Skip to main content

MRADI WA VIUNGO ZANZIBAR WAONYESHA NJIA WANAWAKE, VIJANA

 




Na Nafda Hindi, Zanzibar@@@@

Ikiwa  dunia inaadhimisha siku ya wanawake, ambayo husherehekewa kila mwaka ifikapo tarehe 08 March yenye mnasaba ya kuonesha mafanikio ya kijamii, kiuchumi, kiutamaduni na kisiasa huku ikitetea usawa wa kijinsia.

Katika siku hii ya wanawake, ikiwa na kauli mbiu ya mwaka huu “Wekeza kwa wanawake, harakisha maendeleo”.

 Kwa muktadha huo ikiwa na maana pana kuwekeza nguvu kwa mwanamke kunaharakisha maendeleo kwa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa Ujumla, na kwa kukazia kauli hiyo, hata Viongozi wa dini ya Kiislam katika hadithi za Mtume Muhammad (S W) inasema “Ukifundisha mwanamke mmoja ni sawa na kufundisha wanawake kumi.

Kufuatia siku hii hiyo adhimu kwa wanawake TAMWA, ZANZIBAR hawako nyuma katika kuhakikisha wanatumia nafasi hiyo ili kumkombowa mwanamke kiuchumi kwa kuwa na uwezo wa kujitegemea na kutunza familia.



Kupitia MRADI wa VIUNGO wenye lengo la kuwainuwa wanawake kiuchumi TAMWA, ZANZIBAR walifanya ziara ya siku moja kutembelea wanufaika wa mradi huo wakiambatana na Ugeni kutoka Shirika la Kimataifa linalojishughulisha na masuala ya ardhi (LANDESA) na kuona harakati mbali mbali zinazofanywa na wanawake wa Zanzibar kwa lengo la kujikwamuwa kiuchumi.

Aviwe Songoro ni (40) mkaazi wa Kizimbani, Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja ni  mmoja kati ya wanufaika wa mradi huo anasema kupitia kilimo amesomesha watoto wake watatu,  ngazi ya Shahada ya kwanza na tayari wameajiriwa Serikalini, wawili Wizara ya Afya na mmoja Wizara ya Kilimo ambapo kwa sasa mama huyo anamiliki nyumba ya kuishi ya kudumu.

“Watoto wangu wanakula, wanavaa na nawalipia ada ya school na madrasa  kupitia shughuli zangu za kilimo,” Aviwe Songoro.




Nae Mwanashamba Ahmed (42) Mkaazi wa Kizimbzni ni mkulima anaejishughuliha na kilimo cha Vanila, Hiliki, Pili pili Manga, Karafuu, Shoki Shoki na Doriani amesema  ameanza kupata mafanikio kama vile kusomesha watoto watatu ngazi ya Shahada ya kwanza, wawili wamesoma fani ya Madawa(Phamacy) ambapo mmoja tayari muajiriwa wa Serikali na mmoja amesomea Shahada ya kwanza ya Uhandisi.

“Mimi nina watoto (4) mama mimi na baba ni mimi mwenyewe (Single Mother)  nawalisha, nawasomesha na mahitaji yote ya msingi wanategemea kutoka kwangu na ninawahudumia kupitia harakati zangu za kilimo,” Mwashamba.

Nae Rehema John (43) Mkaazi wa Kijichi Unguja, Wilaya ya Magharibi “A” anaelima Viungo mbali mbali kama vile Vanila, Karafuu, Hiliki na Mdalasini  amesema amejenga nyumba ya kuishi ya kisasa ikiwa na miundo mbinu ya maji na umeme, na anazalisha mafuta mazuri (perfume) yenye harufu ya mdalasini, mlangi langi na karafuu na kuingiza kipato kinachomsaidia kujikimu pamoja na familia.

Kikundi cha Vanila Growing Group kutoka Donge, Mkoa wa kaskazini Unguja kinachojishugulisha na kilimo cha viungo (spice) wameweza kubadilisha mitazamo ya baadhi ya wanaume na jamii kuona kwamba mwanamke hawezi kujishughlisha na kuafanya kazi ya kujiingizia kipato.

“Mwanamke ana haki sawa kama mwanamme kupata elimu, kufanya kazi na kujiingizia kipato ila kuna baadhi ya wanaume wana mawazo mgando ya kuwabana wake zao na watoto wa kike kutokufanya kazi, hilo si jambo jema lazima tubadilike,” Mwanaushirika.

Mratibu wa Mradi wa Shirika la Kimataifa linalojishughulisha na masuala ya Ardhi (LANDESA) Susan Waruhiu amesema ipo haja kwa wanawake na watoto wa kike kujiamini katika kutekeleza majukumu yao ili kutimiza ndoto za maisha yao.

“ Wanawake ni watu wenye akili watakapojiheshimu na kuiamini watafika mbali katika kutimiza malengo yao, hivyo wasikubali kuwekwa nyuma,” Susan Afisa Landesa.

Mapema Mkurugenzi Muhamasishaji kutoka Shirika la Kimatifa linalojishughulisha na masuala ya Ardhi Barani Afrika (LANDESA) Dk  Monica Mhoja amesema wanawake waweke mbele Zaidi vipau mbele vyao kama vile kujifunza, kujiheshimu na kujiamini kwa lengo la kuleta maendeleo na kutokubali kukatishwa tamaa.

Aidha Afisa kutoka LANDESA Kylie Palzer amewasisitiza wanawake kuchangamkia fursa na kupambania kugombea nafasi mbali mbali za Uongozi kuanzia ngazi ya familia, jimbo na hata Taifa.



Afisa Mkuu wa Zone, MRADI wa VIUNGO kutoka TAMWA, Zanzibar Sabrina Mwintanga amesema wanatoa mafunzo mbali mbali ya kuwajengea uwezo wanawake pamoja na vijana kujiekeza katika sekta ya kilimo iliodharauliwa kwa muda mrefu kwa lengo la kulima kilimo cha biashara badala ya chakula pekee na kujipatia kipato.

 Ziara hiyo ya Siku moja iliyoratibiwa na TAMWA, Zanzibar kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa linalojishughulisha na masuala ya ardhi (LANDESA) iliwatembelea wanufaika wa MRADI wa VIUNGO kutoka maeneo mbali mbali ya Zanzibar.

MWISHO                

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch