Skip to main content

WANAWAKE, WATOTO HAWAJAFIKIWA IPASAVYO NA ELIMU YA VVU, UKIMWI



NA ZUHURA JUMA, PEMBA:


………..KUNI ya akiba daima huicheka inayoteketea jikoni……bila ya kujua kuwa ikimaliza nayo itafuata…………..

 Kauli hii ya wazee wa zamani, ndio inayotoa tawira kwa viongozi wa leo ambao huwacheka wanawake na watoto jinsi wanavyokumbwa na changamoto kwenye maambukizi mapya ya VVU na Ukimwi.

Kumbe wanasahau kwamba, watoto ni kuni zilizojikoni na zinateketea na zikimalizika sasa ni zamu ya waliowakuwa wakichekelea na kuwaona watoto na wanawake hawahusiki kupewa taaluma ya ukimwi.

Mimi naamini watoto wa Tanzania, kama walivyo watoto wengine ulimwenguni kote, nao wana haki ya kuzaliwa wakiwa huru bila ya kuwa na VVUna ukimwi.

Watoto hao ambao hutajwa kuwa ndio taifa jipya na viongozi wetu wa kesho, wanaopaswa kulindwa ili kuhakikisha hawaambukizwi na VVU, ambapo matokeo yake hukubwa na magonjwa mengine.

Kwa Tanzania bado suala la elimu ya Ukimwi limekuwa likiguswa kijumla jumla ambapo makundi hatarishi kama ya watoto, wanawake na makundi mengine hayazingatiwi.

Hatari za watoto na wanawake kukumba na VVU na Ukimwi zipo nyingi ikiwa ni pamoja na ile ya kibaologia (kimaumbile) hadi kijamii, kisiasa na kiuchumi.

Sababu hizo na nyengine huwafanya watoto na wanawake kukosa fursa sawa na kuwa na fursa finyu ya kupata taarifa sahihi za maambukizi mapya ya VVU na Ukimwi.

Sababu hii hulifanya kundi hilo, kuwa rahisi kutekwa kimawazo, kiuchumi, kiakili na kusababisha kujiingiiza kwenye vishawishi vya kukumbwana VVU na kisha Ukimwi.

Na ndio maana kwa mujibu wa jarida la wekeza kwa watoto lineleza kuwa, asilimia 50 ya wanawake wenye umri kati ya miaka 20 hadi 49 wameshafanya ngono kwa mara ya kwanza kabla ya kufikia umri wa miaka 18 na asilimia 10 kabla ya kufikia umri wa miaka 15.

Takwimu za sasa zinaonyesha kwamba asilimia ya wanawake wenye kiwango cha ufahamu wa kuhusu VVU na Ukiwmi ni 40 wakati kwa wanaume ni asilimia 47.

Hapa ndipo tunapoona kwamba kundi la wanawake na watoto bado halijaangaliwa ipasavyo juu ya elimu juu ya VVU na Ukimwi nchini Tanzania.

Tunapogusa elimu ya ukimwi kwa watoto wa kike na wanawake pia tunagusa suala la elimu ya kondomu ambayo hutajwa kwamba inaweza kuzuia kwa kiwango fulani maambukizi ya VVU na Ukimwi.

Takwimu zinaonyesha kwamba watoto wa Tanzania ambao hawajaolewa matumizi ya mipira hiyo iko kwa asilimia 55 ingawa changamoto kubwa ni matumizi sahihi na endelevu ya kondomu.


Ali Mbarouk Omar yeye ni Mratibu wa Tume ya Ukimwi Zanzibar ofisi ya Pemba, alisema bado elimu inahitajika zaidi kwa makundi hayo.

“Matumizi ya kondomu kwa anaeamini kwamba yanamzuia na maambukizi ya VVU na Ukimwi, yanahitaji elimu ya kina na hasa juu ya matumizi na uendelevu wake’’,alisema.

Nusu ya maambukizi ya ukimwi ulimwenguni yanawahusu watoto wa kike na hasa kuanzia miaka 20 hadi 24, na ingawa maambukizi zaidi miongoni mwa wanawake ni wale wenye umri kati ya miaka 15 hadi 49, lilieleza jarida hilo.

Kwa vile kundi la wanawake na watoto limekuwa halijawekea mkazo wa kutosha juu ya elimu ya VVU na Ukimwi hata akina mama wenye ujauzito wako hatarini kujifungua watoto waliopata maambukizi.

Na ndio maana kila mwaka wajawazito wenye Ukimwi wapatao 119,000 wanahofiwa kuwa na uwezekano kujifungua watoto wenye UVV moja ya sababu ni kukosa elimu sahihi.

Jarida hilo limetamka kwamba, asilimia 96 ya vituo vya nchi nzima Tanzania, vinavyotoa huduma ya mama na mtoto, vinatoa elimu ya kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto (PMTCT).

Pamoja na hilo, bado kuna mapengo makubwa, maana hadi kufikia mwaka 2011 ni asilimia 64 ya akinamama wajawazito wenye maambukizi ya VVU na asilimia 56 ya watoto wachanga waliokuwa kwenye mazingira ya kuambukizwa Ukimwi walipata huduma ya kurefusha maisha ‘ART’.

Hao walifanikiwa kuzuiwa maambukizi hayo kutoka kwa mama kwenda kwa watoto, ambapo bado elimu ya kina kwa wanawake wasiopata kuolewa na vijana inahitajika.

Asha Mohamed Hassan (40) wa Chakec Chake Pemba ambae anaishi na Virusi vya Ukimwi kwa mwaka sita sasa, ambae alipata mtoto bila ya kuwa na maambukizi, alisema hilo linawezekana kwa asilimi 100.

“Kasoro iliopo hadi kufikia watoto wanazaliwa wakiwa na maambukizi mapya na kudhoofisha kufikia maziro matatu ni ufinyu wa elimu kwa vijana na wanawake’’,alisema.

Afisa elimu na uhamasishaji wa Tume ya Ukimwi Zanzibar ZAC, Sihaba Saadat, alisema kwamba vijana wa kike na wa kiume pamoja na mama wajawazito wakipatiwa elimu endelevu hakutarajiwi kuzaliwwa watoto wenye maambukizi mapya.


“Hatua kama tume ya ukiwmi ya kutoa elimu kwa wanawake, vijana wa kike na kiume tumepiga, maana sasa Zanzibar wapo wanojifungua wakiwa na maambukizi na watoto wao wakiwa huru’’,alisema.

Asha Said Humud wa Wete ambae anaishi na VVU na akiwa mjamzito alisema pamoja na elimu aliokwisha pewa, hana hakika kwamba atapata mtoto alie salama na VVU.

“Unajua hofu yangu ni ya kibinaadamu tu, lakini yupo mwenzangu ambae hajaamua kujitangaaza ingawa alishapewa elimu lakini mtoto wake pia ana VVU’’,alifafanua.

Mwanafunzi wa skuli yasekondari ya Shamiani Khadija Omar Haji alisema hajawahi kupata taalumu ya VVU na Ukimwi, jambo ambalo linampa wasiwasi juu ya maisha yake ya baadae.

Ingawa takriban skuli kadhaa zinavilabu vyanavyozungumzia kuhusu UVV na Ukimwi, lakini mwanafunzi Hamad Mohamed wa skuli ya Kojani, alisema yeye alishapa taaluma ya VVU na Ukimwi ingawa ni kwa muda mfupi.

Hadi mwaka 2014, kisiwa cha Pemba kilikuwa na wanachama watoto 60 wanaoishi na VVU ambapo idadi hiyo ni wale tu ambao kwa njia moja ama neyngine wamesajiliwa kupitia jumuia ya watu wanaoishi na VVU Pemba, ZAPHA+.

Kwa mujibu wa jarida la ‘kwanini kuwekeza kwa watoto?’ linalozungumzia ajenda za watoto, la mwaka 2013, limetamka bayana kwamba, watoto walioko skuli hushindwa kupata elimu sahihi ya VVU na Ukimwi.

 

Kwa mujibu wa tume ya kudhibiti Ukimwi Tanzania, kwenye utafiti wake uliofanya wa kiashirio cha VVUna Ukimwi, Tanzania mwaka 2011/2012 umejumuisha kwa kupima wanawake na wanaume wafikao 20,811.

 

Kwa mujibu wa utafiti huo asilimia 5.1 ya watanzania wenye umri wa miaka 15 hadi 49 wanamaambukizi ya VVU na Ukimwi, ambapo ambukizi hayo ni ya kiwango cha juu miongoni mwa wanawake, kuliko wanaume katika maeneo ya mijini na vijijini.

 

Maambukizi hayo nchini Tanzania yamepungua katika miaka ya hivi karibuni, ambapo kiwango cha hivi karibuni cha VVUna Ukimwi ni asilimia                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                  5.1 ambapo asilimia 6.2 ni wanawake na asilimia 3.8 ni wanaume.

 

 Kwa kulinganisha na utafiti wa kiashirio cha VVU na Ukimwi cha 2007/2008 umebaini maambukizo ya jumla kuwa ni asilimia 5.7 ambapo kwa Mkoa wa Njombe yalionekana kuwa juu na kufikia asilimia 14.8 ambapo kwa wakati huo kiwango cha maambukizo ni cha chini zaidi Pemba ambayo ni chini ya asilimia 1.

Klabu ya waandishi wa habari za Ukimwi Tanzania ‘AJAAT’ imekuwa ikiweka mkazo kwa kuwapa elimu wa kina waandishi wa habari ili kuandika habari za mkundi maalumu.

 

Mkufunzi kwenye mafunzo yaliofanyika hivi karibuni mjini Zanzibar, Chalrse Kayoka, alibainisha kuwa kundi la watoto na wanawake bado halijandikiwa ipasavyo juu ya changamoto wanazokumbana nazo katika kujinga na VVU na Ukimwi.

 

Lakini sera taifa ya kudhibiti Ukimwi Tanzania ya mwaka 2001, ilieleza kuwa, elimu kuhusu hatari ya maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto itatolewa kwa wanawake wote wenye umri wa kuzaa.

 

Sera hiyo ilieleza kuwa, pia kuwapa elimu wanawake ya uwezo wa kiuchumi ili kuwawezesha kuwapatia watoto wao vyakula vyenye virutubisho, sasa hapo ndipo unapogundua kwamba bado kundi la wanawake halijapewa kipaumbele.

 

 

              Mwisho

 

 

 

     

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch