Skip to main content

WANAONYIMWA, KUCHELEWESHEWA MIRATHI PEMBA WAONYESHWA NJIA




NA HAJI NASSOR, PEMBA

MWANASHERIA wa Kamisheni ya Wakfu na Mali ya amana Zanzibar ofisi ya Pemba, Massoud Ali Massoud, amewataka wanawake, wanaonyimwa au kucheleweshewa mirathi, kuitumia Kamisheni hiyo, ili kupata ufumbuzi wa haraka.

Alisema, wanawake wamekuwa ndio waathirika wakubwa, pale familia zinapochelewesha kurithi, ama wakati mwengine kutorithi kabisa, hivyo Kamisheni ni sehemu muhimu kwa waathirika kama hao.

Akizungumza kwenye mkutano uliofanyika Samail Gombani Chake chake, na kuyashirikisha makundi ya wanawake na watu wenye ulemavu, alisema sio busara kwa wanawake kuendelea kukoseshwa haki zao.

Alieleza kuwa, ni wakati sasa kwa jamii za kiislamu kuitumia Kamisheni hiyo, kwa ajili ya kupata ushauri na mamna bora ya kufanya shughuli za mirathi.

‘’Sasa wananchi wanaotaka kufanya mirathi waje ofisini kwetu, maana hata lile tozo, limeshuka kutoka asilimia 5 kabla ya mwaka 2008 na sasa kufikia asilimia 0.25,’’alieleza.

Akatolea mfano kuwa, kwa sasa mirathi yenye thamani ya shilingi milioni 1, gharama inayopaswa kulipwa na wahusika ni shilingi 2500, badala ya shilingi 5,000 ya zamani.

‘’Kwa mujibu wa kanuni yetu, gharama nyingine ni ile ya usafiri kutoka ofisini kwetu, hadi eneo ilipomirathi husika, mabayo hii itamuwajibikia muhusika,’’alieleza.

Hata hivyo, amewakumbusha wanaume, kuacha tabia ya kukalia mirathi kwa muda mrefu, na badala yake watekeleze matakwa ya aya ya Qur-an, inayoharakisha jambo hilo.

Kwa upande wake Mratibu wa Kamisheni hiyo Pemba sheikh Ali Haji Ali, amesema ili ofisi hiyo ifanyekazi, hakunabudi kwa wananchi, kuitumia.



Alisema, serikali kwa maksudi imeshusha gharama ya tozo la urithishaji kutoka asilimia 5 ya mali inayotaka kurithiwa, hadi asilimia 0.25.

Kwa upande wake, Mkuu wa kitengo cha urithi cha Kamisheni hiyo Ali Mbarouk Dadi, alisema kwenye mirathi, wanawake wanayohaki ya kupata mirathi kwa wakati.

‘’Wakati mwengine wapo baadhi ya wanaume, wanapoona warithi wenzake ni wanawake na tena ni wenye ulemavu, huona hawana haki, jambo ambalo sio sahihi,’’alieleza.

Wakichangia mada kwenye mkutano huo, baadhi ya washiriki akiwemo Raya Ali Hamad wa Wete, alisema bado elimu ya matumizi ya ofisi hiyo, iko chini.

Nae Riziki Hadid Rashid, alisitiza haja kwa ofisi hiyo, kufika vijijini na kutoa elimu zaidi kwa wanawake, juu ya haki na nguvu walizonazo kwenye urithi.

‘’Inawezekana wanawake tunaona suala la kupata mirathi yetu kwa wakati, ni kama zawadi kutoka kwenye familia, hivyo kama yatachelewa hatuoni kuwa ni haki kuhimiza,’’alieleza.

Kwa upande wake Raya Khamis Hamad na mwenzake Amina Omar Mohamed, waliipongeza Kamisheni ya Wakfu na Mali ya amana, kwa kufikiria kufanya mkutano huo.

Katika mkutano huo uliojumuisha washiriki 30, mada kadhaa zilijadiliwa ikiwa ni pamoja na ushirikishwaji wa wanawake katika mirathi na wanawake na mirathi. Kamisheni hiyo ipo kwa mujibu wa sheria nambari 2 ya mwaka 2007, ambapo moja ya jukumu lake la msingi ni kuendesha mirathi kwa familia za kiislamu.

                Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch