Skip to main content

DK.MWINYI: 'SERIKALI ZINATAMBUA, KULINDA MCHANGO WA WANAWAKE'

 


Serikali zote mbili zinatambua umuhimu na mchango mkubwa unaotolewa na wanawake hapa nchini na zimekuwa zikichukua hatua mbali mbali za kumlinda na kuwawezesha katika hatua za kimaendeleo.

 

Hayo yamesemwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar. HEMED SULEIMAN ABDULLA katika Kongamano la Uwezeshaji wanawake Kiuchumi Zanzibar linaloenda sambamba Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani lililofanyika katika Ukumbi wa Hotel ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar leo.

 

Amesema kuwa  kwa kutambua mchango wa wanawake nchini serikali imeongeza nafasi za wanawake katika vyombo vya maamuzi kutokana na marekebisho ya katiba ya mwaka 2010 kwa kuongeza asilimia ya viti maalum vya wanawake katika Baraza la Wawakilishi kutoka asilimia 30 hadi asilimia 40.

 

Rais Dkt. Mwinyi amesema kuwa Serikali kupitia Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi imetoa mafunzo mbali mbali kwa wajasiriamali wapatao 5,231 ambao kati ya hao 3,581 ni wanawake sambamba na kutoa mikopo zaidi ya Bilioni 29 kwa wajasiriamali wakiwemo wanawake kwa lengo la kuwaendeleza kuichumi.

 


Sambamba na hayo Dkt. Mwinyi amesema Serikali inakamilisha kwa hatua za mwisho katika ujenzi wa masoko ya kisasa ambayo fursa kwa wajasiriamali kufanya biashara zao bila ya usumbufu na kukuza kipato kwa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

 

Hata hivyo Rais wa Zanzibar amesema Serikali itaendelea kushirikiana na mashirika na Taasisi binafsi katika kutoa fursa mbali mbali kwa wanawake na wajasiriamali kwa lengo la kuhakikisha mwanamke anasimama na kuweza kujitegemea katika maisha yake sambamba na kutoa wito kwa wadau wa maendeleo kushirikiana na Chemba ya wanawake wafanya biashara wa Tanzania (TWCC) ili kuipa nguvu na kuwawezesha wanawake wengi zaidi nchini.

 

Mapema Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Riziki Pembe Juma amezishukuru Serikali zote mbili ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzaia inayoongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassan pamoja na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inayoongozwa na Dkt Hussein Ali Mwinyi, kwa juhudi kubwa wanazozichukua katika kuwainua wanawake kiuchumi hapa nchini sambamba na kuwaunganisha katika majukwaa ya wanawake.

 


Amesema kongamano hilo la uwezeshaji wanawake kiuchumi, linakwenda sambamba na maadhimisho ya siku ya Wanawake duniani yakiwa na kauli mbiu ya mwaka huu isemayo, “Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi kwa Maendeleo ya Taifa.” Ikiwa lengo ni lile la kumuendeleza mwanamke.

 

Aidha amesema Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto itaendelea kushirikiana na wadau mbali mbali katika kuhakikisha wanamuinua mwanamke kiuchumi pamoja na kupiga vita vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia dhidi ya wanawake na wanawake na watoto,

 

Naye Mwenyekiti wa Taasisi ya Tanzania Women Chember of Commerce (TWCC) kwa upande wa Zanzibar, Bi Tatu Suleiman Tandu katika risala yao wameishukuru Serikali kwa kazi nzuri inayoendelea kufanyika katika kuukuza Uchumi wa Buluu sekta ambayo inachangia maendeleo ya haraka na jumuishi kwa wanawake ambayo itasaidia kupunguza umasikini, kuboresha maisha ya wananchi na kuimarisha uchumi wa Zanzibar kwa ujumla.

 

Hata hivyo amesema kuwa Serikali ya awamu ya nane imewafanyia mambo mengi yakiwemo kuwapatia huduma wajasiiramali kwa kupata nembo ya ubora kwa gharama nafuu kutoka laki saba hadi elfu 50 ambayo inasaidia kupata masoko ndani na nje ya Zanzibar.


 


Aidha wameiomba Serikali kuangalia upya gharama za Tozo, Ada, pamoja na kodi za uingizaji wa malighafi za uzalishaji wa bidhaa na vifungashio sambamba na kuwaunganiasha na wajasiriamali wa nje ya Tanzania kwa lengo la kujifunza kwa vitendo.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch