Skip to main content

WALIOEKEZA SHILINGI 55,000 MISOONI UPANDAJI MIGOMBA KUCHEKELEA MAVUNO

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

USHIRIKA wa ‘tudumishe maendeleo’ uliopo Misooni shehia ya Shungi wilaya ya Chake chake, umesema kama migomba yao 50 walioipanda mwaka jana, itazaa kwa pamoja, watajipatia faida ya shilingi 195,000.

Kwani ushirika huo umetumia shilingi 25,000 kwa ununuzi wa miche 50 ya migomba aina ya mkono wa tembo, mtwike, kipukusa kwa wastani wa shilingi 500 kila mche mmoja na shilingi 30,000 kwa kulimishia shamba loa kwa hatua ya awali.

Mwenyekiti wa ushirika huo Mbarouk Idrissa Omar, wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi kijijini hapo alisema, waliamua kujikusanya pamoja na kuendesha kilimo hico, ikiwa ni njia moja yapo ya kujikwamua na umaskini.

Alisema, walichagua kilimo cha migomba, kutokana na eneo walilo linakukubali vyema hasa kwa aina ya ardhi yao ilivyo, kilimo hicho ndio kilichoonekana kunawiri vyema, ilikinganishwa na mazao mingine.

Alieleza kuwa, matumiani yao ni kuwa, kama migomba hiyo 50 walioipanda mwezi Januari mwaka jana, na kuzaa kwa pamoja na wanaweza kuvuna ndizi 50 na baada ya kuuza kila moja kwa wastani wa shilingi 5,000 kwa bei ya jumla, watajipatia shilingi 250,000.

‘’Kima hicho sio kidogo, maana hata tukishatoa gharama zetu za miche, mbolea, usafishaji tunaweza kupata faida ya shilingi 195,000 jambo ambalo kwetu sio dogo, maana na shughuli zetu nyingine za binafsi hazijasimama,’’alieleza.



Katibu wa ushirika huo Ame Suleiman Juma, alisema walichokifanya ndani shamba hilo la migomba, wamepanda na mihogo wastani wa mashina 50, ambayo nayo baadae wanampango wa kuuziana wenyewe.

‘’Huu muhogo umepandwa hivi karibuni, lakini nao kama utazaa vyema, tunaweza kujipatia wastani wa shilingi 100,000, kwani shina moja ni kati ya shilingi 1,500 hadi shilingi 2,000 hutegemea na mzao ulivyo,’’alifafanua.

Hata hivyo Katib huyo, alieleza kuwa, mbali na kilimo cha migomba na mihogo, ushirika wao unajishughulisha na kilimo cha mchicha na bilingani, ingawa changamoto katika eneo, hilo ni maji.

‘’Inatubidi tubebe maji kwa kichwa, kutoka kilipo chanzo hadi kwenye kilimo chetu, jambo ambalo wakati mwingine huongezeka gharama, kwa kule kuwalipa watu wa nje,’’alifafanua.

Mshikafedha wa ushirika huo Moza Salim Mohamed, alieleza kuwa kwenye kilimo cha mboga wameshavuna misimu saba, ambayo yote baada ya kutoa gharama, wamejipatia shilingi 100,000.

Alisema mavuno huwa mabaya, kutokana na changamoto kadhaa ikiwemo, ukosefu wa maji ya uhakika, utaalamu mdogo, ukosefu wa mbole hasa ya kuulia wadudu, ambao hupendelea kushambulia micheo yao.



‘’Tulianzia na mtaji wa shilingi 90,000 kwa mara ya kwanza, zilizotumika kwa ununuzi wa mbegu za mchicha, bilingani, mbolea, upigishaji matuta, na kwa mara ya kwanza tulipata faidi shilingi 20,000 pekee,’’alifafanua.

Akizungumzia kuhusu soko, alisema wateja wa kwanza ni wanachama wenyewe, familia zao, majirani na kisha bidhaa inayobakia huirandisha kijijini kwao, na hubahatika kununuliwa yote.

Mwanachama wa ushirika huo Asha Suleiman Hamad na mwenzake Fatma Mohamed Kassim, walisema kwa sasa maisha yao yamebadilika kiasi, kwa kule kuwa na uhakika fedha japo ndogo.

‘’Maana pamoja na changamoto zote hizo, lakini tunazo fedha kiasi kama akiba, na ushirika unaendelea kubuni miradi mingine, sasa unapopata changamoto ya kimaisha, kwa sasa tunajua wapi tuelekee tofauti na zamani,’’walisema.

Ushirika huo wa ‘tudumishe maendeleo’ uliopo kijiji cha Misooni shehia ya Shungi, wilaya ya Chake chake, ambao una wanachama saba, wakiwa wanawake watano na wanaume wawili, ulianza mwaka 2022, unajishughulisha na kilimo cha mchicha, bilingani, migomba na mihogo.

                 Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch