Skip to main content

DK. MWINYI KULIZINDUA TAMASHALA LA UTAMADUNI WA MZANZIBARI PEMBA LEO

 

 




NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi, katika uzinduzi wa tamasha la 31 la utamaduni wa mzanzibari, linalotarajiwa kufanyika leo hii, uwanja wa michezo Gombani Chake chake Pemba.

Uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika, kuanzia majira ya saa 8:00 jioni ya leo, na shamara shamara na maandalizi ya tamasha hilo zitaanzaa mapema, uwanjani hapo.

Akizungumza na mwandishi wa habari, Kamishna wa Utamaduni Zanzibar Dk. Omar Salum Mohamed alisema, maandalizi yote yameshakamilika, kwa ajili ya uzinduzi wa tamasha hilo.

Alisema kuwa, lengo kuu la kuanzishwa tamasha hilo, ni kuhakikisha wazanzibari wanaendelea kukumbushwa, kuelimishwa na kushajiishwa, kuzingatia mila silka, desturi, maadili na mambo mengine yote yanayohusu utamaduni wao.

"Katika tamasha hili hapa kisiwani Pemba mchana wa leo, tunatarajia sana, kuwa mgeni rasmi awe Rais wetu wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi, maana yeye ndio, mpenda utamaduni wa mwanzo ndani ya taifa hili,’’alisema.

Alisema kuwa, katika tamasha hilo, litawakumbusha na litawarithisha vijana, kuendelea kuhifadhi utamaduni wao wa kizanzibari, ili vizazi viendelee kurithi.

Alieleza kuwa, tangu kuanzishwa kwa tamasha hilo kwa mwaka huu ni 31, na matarajio yao, ni kushiriki zaidi ya vikundi 20 vya burudani na ngoma za asili na kuwepo kwa wajasiriamali wa bidhaa za kiutamaduni, wasiopungua 50.


Aliongeza kwa upande wa Pemba katika tamasha hilo, kwa kuanzia litazindulìwa leo hii, na litadumu wastani wa siku nne, na litaendelea kisiwani Unguja  hadi Septemba 25.

Alibainisha kuwa, baada uzinduzi huo uwanja wa michezo Gombani, kesho Septemba 20, wataelekea Wete, ukumbi wa Baraza la Wawakilishi, kwa kupambwa na vikundi mbalimbli vya maulidi ya home, dufu, mnanda na maagizo yenye mnasaba na utamaduni.




 Alisema kuwa, Septemba 21, watahamia wilaya ya Mkoani, ambapo tamasha hilo la 31 la utamaduni wa mzanzibari, litahusisha manahoza 15, wakiwania ushindi wa kwanza, kwa resi za ngalawa.

Kamishna huyo alisema, siku inayofuata baada ya Rais wa Zanzibar kulizindua, litakuwa Pujini, kwa kupambwa na resi za baskeli, zitakazoanzia Kiwani  hadi Pujini.

‘’Niwaombe wananchi kwa hili, wasikubali kuhadithiwa, maana baada ya kuwapokea washindi wa biskeli, uwanja wa mpira wa Pujini, sasa utanogeshwa kwa mchezo wa Ng’ombe,’’alifafanua.

Aidha Kamisha huyo alifahamisha kuwa, mbali na matukio hayo, kuendelea wajasiriamali watakuwa katika kiwanja hicho cha Gombani kwa siku zote, wakiendelea na burudani na sarakasi, kama kawaida, kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 2:00 usiku.

Akizungumzia kuhusu tamasha hilo, alisema kwa upande wa Unguja, litahamia kuzia Septemba 23 hadi 25, ambapo nako shughuli kadhaa, zitafanyika.

Hivyo, amewaomba wasanii, waandishi wa habari, wanafunzi, viongozi wa chama na serikali na wananchi wa Pemba, kuwasili mapema leo uwanja wa Gombani.


Mapema Kaimu Ofisa Mdhamini wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Pemba Sharifa Hamad Shapandu, amezishukuru kamati za maandalizi ya tamasha hilo, kwa kufanikisha shughulizi walizopangiwa.

Alisema kamati hizo, zimekuwa zikifanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na wa pamoja, jambo lililofanikisha uzinduzi huo na shamra shamra zake.

"Zipo kamati zaidi ya tano, zilizozinduliwa kwa ajili ya kufanikisha hafla ya tamasha hilo, ambapo mchana wa leo, kiongozi wetu Dk. Hussein Ali Mwinyi anatarajiwa kulizindua,’’alifafanua.

Hata hivyo amewataka wakuu wa Idara zilizomo ndani ya wizara hiyo, kuwakumbusha watendaji wote wa wizara, kuhudhuria kwa wingi kwenye tamasha hilo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Divisheni ya Utamaduni Pemba Hamad Ali Haji, alisema tamasha hilo litakuwa la aina yake kwa mwaka huu, kwa kuvishirikisha zaidi ya vikundi 10 vya ngoma asili, kutoka Unguja na Pemba.

 

Alisema, tangu kuanzishwa kwa tamasha hilo, kwa mwaka huu, ambalo ni 31, kwa wanachi watakaojitokeza watanufaika na mambo makubwa, ikiwemo resi za ngalawa, Punda, msewe wa zamani na sasa, taarab asilia na mbio za baiskeli.

 

‘’Kwa mwaka huu wizara yetu ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, chini Waziri Riziki Pembe Juma Khamis na Katibu Mkuu Matar Zahor Massoud, tamasha hili, litakuwa la kuvutia na si la kukosa,’’alisisitiza.

 

Tamasha hilo lililoasisiwa mwaka 1995 na Rais mstaafu wa Zanzibar awamu ya tano Dk. Salim Amour Juma na Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, imekuwa likitekeleza agizo hilo la kuendesha tamasha hilo kila mwaka.

Ambapo ujumbe wa mwaka huu unasema ‘UTAMADUNI WETU NDIO URITHI KWA VIZAZI VYETU’

                    MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...