Skip to main content

‘WANANCHI MICHEWENI ZIRASIMISHENI ARDHI ZENU’


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANANCHI wa shehia za Majenzi, Chamboni, Micheweni, Shumba mjini na Mjini wingwi wilaya ya Micheweni Pemba, wamekumbushwa kuzirasimisha ardhi zao, mara baada ya kuzimiliki, ili kujiepusha na migogoro isiyokuwa ya lazima.

 

Ushauri huo umetolewa leo Juni 1, 2025 na Mkuu wa Idara ya Upimaji na Ramani Pemba, Salim Khamis Haji, alipokuwa akizungumza na wananchi hao, kwenye muendelezo wa kampeni ya kitaifa ya msaada wa kisheria ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mkutano uliofanyika skuli ya Micheweni.

 

Alisema, migogoro kadhaa hujitokeza, kwa wananchi waliowengi kushindwa kuzirasimisha ardhi zao, katika taasisi husika, na kusababisha siuntafahamu baina ya pande moja na nyingine.

 


Alieleza kuwa, njia za kumiliki ardhi kisheria zipo tano ikiwemo kununua, kupewa na serikali, kuvunja pori, kurithi pamoja na kupewa zawadi ingawa kisha kinachofuata ni kuzirasimisha na kupata hati za matumizi.

 

‘’Niwanasihi wananchi wenzangu wa wilaya ya Micheweni, kufanya haraka mara mnapokuwa na ardhi, mhakikishe mnazirasimisha, ili ziongezeke thamani,’’alifafanua.

 

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Idara, aliwakumbusha wananchi hao, kuzitumia siku tisa za kampeni hiyo, kujifunza mambo kadhaa ya kisheria, ili kujua haki na wajibu wao.

 


Kwa upande wake Kadhi wa wilaya ya Micheweni sheikh Mansabu Khamis Omar, amewataka wazazi na walezi, kusimamia haki ya mahari ya watoto wao, kabla ya ndoa kuvunjika.

 

Alieleza kuwa, kumekuwa na wimbi kubwa la vijana kulalamikia juu ya kutomaliziwa mahari yao, jambo ambalo husababisha mifarakano kwa wanandoa na familia zao.

 

‘’Wazazi tunaowajibu wa kuhakikisha, watoto wetu wamaliziwa mahari yao, maana wanapokuja mahakamani kulalamikiana juu ya kesi zao, na haki ya mahari huitaja,’’alifafanua.



 



Mapema Afisa sheria kutoka Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana Pemba, Massoud Ali Massoud aliwakumbusha wananchi, kurithi mali za marehemu mapema, ili kuepusha migogoro inayozuilika.

 

Alieleza kuwa, tayari dini ya kiislamu imeshaelekeza kuwa, miongoni mwa mambo ambayo yanastahili kufanywa haraka, baada ya mtu kufariki pamoja na urithi. 

Baadhi ya wananchi wa shehia hizo, wamesema ujio wa wataalamu hao wa sheria, umesaidia kupata ufafanuzi wa masuala kadhaa waliokuwa wamekwama.

 

Mohamed Shamata Kombo, alisema sasa amepata ufafanuzi wa kesi yake ya ardhi, baada ya kukutana na mtaalamu kutoka Idara ya ramani na upimaji.

 

Nae Hidaya Mjaka Kassim na Halima Mzee Othman, walisema sasa wamepata mwelekeo wa kulipata shamba la eka, ambalo walikuwa hawajui wafanye nini baada ya wazazi wao kufariki.

 

Zaidi ya wananchi 237 wamejitokeza na kupewa elimu, ushauri na msaada wa kisheria kutoka katika shehia hizo tano, kwenye muendelezo wa kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia.

Mwisho.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...