Skip to main content

DC. MKOANI: SMZ ITAENDELEA KUYAPA HAKI MAKUNDI YOTE BILA YA UBAGUZI


 


NA ASHA ABDALLA, PEMBA @@@@


SERIKALI ya Mapindunduzi ya Zanzibar ya awamu ya nane chini ya uongozi wa Dk.Hussein Ali Mwinyi, inaendelea kufanya harakati kwa makundi mbalimbali katika kuhakikisha kila mzanzibar anapata haki zote za msingi bila ubaguzi wa rangi, silka na  itikadi  yake .




Ameyasema hayo Mkuu wa wilaya ya Mkowni Khatibu Juma Mjaja kwaniaba ya  Mkuu wa Mkowa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Masoud, wakati alipokua akigawa vifaa maalumu vya  watu wenye uUlemavu wa ngozi  kutoka katika mradi wa ZAHO  huko ukumbi wa Manis[paa ya Mji Chake chake Pemba Machi 9, 2024.

Amesema kuwa serekali inaweza kuwawezesha zaidi watu wenyeulimavu wa ngozi kwa miundombinu mbalimbali kwakupatiwa elimu ,afya bora na hata kupatiwa  mikopo ambayo  itaweza kuwasaidia katika kufanya biashara ndogondogo nakuweza kujikwamua kimaisha.



"Niwaleze wazazi  nawelezi kua nikosa kisheria kuwaficha watu wenye ulemavu au kumdalilisha kwani nawao ni watu kama  watu wengine duniani."alifafanua 



Hata hivyo aliahidi kushirikiana kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa kusini Pemba nao na kutoa wito kwa wazazi wote wajitahidi kuwapatia elimu  watoto wenye ulemavu inayostahiki kwa sababu hao  ndio taifa la baadae .


Kwa upande wake Mkurugenzi  mkuu katika jumuiya ya watu wenye ulemavu wa ngozi ZAHO ambae nimiongoni mwa watu wenye ulemavu Mohamed Rashid Mohamed, alisema kua walemavu wangozi wanazo changamoto mbalimbali, ambazo wanakumbana nazo zikiwemo vifaa vya kutumia ,kudharauliwa na hata kutopata elimu yakutosha kwa watu hao.




Aidha alisema kuwa  walemavu wa ngozi wanakabiliwa na ukosefu wa upatikanaji wa ajira wakati wanapomaliza kusoma kwani wanaonekana kama hawezi kushirikiana na watu katika kufanya kazi ya aina yoyote.



Hata hivyo aliomba serekali kupatiwa eneo lakaribu katika wilaya  ya Chake chake ambalo litawawezesha kujengewa kituo maalumu  cha afya cha watu wenye ulemavu wa ngozi ili waweze kupata huduma kwa wakati bila ya usumbufu wowote.






Nae mwakilishi wa baraza kuu lataifa la watu wenye ulemavu Zanzibar Ayoub Juma Shame alisema kuwa vifaa ambavyo vimetolewa nikwa ajili ya watu wenye ulemavu  pekee na nikosa  kutumia mtu mwengine kwani itakujapelekea kupata madhara.


Afisa wa watu wenye ulemavu katika wilaya ya Chake chake Mwadini Juma Ali alisema kuwa inapokuja kama hizi waweze kuzitumia vizuri kwani jumuiya ya watu wenye ulemavu wa ngozi wamekuja kwa kuwawezesha kimaendeleo zaidi. 


 



Nae mzazi mwenye watoto wenye ulemavu Rashid Mohamed alisema kuwa wazazi wanatakiwa kuwa na ushirikiano mkubwa  na watoto ili weweze kupata  elimu na kuweza kujikwamua kimaisha .



Hatahivyo  aliishukuru taasisi hiyo na viongozi mbalimbali  kwakuweza kushirikiana katika kuwapatia misaada  hii ambayo itaweza  kuwasaidia  watoto hao.



Vifaa hivo vikiwemo lotion, na kofifia vilitolewa na jumuiya mama Maryam  Mwinyi foundation kwa ajili ya kuweza kuwasaidia watoto wenye ulemavu  ili kuepukana na changamoto zinazijitokeza katika  miili yao .

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch