Skip to main content

'NJOONI MUFANYE MAZOEZI YA VIUNGO VILABU ''FULL NIDHAMU'

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA

WANANCHI kisiwani Pemba, wameshauriwa kujiungu na vikundi vya mazoezi ya viungo, kwani vimejiwekea utaratibu mzuri, ambao unapingana na utovu wa nidhamu kwa wanamaoezi.

 

Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa muda wa Umoja wa vilabu vya mazoezi ya viungo Pemba ‘PAFIC’ Khalfan Amour Mohamed, wakati akizungumza kwenye mafunzo ya siku moja, kwa wanamazoezi wa vilabu hivyo, yaliyofanyika skuli ya msingi Mchanga mdogo wilaya ya Wete.

 

Alisema, wamekuwa wakisemwa vibaya na baadhi ya watu, kuwa ndani ya vilabu vya mazoezi kuna kuvunjiana heshima, jambo ambalo sio sahihi.

 

Alieleza kuwa, wamekuwa na utaratibu mzuri ambao jinsia moja na nyingine, hazivunjiani heshima, hivyo kama wapo waliokuwa wakilihofia hilo, wasiwe na wasi wasi nalo.

 



Katibu huyo wa muda alifafanua kuwa, wanachama wa vilabu vyote, wamekuwa wakielimishwa kila siku, juu ya umuhimu wa kuheshimiana na kulindiana nidhamu, ili lengo la kufanya kwao mazoei lifikiwe.

 

‘‘Kama wapo wananchi wenzetu walikuwa na wasiwa wasi, na vilabu vya mazoezi kwamba vina jambo jengine lililokinyume na maadili linafanyika, waondoe shaka hiyo na vikundi viko salama,’’alieleza.

 

Akizufungua mafunzo hayo Afisa Mdhamini wizara ya habari, vijana, utamaduni na Michezo Pemba, Mfamau Lali Mfamau, alivishauri vilabu vya mazoezi, kuanzisha na michezo mengine ndani yake.

 


Alieleza kuwa, kwa vile lengo lao ni kufanya mazoezi kama afya, sio vibaya wakaangalia kushiriki kwenye michezo kama mpira wa miguu, mikono, kikapu na mpira wa meza ili kuongeza idadi ya wanachama.

 

‘‘Inawezekana hamupati watu wengine kwa sababu, wengine hawapendi kufanya mazoezi ya viungo pekee, lakini kama mtaanzisha michezo mengine itakuwa sehemu pia ya kuifufua,’’alieleza.

 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa muda wa Umoja wa vilabu vya mazoezi Pemba Ali Hamad, alisema mafunzo hayo ni kwa ajili ya waalimu wa mazoezi na wasaidizi wao, ingawa hapo baadae itakuwa ni kwa ajili ya wanachama wengine.

 


Alisema, mafunzo hayo yalitokana na vikao mbali mbali ya viongozi wa vilabu vya mazoezi kutoka wilaya nne za Pemba, baada ya kuwepo changamoto ya nidhamu kwenye vilabu vyao.

 

‘’Ndio maana ili kujiweka sawa kama tasisi, tumewafundisha nani mwalimu bora, nini maana ya mazoezi, mbinu za kufundisha mazoezi na kuchunga nidhamu,’’alieleza.

 

Mkunzi wa mafunzo hayo, Mwalimu Talib Ali Rajab, alisema kati ya sifa kadhaa za mwalimu bora, miongoni mwao ni kujiheshimu, nidhamu, kujiamini na kujenga upendo.

 





‘’Lakini pia mwalimu anatakiwa awe mbunifu, anayependa kujitolea, kuwajali wenzake, kuwaunganisha, kujiepusha na migogoro pamoja na kuacha vitendo vya udhalilishaji,’’alieleza.

 

Kwa upande wake mkufunzi Ali Siyahi, alisema mwalimu wa mazoezi anatakiwa ajiepushe na kufanya vitendo kwa kasi, kwani wapo baadhi ya wazee hawahimili hilo.

 







Wakichangia mada kwenye mafunzo hayo, mwanamazoezi kutoka Gombani Fitness Club Ali Mbarouk Omar, alisema suala la uvumilivu kwa mwalimu ni sifa nzuri kujipambana nayo.

 

Nao Kassim Ahmed Seif na Siti Hamad Massoud, walisema kwa vile lengo ni kuwa na afya bora, hakuna haja ya kufanywa vitendo vya kiungo kwa haraka kupitilia.

 

Mafunzo hayo yalioandaliwa na Umoja wa Vilabu vya mazoezi ya viungo Pemba ‘PAFIC’ yalivishirikisha vilabu vya Gombani Fitness Club, KMKM Wete, Gando, New Solution, Shumba, Kisauni, Tumbe, Zaphias Chake chake na Mkoani pamoja na wenyeji Kambini Fitness Club.    

             mwisho

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...