Skip to main content

WANANCHI NJUGUNI, SIZINI, MTEMANI WASIFIA KAMPENI YA KITAIFA YA MAMA SAMIA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

 WANANCHI wa shehia za Mtemani, Njuguni, Sizini na Mtemani wilaya ya Micheweni, wamesifu ujio wa kampeni ya kitaifa ya msaada wa kisheria ya Mama Samia Suluhu Hassan, kwa kupata uwelewa wa mambo kadhaa ya kisheria.

 

Hayo yameyasema leo Juni 2, 2025 kwenye mikutano tofauti ya wazi, iliyofanyika skuli za Sizini na Wingwi, ikiwa ni muendelezo wa kampeni ya kitaifa ya msaada wa kisheria ya Mama Samia Suluh.

 


Juma Haji Juma wa Kilindini, alisema sasa amepata ufahamu wa njia za kufuata, ikiwa atabaini cheti chake au cha mtoto wake, kimekosewa herufi.

 

Nae Aisha Juma Makame wa shehia ya Mtemani, amesema kwa sasa amaelewa njia tano za kuimiliki ardhi, jambo ambalo hapo awali, hakuwa anafahamu.

 

‘’Ilikuwa sielewi kuwa, hata ukivunja pori baada ya miaka kadhaa, kama hajatokea mwenyewe, ardhi hiyo unaweza kuimboa hati za matumizi,’’alieleza.

 



Kwa upande wake Asha Makame Haji, amesema alichofaidika yeye, ni kupata ufahamu juu haki na wajibu wa watoto.

 

‘’Sasa najua kuwa, hata kumpa mtoto jina zuri, kumpeleka masomoni na matibabu ni haki zake kwa mujibu wa sheria,’’alifafanua.

 


Akizungumza kwenye mikutano hiyo, Afisa sheria kutoka ofisi ya Mwanasheria mkuu Pemba, Massoud Nassor Mohamed, alisema sheria ni jambo pana, ingawa kupitia kampeni hiyo, inawasaidia wananchi kupata ufahamu japo mdogo.

 

Afisa Usajili wa Matukio ya Kijamii wilaya ya Micheweni, Almas Massoud Hamad, aliwasisitiza wananchi kutokubali kughilibiwa na baadhi ya watu, wakati wanapotafuta vyeti.

 



‘’Itumieni ofisi yetu kutafuta vyeti vya kuzaliwa, ama kurekebisha makosa, na msiwatumie watu wa nje maana, madhara yake ni makubwa,’’alifafanua.

 

Mapema Mkuu wa Idara ya Upimaji na Ramani Pemba, Salim Khamis Haji, aliwakumbusha wananchi, wanapotaka kurithi ardhi zao kupitia serikalini, ili kupata nyaraka halisi.

 


‘’Unapokwenda Kamisheni ya wakfu kwa ajili ya kurithishwa, faida yake kubwa kwanza ni kupata nyaraka, ambazo ni njia moja wapo ya kujiepusha na migogoro,’’alifafanua.

 

Akifungua mkutano uliofanyika skuli ya Sizini, Sheha wa hiyo Suleiman Shaame Hamad, aliwapongeza watendaji wa Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria kwa kuisimamia kampeni hiyo.

 


‘’Nguvu za utendaji kazi, lazima tuipongeze Idara husika ambayo imesababisha leo, kutufikia katika shehia yangu, na sasa ni wajibu kwa wananchi, kuuliza na kutaka ufafanuzi,’’alifafanua.

 

Kampeni ya kitaifa na msaada wa kisheria ya Mama Samia Suluhu, kwa upande wa wilaya ya Micheweni itaendelea tena kesho katika skuli, madrassa, vyuo na mikutano ya ana kwa ana na wananchi.

mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...