NA
HAJI NASSOR, PEMBA@@@@
‘’TUMESHAWAHI kusimamisha shughuli ya harusi
kwa dakika 10, mke asichukuliwe, baada ya kugundua hatujamtia pambo la kipini cha
pua,’’anasema Rehema Faki Shehe (60) wa Kwale Micheweni Pemba.
Ilishazoelekea kuwa, kuwa mapambo ni aina ya mafuta,
podari, pete, mkufu, udi, wanja na hina, ingawa kwa wanawake wilaya ya Micheweni,
kipaumbele ni utoboaji wa pua kwa ajili ya utiaji wa kipini.
Utamaduni wa utoboaji (utomoaji) wa pua tena ya upande wa
kushoto, wenyewe wanawake wa Micheweni waliurithi zaidi ya miaka 200 iliyopita.
Kwa mfano, Rehema Faki Shehe (60) alimkuta bibi yake wakati
akiwa huo akiwa na miaka 50, akiwa ametobolewa tundu la upande wa kushoto ya
pua, akiwa na kipini.
KINA
MAAGA GANI KIPINI CHA PUA?
Sharifu Massoud Hamad (60) wa Kwale Micheweni mkoa wa
kaskazini Pemba, anasema moja ni tofauti kati ya mwanamke na mwanamme.
Anaona hata unapokuta wamevaa mavazi yenye kufanana,
lakini dalili kubwa ya tofauti hiyo, ni kumuangalia kwenye mlango wa tundu ya
pua ya upande wa kushoto, atakuwa na sehemu ya kuwekea kipini.
‘’Ukifika miaka kati ya mitano hadi minane, lazima kwa mtoto
wa wilaya ya Micheweni apelekwe kwa mtoboaji na afanye hivyo, ili ajitayarishe
kwa baade kuweka kipini,’’anasema.
Saada Said Kombo (68) anasema, kwa umri wake huo hakukuwa
na dada yake wala mdogo wake wa kike ambae hakutobolewa pua, kwa ajili ya kuwekewa
kipini.
Anasema kila familia imekuwa na mtoboaji wake maalum, tena
huwa bila ya malipo, kwa kila mmoja.
NANI
ANAVA AKIPINI?
Kumbe uvaaji wa kipini ni kwa ajili ya mwanamke ambae
tayari ameshaolewa pekee na sio mwengine, ambae bado hajafunga ndoa.
Hii wanasema, utamaduni unasindikiza kwa namna ya
kumtofautisha kati ya mwari ‘kigori’ na mtu aliyekwishaolewa au mjane.
Aisha Hamad Shamata (65) anasema, tena ilishamtokezea mara
mbili katika maisha yake, bibi harusi kumzuia kwa dakika 10, baada ya kusahau
kumtia kipini.
Anasema, hakuna hata pambo moja ambalo ni muhimu na la
lazima kwa harusi wa kike wa Micheweni, kama sio kipini cha pua.
Fatma Hamad Ali (40) anasema, hata yeye alipoolewa
alilazimika wiki tatu kabla ya harusi yake, kutobolewa pua, kwa vile hakulelewa
eneo hilo na alikosa huduma hiyo awali.
‘’Kwa mfano mimi sikulelewa Micheweni, ingawa ndio kwetu
lakini nililazimika kutobolewa, ili kuiheshimisha ndoa na familia
yangu,’’anasema.
Kweli anasema, mwanamke alimpenda mno baada ya kumkuta
akiwa na kipini cha pua, na hayo anasema aliyabaini siku waliokwenda kuwasalimu
wazazi, wiki mbili baada ya harusi yao.
Aisha Hashim Said (25) anasema wao ni utamaduni
waliourithi na imekuwa vigumu hasa ikiwa utalelewa Micheweni, kuuacha.
Halima Ibrahim Khamis (30) na mwenzake Hadia Ramadhan
Himid (22) wanasema, ingawa siku ya kutobolewa hupata maumivu, lakini haiwi
kikwazo kwa wingine kutobolewa.
‘’Maumivu yake kama sindano ya kawaida, lakini ninachoamini
kama unataka uzuri, lazima kwanza uzurike,’’anasema Halima Ibrahim Khamis.
Maryam Issa Khamis anasema yeye alikataa kutobolewa pua
akiwa na miaka 20, na aliolewa hadi sasa ana watoto watano, akiwa kwenye ndoa
bila ya kipini.
‘’Kama hutaki kutobolewa, wenzako wingine wanakucheka wingine
wanakuunga mkono na unaolewa bila ya shida,’’anasema.
WANAUME
WA MICHEWENI WANASEMAJE?
Wanasema, kama wanawake
waliowaoa hawakuwakuta na utamaduni huo, huwa na maswali yanayokosa majibu
vichwani mwao.
Kwa mfano Faki Khamis Kai (64) anasema, moja ya pambo
ambalo haliishi hamu, ni uwepo kwa pua yenye kipini kwa mke wake.
Kwao suala la udi, hina, piko, podari na asumini yapo kama
mapambo ya ujumla, ingawa utamaduni wa utoboaji wa pua na kuweka kipini huwa
ndio kipaumbele.
‘’Hata sisi kwenye vikao vyetu, huwa tunataniana na
kuelezena kuwa, ikiwa mwanamke hana kipini cha pua hana tofauti na
mwanamme,’’anasema.
Khamis Juma Khamis (73) anasema kipini cha pua ndio mpango
mzima kwa mke, na mapambo mingine kama udi, hina na piko ni vitu vya kuondoka.
‘’Hata kama mwanamke anaumwa, au wewe mwanamme unaumwa,
bado mke anakuwa anakupendezesha kwa kule kuwa na mng’ara pua kwa
kipini,’’anasema.
Kwao hawajali na wala hawashughuliki aina ya kipini, kiwe
cha dhahabu, almasi, silva hata cha kutengeneza kwa mali ghafi zinazotoka
Micheweni, kwao huvutia.
Issa Hamad Shehe (25) anasema hata vijana wa leo utamaduni
wa utoboaji pua, wanaupenda kwa wake zao, maana ndio pambo lisilo na gharama.
‘’Udi mpaka uwe na shilingi 1,000 kila baada ya muda, piko
na hina zinawakati huchakaa kama ilivyo kwa udi, lakini kipini mpaka mtu anafariki,’’anasema.
Kombo Haji Simba (35), anasema ni aibu kubwa kwao kuoa mke
ambae mmetakana na familia yake, kukosekana kwa pambo la kipini cha pua.
HISTORIA
YA UTOBOAJI WA PUA
Kwa zaidi ya karne tatu (miaka 300), hapo zamani wanawake
wa jamii ya Kihindi na wale wa mwambao wa pwani hasa Tanga, walinza kutoboa
sehemu katika pua.
Pia kwa wakati huo, halikuwa jambo la ajabu kuweka jino la
dhahabu na hata kutoboa masikio yote mawili.
Ingawa historia inaonesha, unapotoboa pua, lazima kisha
uweke kipini cha dhahabu, baada ya maumivu kupona na sio kweka jambo jingine
lolote.
Kutoboa
pua kumekuwepo kwa miaka mingi, katika ustaarabu tofauti ambao, umetumia
kurejelea vitu tofauti.
Ukubwa
wa mapambo ya kujitia puani yalikuwa na maana ya utajiri wa kifamilia kwa
makabila katika Afrika na Mashariki ya Kati.
Na
mithili ya pete za pua zinadaiwa kutolewa kwa marafiki wa kike wapya na waume
zao, kama hatua ya usalama.
Vivyo
hivyo, ustaarabu wa Amerika ya Kati na Kusini umetumia kutoboa kwa septamu na
mapambo yao kama alama za hadhi.
Katika
jamii ya kisasa ya Magharibi, kutoboa pua kunahusishwa na tamaduni anuwai kama
punk, tamaduni mbadala, na tamaduni ya bohemia.
Kutoboa
pua hakuhitaji tu tahadhari na uvumilivu wa maumivu, lakini muhimu zaidi kuliko
inavyosikika.
Kutoboa ncha ya pua ya wima
ni kutoboa pua ya kipekee na nadra, ambayo hutembea wima, kama jina
linavyopendekeza, kutoka juu tu ya ncha ya pua hadi chini tu ya ncha ya pua.
Kwa sababu ya muundo wa pua
yako, baa iliyopindika kwa kweli ni mapambo pekee yanayokubalika kwa aina hii
ya kutoboa.
ATHARI ZA UTOBAJI PUA USIOZINGATIA UTAALAMU
Maumivu ya pua, yanaweza
kusumbua na kuumiza, na wakati mwingine yanaweza kusababishwa na homa, yenye
kuambatana na mvutano wa misuli kwenye taya.
Daktari Issa Khamis Ali anasema lakini hata kwa mtobolewaji anaweza kukumbwa na shinda kwenye sehemu ya shingo, muoteo wa meno, muwasho usio wa kawaida, kwenye pua ndani na nje.
Mwisho



.jpg)

Comments
Post a Comment