Skip to main content

PP AMSOTESHA RUMANDE ANAYEDAIWA KUUA KWA MAKSUDI

 



 NA MARYAM NASSOR, ZANZIBAR@@@@

MTUHUMIWA wa kesi ya kuua kwa makusudi, inayosikilizwa mahakama kuu Tunguu Zanzibar, inayomkabili Omar Mahmoud Abdallah (36) mkaazi  wa Jang’ombe Unguja, ameendelea kusota rumande, baada ya upande wa mashtaka, kushindwa  kukamilisha  upelelezi wa shauri hilo kwa wakati.

 Mara baada ya kufika mahakamani hapo, mtuhumiwa huyo akitokea rumande, Mwendesha mashtaka kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka Zanzibar Said Ali Said, alimueleza Jaji wa mahakama kuu Zanzibar kuwa, kesi iyo ipo kwa ajili ya kuanza kusikilizwa maelezo ya awali, lakini  bado upelelezi wa shauri hilo haujakamilika.

“Mheshimiwa Jaji leo, kesi hii ipo kwa ajili ya kusikilizwa, lakini bado hatujakamilisha upelelezi wa kesi na mashahidi, hivyo tunaomba utupangie tarehe nyingine, kwa ajili ya kusikilizwa,’’ alidai.

 Baada ya maelezo hayo, Jaji wa mahakama kuu Zanzibar Ali Mohamed Ali, aliwauliza mawakili wa upande wa utetezi uliokuwa ukiongozwa na Ali Rashid Ali na Elia Elisha  kuwa, wanakubaliana na ombi la upande wa  mashtaka.

 Wakili hao walidai kuwa, hawana pingamizi yoyote juu ya ombi hilo, ila wanataka upande wa mashtaka  kujihimu kukamilisha maelezo ya kesi, na mashahidi illi kesi hiyo ianze kusikilizwa.

“Hatuna pingamizi na upande wa mashtaka ila tunataka, wajihimu kukamilisha  maelezo ya kesi, ili mteja wetu ajuwe hatma yake mapema,” walidai mawakili hao.

Jaji wa mahakama hiyo, aliuliza  upande wa mashtaka kuwa ni lini,  watakuwa wameshakamilisha maelezo ya kesi na mashahidi na kujibu hivi karibuni.

Jaji huyo, aliutaka upande wa mashtaka kuwa wanatakiwa kukamilisha maelezo ya kesi na mashahidi kwa wakati, ili kesi hiyo ianze kusikilizwa.

Kwa mara ya kwanza shauri hilo, lilisomwa mahakamani hapo  August 29  mwaka 2023 na kuhairishwa miezi mitatu  mfululizo, kutokana na kutokamilika kwa upelelezi wa kesi hiyo.

Awali ilidaiwa mahakamani hapo  na mwendesha mashtaka kutoka afisi ya mkurugenzi wa mashtka Zanzibar, kuwa mstakiwa huyo anadaiwa kumuua kwa makusudi kijana Seif Omar Salum.

Mshtakiwa huyo, alitenda kosa hilo, Jang’ombe wilaya ya Mjini, mkoa wa mjini Magharibi Unguja, majira ya saa 1:00  usiku.

Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa, kutenda  hivyo ni kosa kinyume na kifungu  cha 179 na 180 chini ya  kifungu namba 6 cha mwaka 2018 sheria za Zanzibar.

Jaji huyo, aliutaka upande wa mashtaka kukamilisha  upelelezi wa shauri  hilo, ili  kesi hiyo ianze kusikilizwa mahakamani hapo na kuihairisha kesi hiyo hadi Machi 20 mwaka huu, kwa ajili ya kusikilizwa maelezo ya awali na mtuhumiwa kurejesha rumande.

                                    MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch