Skip to main content

KADUARA ATOA AGIZO ZITO KWA ZECO PEMBA

 




Na Salma Lusangi

WAZIRI wa Maji, Nishati na Madini Zanzibar Shaibu Hassan Kaduara, ameuagiza uongozi wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) kufikisha huduma ya umeme haraka sehemu  ambazo wananchi wameekeza kilimo ili waweze kuzalisha kwa gharama ndogo na nafuu.                          

Aliyasema hayo leo wakati akizungumza watendaji wa shirika hilo  Tibirizi Wilaya ya Chake Chake Pemba.

 Alisema mkulima yeyeto akifikishiwa  huduma ya umeme ataweza kuzalisha mazao kwa gharama ndogo hali hiyo itapelekea bidhaa kuuzwa kwa bei ndogo kwasababu alizalisha kwa gharama ndogo.

Alifahamishwa kwamba Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ameshatoa agizo  nguzo za umeme zitolewe bure kwa wananchi, hivyo ZECO harakisheni kuwafikishia wananchi nguzo za umeme hasa kwa wanaodhalisha mazao mbali mbali ili wapate urahisi wa kuzalisha bidhaa zao.

“ZECO kwanini mnachelewesha kufikisha nguzo za umeme kwa watu wanaozalisha, acheni kuzipigia hesabu gharama za nguzo, hizo peza sio za mtu binafisi ni za serikali,'alieleza.


Pia  Waziri huyo amewataka watendaji wa ZECO kuwajibika ipasavyo katika kuwahudumia wananchi wanaohitaji kufungiwa mita za umeme majumbani mwao wakati wameshalipa gharama zote za fedha zilizohitajika.             

 Alisema hali halisi ya ZECO ilivyo kwa sasa sio ya kusemwa vibaya lakini bado watendaji wa ZECO hawajawajibika ipasavyo hivyo endapo ataendele kupata malalamiko ya wateja kwamba wameshalipa lakini ZECO hawajatimiza wajibu wao wa kuwafungia mita wateja ameahidi atawafukuza kazi baadhi wa watendaji wa Shirika hilo kwa kutokuwajibika.

“ Siko tayari kutolewa madarakani kwasababu ya wafanyakazi wa ZECO kutokuwajibika, nitawafukuza wafanyakazi hata mia (100), kama mtu hana uwajibikaji kwanini aendelee kubaki katika Shirika! Mnafanyakazi kwa uzembe. Mtu akiniharibia tutaharibiana, ukinizingua tutazinguana.Wajibikeni kwanza na baadae mdai haki zenu.

Waziri huo alieleza  kwamba anafahamu wafanyakazi wa ZECO wanadai mishahara yao hivyo ameagiza Utawala wa ZECO kuhakikisha kila mtu anapata haki yake anayodai pamoja na kupewa muongozo wa majukumu yake ya kila siku (Job Descriptions)  kwamujibu wa sheria na kanuni za Utumishi.       


  

 Aidha aliwataka watendaji wa ZECO kusimamia mapato ya huduma ya umeme na kujiepusha na vitendo vya kuhujumu uchumi, kwani katika zoezi la kuwafungia watu mita na kuwasaka watu wanaojiungia umeme kinyume na sharia (Kadua Operesheni) aliwakamata watu sita ambao wanahujumu uchumi.

Naye katibu Mkuu wa Wizara hiyo Joseph Kilangi aliwataka watendaji wa Shirika hilo kutumia vizuri vifaa vya Serikali,  kufuata taratibu za manunuzi pamoja na kuongeza mashirikiano baina yao ili kuleta ufanisi katika majukumu yao.

Pia aliwasisitiza wafanyakazi hao kujiepusha na kosa la utoro kazini pamoja na kutekeleza maagizo yote yalitolewa katika kikao hicho yatekelezwe kwa wakati ikiwemo kuwafungia wateja mita, nguzo za umeme kufikisha maeneo ya wakulima  kwa wakati. Alisema  anahitaji kupata ripoti nzuri.

Kwa upande wao wafanyakazi wa ZECO waliomba kupatiwa mafunzo ya fani tofauti, pamoja na vitendea kazi ikiwemo gari, viatu pamoja na kulipwa maposho yao ya kufanyakaza kwa zaidi ya saa za kazi zilizoekwa kisheria.

Mwisho




Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch