Skip to main content

'MUDA NILIYODAIWA KUBAKA NILIKUWA NAPIGA MSWAKI' MTUHIMIWA PEMBA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA

MTUHUMIWA wa ubakaji, Sabour Juma miaka 47 mkaazi wa Chanjaani wilaya ya Chake chake, ameiambia mahkama ya makosa ya udhalilishaji ya mkoa wa kusini Pemba iliyopo Chake chake kuwa, muda aliyodaiwa kuwa amebaka, alikuwa kwake akipiga msuwaki.

 

Alidai kuwa, maelezo ya mashahidi kuwa majira ya asubuhi alimuingiza mtoto wa miaka 11 ndani ya choo cha nyumbani yake sio sahihi, kwani muda huo alikuwa nje ya nyumba akipiga msuwaki ‘akisugua meno’.

 

Aliyadai hayo mbele ya mahakama hiyo, chini ya Hakimu Muumini Juma Ali, wakati mtuhumiwa huyo aliyekuwa akiongozwa na wakili wake Suleiman Omar, akijitetea, baada ya upande wa mashtaka kufunga ushahidi wao.

 

Alidai kuwa, familia ya mtoto huyo inachoyo naye na imemtengenezea mazingira ili kumshitaki na kumfungisha, na wala hakumumbuki kumbaka mtoto huyo.

 

‘’Sikumbuki kumbaka mtoto huyo wa miaka 11, aliyekuja kutoa ushahidi mahakamani hapa, bali wamenitengenezea zengwe kwa njia ya kunibambikizia kesi hii,’’alidai.

Aidha mtuhumiwa huyo, alidai kuwa hana mazoea na mtoto huyo, na wala hawajahi kumpa fedha za matumizi ya skuli, kama alivyodai, wakati akitoa ushahidi wake.

 

‘’Hata kwangu hakuwa na kawaida ya kuja, na mimi sikuwa nikimfahamu, bali siku moja moja humuona aidha anakwenda au anarudi skuli,’’alidai.

 

Alipoulizwa na wakili wake, Suleiman Omar Suleiman kwa vile ameshamuacha mke wake kwa zaidi ya miaka mitatu sasa, anafanya nini anapojiskia kutaka kufanya tendo la ndoa, na alidai hafanyi maana ni kosa kwa Muumba.

 


‘’Ni kweli mke wangu nimeshamuacha kwa miaka mingi, lakini mimi hata nikijiskia kutakufanya tendo hilo, hujikataza maana kisheria ni kosa,’alisisitiza mtuhumiwa huyo.

 

Baada ya mtuhumiwa pamoja na wakili wake kumaliza kutoa ushahidi wao, Hakimu wa mahkama hiyo Muumini Ali Juma, aliupa nafasi upande wa mashtaka, uliokuwa ukiongozwa na wakili Mussa Khamis Ali na Ali Amour Makame, kumuuliza mtuhumiwa.

 

‘’Je mtuhumiwa Sabour Juma, utakubaliana na mimi kuwa anayejua kuwa tendo la ndoa limefanyika ama halikufanyika ni kati ya mwanake au mwanamme,’’aliiuliza wakili wa serikali Ali Amour.

 

Ambapo wakili huyo, alimueleza mtuhumiwa kuwa, mtoto aliyembakwa alimtaja mtuhumiwa huyo kuwa ndie aliyemfanyia vitendo vya ubakaji wakiwa chooni.

 

Wakili wa serikali nambari mbili, Mussa Khamis Ali, alitaka kujua kutoka kwa mtuhumiwa huyo, sababu ya yeye kuwepo mahakamani hapo.

 

Baada ya maswali ya mawakili hao, Hakimu wa mahkama hiyo Muumini Ali Juma, aliupa nafasi upande wa utetezi pamoja na mtuhumiwa wake, kujadiliana ikiwa wanaweza kuleta shahidi wa utetezi.

 

‘’Mheshimiwa baada ya kuzungumza na mteja wangu, tumeona tupangiwe siku nyingine kuja kuendelea na utetezi wetu, tukiwa na shahidi wetu siku hiyo,’’aliomba wakili wa utetezi.

 

Hakimu wa mahaka hiyo, alikubaliana na ombi la wakili wa utetezi, na kuliahirisha shauri hilo hadi Oktoba 11, mwaka huu.

 

Mapema Septemba 19, mwaka huu mahakama hiyo ilimfutia kosa la utoroshaji mtuhumiwa huyo, na kuendelea na tuhma moja ya ubakaji.

 

Ambapo tendo hilo anadaiwa kulifanya Machi 10, mwaka huu kwa kumbaka mtoto wa miaka 11, ni kosa kinyume na vifungu vya 108 (1), (2), (e) na 109 (1) sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018.

 

                Mwisho     

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch