Skip to main content

RUZUKU YA TASAF YAWAPA UHAKIKA WA KIPATO WANAWAKE TUMBE PEMBA

 





NA HAJI NASSOR, PEMBA

SHEHIA ya Tumbe Mashariki wilaya ya Micheweni Pemba, inawakaazi 7,675 kati ya hao, ni wananchi 225 wanaoendelea kupokea rukuzu kutoka TASAF.

Kati hao, wapo wananchi 20 kutoka ndani ya mpango huo sasa, wameamua kujiajiri na kuendesha maisha yao, kwa kuanzisha miradi kama vile biashara na kilimo cha mboga mboga.

Shehia ya Tumbe iliyoko wilaya ya Micheweni Pemba, ni kati ya zile shehia 78 zinazoendelea kuhudumiwa na TASAF, kwa wananchi wake kuendelea kupokea rukuzu.

Maana TASAF, inao walengwa 14, 280 kwa wilaya zote nne za Pemba, ambao hao wapo walioanzisha vikundi vya ushirika iwe ni utengenezaji sabuni, mboga mboga, ufugaji ama biashara.

Katibu wa sheha wa shehia ya Tumbe Mashariki, Makame Hassan Makame, anasema moja ya shehia ambazo TASAF imeacha alama ya mafanikio, ni yao kwao.



‘’Wapo walengwa wa kunusuru kaya maskini 20, hawa sasa hatuwatarajii kurudi tena kwenye umaskini wa kipato, kama ilivyokuwa kabla ya ujio wa TASAF,’’anaamini.

 Pamoja na hao mmoja mmoja, lakini wapo walioanzisha ushirika wa biashara kilimo cha mboga, ufugaji na hata vikundi vya kuweka na kukopa.

Hapa akatolea mfano ushirika wa ‘kiumbe mzito’ ambao umekusanya wanawake 20, na sasa wameshaanza kufikia pahala pazuri kimaisha.

‘’Ushirika huu ni wale walengwa wa mpango wa kunusuru kaya maskini, na waliamua kujikusanya kwenye kuweka na kukopa na sasa wameanzisha ushirika wa duka la nguo na vipodozi,’’anaeleza.

Katibu anasema, mfano wa vikundi kama hivi shehiani mwake, vipo wengine wanaotengeneza sabuni, kilimo na ufugaji wa kuku.

USHIRIKA WA ‘KIUMBE MZITO’ ULIANZAJE?

Ushirika huu, ni zao la mpango na mikakati ya TASAF ambapo ilikuwa ikiwataka walengwao hao, kuhakikisha ruzuku wanayoipata inazaa matunda.

Hapa Mratibu wa TASAF Pemba Mussa Said Kisenge, anasema pamoja na uwepo wa vikundi 942, lakini ushirika wa kiumbe mzito ni mfano mzuri ndani ya TASAF.



Maryam Haji Khatib ni Mwenyekiti wa ushirika huo, anasema baada ya kupokea ruzuku kutoka TASAF na wakiwa kwenye ushirika wa kuweka na kukopa, walizaa wazo la kuanzisha ushirika huo wa duka.

Ijapokuwa, wapo waliotamani kuanzisha duka la chakula, lakini kwa wakati huo, waliafikiana kuanzisha duka la kivazi, kama nguo za kike na viatu.

Kwenye ushirika huu, ambao unawanachama 18, kila mmoja kwa kuanzia alichanga shilingi 5,000 na kwa hatua za mwanzo wakajipatia shilingi 90,000.

Kisha waliendelea na mchango kwa miezi minne, na wakajitilia kibindoni shilingi 700,000 kwa dhamira ya kuanzisha ushirika huo wa duka la viatu na nguo.

‘’Kwa hatua za mwanzo tulinunua nguo za watoto, viatua aina ya yebo yebo, vishungi, kanga, mahafu, sidiria, shati, suruali na badhi ya vipodozi,’’anasema Mwenyekiti.

Ushirika huo ambao uliasisiwa mwaka 2019, hauwajahi kugawa faida, ingawa hadi mwishoni mwa mwaka 2021, baada ya kufanya hesabu, walijikuta na mtaji wa shilingi milioni 1. 

Ambapo baada ya kutoa mtaji wa shilingi 90, 000 wamejikuja na faida ya shilingi milioni 1 na elfu kumi.  

Fatma Hamad Mkandi, ni Katibu wa ushirika huo wa ‘Kiumbe Mzito’ anasema hawajagawa faida, kutokana na kuwa na ushirika wa kuweka na kukopa.

Anasema, wote waliomo kwenye ushirika wa duka, wanakutana kwenye ushirika wa kujiwekea fedha na kukopa, ambako wanachama hukopeshwa.

‘’Jinsi ushirika wetu unavyokwenda kwa sasa hata akitokea mfadhili akitukopesha shilingi milioni 200 tunajiamini kuzichukuwa na kurejesha taratibu.

‘’Kama tukikopeshwa fedha hizo, kwanza tutanunua mashine za kukobolea nafaka, mashine ya kutengenezea sabuni, masheni ya kutotolea vifaranga na kujenga ofisi yetu,’’anaelezea ndoto zao.

Katibu anasema malengo yao ya baadae, ni kuona kila mwanachama kati ya wale 18, awe anajitegemea katika kuendeleza maisha yake.

''Tunatamani iwe suala la shilingi 100,000 hadi shilingi 500,000 kwa mwanachama anapohitaji kwa ajili ya kukidhi mahitaji yake,''anasema.

Kwa sasa, hali ya maisha kwa wanachama wao, imebadilika hasa baada ya kuwa na sehemu ya uhakika wa maisha ‘kukopa’ ambapo hapo kabla hawakuwa na pakwenda.


Yupo mwanachama ambae aliwahi kupata msiba kisiwani Unguja, na alifika kwenye ushirika na kikundi, na kukopeshwa shilingi 100,000.

‘’Hata mimi niliwahi kukopa shilingi 200,000 kwa ajili ya matibabu ya mtoto wangu na yupo mwengine alikopa hadi shilingi milioni 1, na baada ya miezi sita alirejesha,’’anasema.

Hapa mshika fedha wa ushirika huo Awena Shavuu Abdalla, anasema kwa siku msimu kama wa sikukuu, huuza kati ya shilingi 80,000 hadi shilingi 100,000.

Anasema kwa sasa, wanaendelea kuutumia mlango wa kuazimwa, ingawa wanatarajia kuona wanakuwa na wao ili kupunguza gharama.

KABLA YA TASAF

Kwanza hawakufikiria kuanzisha ushirika wa duka wala mpango wa kuweka na kukopa, kutokana na kukosa chanzo cha kuyafanya hayo.

Asiya Faki Suleiman, ambae ni mwanachama, anasema hali ya ukosefu wa kipato kwake ilikuwa ya kawaida, na hakuja wapi aende.

‘’Hata ukibahatika kumpata mtu, lakini sio kumuazima fedha, labda nguo ama chakula, maana kila mmoja kwa hapa kijijini kwetu, fedha ilikuwa ngumu,’’anasema.

Anakumbuka vyema, hakuwa mtu wa kutoa mchango wa harusi, ugonjwa wala matanga katika familia yake, kutokana na kukosa shughuli ya kufanya ya kujiingizia kipato.

Fatma Hamad Mkandi, anasema kipato kwake kilikuwa kizito, hadi anapoamua kwenda kwenye kilimo cha mwani, ambako fedha yake haina haraka.

‘’Utegemee mwani mpaka ukauke, na kisha waje wanunuzi kwa siku watakazo, na hapo ukimaliza kuuza ni kulipa deni, ambalo umekopa,’’anasema.



TASAF

Mratibu wa TASAF Pemba Mussa Said, anasema wapo walengwa 14, 280 kwa Pemba ambao wanaendelea kupata fedha za kunusuriwa na umaskini.

Walengwa hao wapo kwenye shehia 78, ikiwemo ya Tumbe Mashariki, ambapo tayari shilingi bilioni 14. 4 zimeshwafikia.

‘’Mtu kama bi Fatma ndio hasa malengo ya TASAF ya kumtoa mwananchi katika unyonge, na kumleta kwenye taa, ili nae aishi maisha mazuri,’’anasema Mratibu.

“TASAF inaorodha ya zaidi ya walengwa 50,000 kutoka wastani wa walengwa 15 kila shehia, kati ya shehia 78, ambao wamenzisha miradi ya kujikwamua.

“Mtu kama bi Fatma wa Tumbe, Amina wa Mgogoni, Mfaki wa Kwale Gongo na Maryam wa Ukunjwi ambao hatuna shaka, hawawezi kurudi tena kwenye umaskini mzito wa kipato, wanafikia 50,000 kwa Pemba yote,’’anaeleza.

Mratibu Mussa anabainisha kuwa, kwa mwaka 2014/2015 walengwa hao wa kunusuru kaya maskini, waliibua miradi ya kijamii 41, idadi iliongozeka mwaka uliofuata kwa kufikia miradi 84.

Mwaka 2017 hadi mwaka 2018, walijukuta na miradi mengine ya kijamii 21, inayuhusisha upandaji miti kama shehia ya Makangale, uazishwaji wa vitalu na ujenzi wa matuta ya kinga maji ya bahari Ndagoni, Kiwani, Micheweni na Tumbe.

Achia mbali idadi ya watu 50,000 waliojiwekeza wenyewe, vipo vikundi 942 vikizaa walengwa 12,000 vilivyoanzishwa, kuanzia mwaka 2014 hadi sasa.

WANANCHI WA KAWAIDA

Rukia Omar Kheir, anasema fedha zilizoekezwa kunusuru kaya maskini kutoka TASAF, zimetumika vizuri kwa vile matunda yanaoonekana kwenye shehia yake.

‘’Kama TASAF ikiondokana inataka kuacha alama ya maendeleo, basi mfano mzuri ni kwa shehia ya Tumbe Mashariki, ambapo sasa wanawake wameshaukimbia umaskini kwa vitendo,’’anasema.

Hata Aisha Issa Hassan na mwenzake Is-mail Haroun Juma wanasema, kilichobakia kwa sasa ni tasisi nyingine kuvilea vikundi kama hivyo.


WATEJA WAO

Omar Haji Issa na mwenzake Khadija Bakar Juma wanasema, sasa hawafuti tena huduma za nguo na viatu Wete mjini (kilimo 30) baada ya ushirika huo kuweka duka.



                     Mwisho           

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch