Skip to main content

ZHC: 'TUMEANZA HARAKATI UJENZI WA NYUMBA BORA 72 ''

 




Na Salma Lusangi Zanzibar

Mkurugenzi Shirika la Nyumba Zanzibar (ZHC) Mwanaisha Ali Said amesema ZHC imeanza harakati za ujenzi wa nyumba 72 za makaazi katika eneo la Mombasa kwa Mchina Unguja ili kuwaletea wananchi wa Zanzibar makaazi bora.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na muandishi wa habari hizi, Mkurugenzi huyo amesema harakati za Ujenzi wa nyumba hizo zimeanza Mwezi Machi mwaka huu ambapo shirika hilo limefunga mkataba wa ujenzi na Mkandarasi Simba Developers Ltd. Hivyo Mkandarasi huyo ameanza kazi rasmi.

Mkurugenzi Mwanaisha amesema ujenzi huo utagharimu shilingi za Tanzania bilioni tisa nukta nane (9.8) hadi kumalizika kwake kati ya fedha hizo shilingi bilioni tatu (3) zitatoka katika mfuko wa ZHC na fedha zingine zimetoka katika mfuko wa Serikali kuu kwa maana ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inayoongozwa na Dkt, Hussein Ali Mwinyi.

Alifahamisha kwamba ZHC imekubaliana na Mkandarasi huyo katika kipindi cha muda wa miezi 15 kuanzia Machi 2023 nyumba hizo ziweze kamilika ili shirika liweze kuziuza nyumba hizo kwa wananchi mbalimbali ambao watahitaji kununua.

“Lengo letu ni kuziuza nyumba hizo kwa mwenye kuhitaji, pesa za ujenzi Bilioni tatu tumetoa ZHC na fedha zingine tumepewa na Serikali kuu, nyumba zote zitakua 72 mtu pesa za kwetu”. Alisema Mwanaisha.

Aidha Mkurugenzi Mwanaisha amesema bei ya kuziuza nyumba hizo zitatofautiana kwa sababu kutakuwa na nyumba za vyumba vitatu na zingine vyumba viwili ila kiwango cha bei itapangwa na Serikali baada ya ujenzi kukamilika.



Naye Meneja Mkuu wa kampuni ya Simba Developers Ltd Nurdin Hussein ameishukuru Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kuiamini kampuni yake na kuipadhamana ya kujenga nyumba hizo.

 Hivyo ameahidi kwamba kampuni yake itafanyakazi kwa ufanisi na kwa wakati muwafaka kama walivyokubalina na ZHC.

Kwa Upande wao wananchiwa Zanzibar, akizungumza Bi Asha Ali Kombo (51) Mkaazi wa Fuoni Uwandani ameishukuru Serikali ya awamu ya nane inayoongozwa na Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa uamuzi wa kujenga nyumba mpya kwani ni wazi kwamba Nyumba za Maendeleo Zanzibar ni chache na kongwe hivyo hatua hiyo itasaidia kuondoa malalamiko kwa Shirika la Nyumba Zanzibar.



Naye Omar Ali Issa (48) Mkaazi wa Raha leo ameiomba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuweka mpango wa kuwauzia watu kwa kulipa fedha kidogo kidogo kwa wenye kipato cha chini. 


Alieleza kwamba kutokana na kipato tofauti baadhi ya watu hawataweza kutoa kiwango kikubwa cha fedha kwa pamoja ila kwa kulipa nusu nusu wataweza.

Mwisho

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch