NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@
WIZARA ya Katiba na Sheria ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, imewataka wananchi wa Kisiwa cha Kokota shehia ya Mtambwe
kusini wilaya ya Wete, kuendelea kuzitumia mamlaka za serikali, ili kupata ufumbuzi
wa matatizo yao ya kisheria.
Kauli hiyo imetolewa Juni 6, 2025 na Afisa Habari wa wizara hiyo, Pilly
Nashon wakati akizungumza na wananchi hao, kwenye mkutano wa wazi, wa ufungaji
wa kampeni ya kitaifa ya msaada wa kisheria wa Mama Samia.
Alisema, kwa wananchi hakuna namna ya kuzitumia mamlaka ya serikali
kwa kutafuta haki zao, maana vyenginevyo wanaweza kupewa nyaraka, mfano wa vyeti
vya kuzaliwa visivyohalali.
Alieleza kuwa, nyaraka hizo pamoja na vyeti vya ndoa, hati za
ardhi, vitambulisvyo ya taifa na vile vya ukaazi vya Zanzibar, vitaendelea
kutolewa na mamlaka za serikali na wananchi wanapovihitaji waelekee huko.
‘’Jiepusheni na kuwatumia watu kwa umaarufu wao, mnapohitaji
nyaraka mbali mbali, kama vile vitambulisho vya taifa na vyeti vya kuzaliwa,
maana vyenginevyo watapata vyeti vichafu ‘feck’,’’alieleza.
Katika hatua nyingine Afisa habari huyo, aliwakumbusha wenye
mamlaka serikalini, kuwatumikia wananchi kwa nia ya dhati, ili haki ipatikane.
Alifahamisha kuwa, haki ikipatikana amani na utulivu unapata msingi mkuu wa kuneemeka,
kwa kule wananchi kupata haki zao mbali mbali.
Mapema Wakili wa serikali kutoka Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Pemba, Zubeir Awamu Zubeir aliwakumbusha wananchi hao, kuacha kuzikalia kitako kesi za jinai, na badala yake, wazifikishe mbele ya vyombo vya sheria.
‘’Kesi za jinai kama za udhalilishaji, hazipaswi kufanyiwa sulhu wala wananchi hawana mamlaka ya kupigana faini, maana kufanya hivyo ni kuyanawirisha makosa hayo,’’alifafanua.
Nae Afisa Ustawi wa Jamii wilaya ya Wete, Salma Saleh Hamad,
amewaelekeza wananchi hao, kuendelea kuzisimamia haki za watoto wao, ili
kufuatilia vyeti vyao vya vya kuzaliwa.
Kwa upande upande wake, Mkuu wa Idara ya Upimaji na Ramani Pemba Salim Khamis Haji, aliwasisitiza wananchi, kuepuka kununua na kuuza ardhi kiholela, kwani kunaweza kujitokeza migogoro isiyotarajiwa.
Awali akifungua uzinduzi wa kampeni hiyo, Mkuu wilaya ya Wete
Pemba, Abdalla Rashid Ali, alisema uendelezaji wa kampeni ya msaada wa kisheria
ya Mama Samia Suluh Hassan, ni chachu ya upatikanaji haki kwa wananchi
wasiokuwa na uwezo.
Alisema, wazo la Mama Samia, ni jema ambalo pamoja na kuwasaidia wananchi kutambua haki zao za msingi, ni msingi wa kulinda na kuendelea amani iliyopo.
Kampeni ya kitaifa ya msaada wa kisheria
ya Mama Samia, ni maono yake, baada ya baada kuona makundi ya wanawake, vijana,
watu wenye ulemavu na wanaoishi kwenye mazingira magumu, na kampeni hiyo inatarajiwa
kumaliza Febuari 2026.
Mwisho
Comments
Post a Comment