabiliwa na changamoto, ingawa wanawake ndio wanaongoza kwa kutelekezwa.

‘’Wazee tunakabiliwa na changamoto za kutelekezwa na familia na wakati mwengine huwa tunajiingiza kwenye omba omba bila ya kupenda, jambao ambalo sio zuri,’’anasema.

Mussa Iddi Mussa wa Wawi, anasema wakati umefika sasa kwa jamii, kuungana pamoja katika kuwalinda wazee, ili nao waishi kwa salama na amani.

VIONGOZI WA SERIKALI

Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, anasema kila mmoja, kwa wakati huu awatendee mema na mazuri wazee, maana uzee ni njia kila mmoja atapita.

‘’Kama kuna sheria ambayo inakandamiza kundi la wazee, muda ndio huu kwa vijana wa leo, kuzirekebisha ili kesho na keshokutwa ziwafae na wao,’’anashauri.

Mkuu wa wilaya ya Mkoani Khatib Juma Mjaja, anasema hakuna namna ya wala mbadala, juu ya kuwatunza na kuwaenzi wazee, maana ndio wazazi wa vijana wa leo.

Anasema, wakati huu Zanzibar ikitarajiwa kuungana na dunia katika maadhimsho ya siku ya wazee hapo Oktoba 1, kila mmoja na kwa nafasi yake, awatunze wazee.

‘’Angalia eneo la kazi ulipo, kama ni hospitalini, dereva, kiongozi sehemu za kazi, mwanasheria na mwengine atumie nafasi yake kuwasaidia wazee,’’anasema.

Aliyekuwa Afisa mdhamini wizara ya Afya Pemba dokta Yakoub Mohamed Shoka, aliwahi kusema kuwa, suala la kuwa mzee na kubezwa kwa haki zao halihusiani.

WADAU WA HAKI ZA BINADAMU

Mratibu wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ Zanzibar ofisi ya Pemba Safia Saleh Sultan, anaona moja ya jukumu la kisheria kwa jamii, ni kuwatunza wazee.

Mwanasheria wa kujitegemea Mohamed Hassan, anasema haipendezi kwa familia, kuacha kumlea mzee wao na kumkabidhi serikalini.

‘’Matunzo ya wazee walioko serikalini, huwa mara nyingi ni wale waliokosa watunzaji madhubuti, na hivyo ni vyema kuhakikisha familia inawalea wazee,’’anaeleza.

Aliyewahi kuwa mjumbe wa jumuiya ya wazee na wastaafu Zanzibar kwa upande wa Pemba Sifuni Ali Haji, anasema licha ya serikali kuweka mazingira rafiki kwa wazee, lakini utekelezaji bado hafifu.

‘’Siku ya wazee duniani ni jukwaa kwa wazee na watetezi wa haki zao, kujadili changamoto na mafanikio yao, ili kuona mwelekeo wa baadae,’’anasema.

VIJANA

Mratibu wa vijana Pemba Ali Mussa, anasema kama vijana wa leo, wanaelewa iko siku atakuwa mzee wa nchi hii, ahakikishe sasa wanatengeneza mazingira imara kwa wazee.

Kijana Kheir Juma Mrisho, anasema haipendezi kuona vijana wanawadhalilisha wazee, kwa sababu ya kukosa uwezo wa kimwili na fedha, maana uzee ni kama barabara.

‘’Vijana wa leo, lazima tukumbuke kuwa kesho sisi ndio wazee, hivyo maslahi yao na haki zao zitunzwe, ili hapo baadae zetu iwe rahisi,’’anasema.

Siku ya wazee duniani, huadhimishwa kila ifikapo Oktoba 1 ya kila mwaka, ambapo kwa mwaka huu, rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.

Katika maadhimisho, Dk. Mwinyi anatarajiwa kuwakabidhi wazee 689 wa mkoa wa mjini wa Magharibi Unguja, vitambulisho maalum, ambavyo watavitumia katika maeneo mbali mbali.

Kwa mujibu wa waziri wa wizara ya Maendeleo ya Jami, Jinsia, Wazee na Watoto Zanzibar Riziki Pemba Juma, anasema, vitambulisho vyengine 24,000 vinaendekea kuvitengeneza na baadae, vitasambaazwa kwa wazee wengine ambapo Zanzibar ikikadiriwa kuwa na wazee 28,706.

             Mwisho  

       

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch