Skip to main content

MZEE MIAKA 70, AFARIKI AKIWA KWENYE FOLENI KUTAKA MAJI YA TIBA MSUKA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

ABRAHMAN Juma Abdalla miaka 70, mkaazi wa kijiji cha Kuyuni wilaya ya Mkoani, ameanguka ghafla na kufariki dunia papo hapo, akiwa kwenye foleni ya kuchukua maji ya kiimani katika bahari ya Msuka, wilaya ya Micheweni kisiwani Pemba.

Itakumbukuwa kua, eneo hilo lilishafukiwa na kupigwa marufuku na serikali, kuwataka wananchi wasiyatumie maji hayo, kwa kutokuwa salama kiafya.

Pamoja na marufuku hiyo, imeabainika kuwa wapo baadhi ya wananchi, wamekuwa wakilitumia eneo hilo na kuchota maji ya kiimani, yanayodaiwa kuponyesha magonjwa na maradhi sugu.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, walisema mpatwa na mauti, alifika shehia ya Msuka mashariki leo Mei 6, mwaka huu majira ya saa 3:00 asubuhi, akitokea kijijini kwao Kuyuni wilaya ya Mkoani.

Walisema, mzee huyo alifika eneo hilo, akikabiliwa na magonjwa sugu, ili kuchukua maji hayo, ambayo alikuwa anaamini, yanaweza kumponyesha magonjwa yake.

Mmoja kati ya mashuda hao Omar Kije Omar alisema, mzee huyo alimpita njiani, akiwa na dumu la lita 20, akielekea kwenye eneo la uchukuaji maji hayo.

‘’Mimi nilikuwa na safari zangu za kwenda kwenye kilimo, lakini alinipita na kuniuliza ikiwa kuna walinzi ama laa katika eneo hilo, na kuelekea kwenye chem chem hiyo,’’alieleza.

Alifafanua kuwa, ghafla akiwa kwenye shughuli zake karibu na eneo hilo, aliona kundi la watu, likiwa limejikusanya eneo karibu na chem chem hiyo, na aliposogea aliona mwili ukiwa umefunikwa.

Sheha wa shehia ya Msuka Mashariki Bakar Ali Bakar, alithibitisha kutokea kwa kifo hicho, na kusema kuwa, alipokea taarifa hizo majira ya saa 5:00 asubuhi ya Mei 6, mwaka huu.

Alisema, baada ya kupokea taarifa hiyo, alifika eneo la tukio na kuukuta mwili wa marehemu, ukiwa umefunikwa na tayari ameshafariki dunia.



‘’Taarifa nilizozipata ni kuwa, marehemu hakufariki wakati wa kuchota maji, bali alikuwa kwenye foleni ya kuelekea kuchota maji hayo, licha ya kuzuiwa na serikali,’’alieleza.

Alieleza kuwa, pamoja na marufuku ya serikali na kufukiwa, lakini bado wastani wa watu kati ya 10 hadi 15 kutoka maeneo mbali mbali, hufika na kuchukua maji hayo.

Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo, na kusema baada ya uchunguzi marehemu, ameshakabidhiwa kwa jamaa zake.



Alisema, marehemu aligundulika kuwa na maradhi ya presha na sukari, na ndio ambayo kutokana na machofu iliyosababisha kifo chake.

‘’Marehemu hakufariki kwenye chem chem ya maji ya kiimani, kama wengine wanavyoeleza, bali alianguka akiwa kwenye foleni ya kwenda kuchukua maji hayo,’’alieleza.

Kamanda huyo aliwataka wananchi, kuheshimu amri halali ya serikali ya kutolitumia eneo hilo la Msuka wilaya ya Micheweni, kutokana na maji hayo, kutokuwa salama.

 April 5, mwaka huu Wizara ya Afya Zanzibar, ilipinga kutumika kwa maji hayo, ikisema sio salama kwa matumizi ya bindamu kwa kule kuwa na vimelea kati ya 220 hadi 1800 kwa kila lita moja ya maji hayo.



Waziri wa wziara hiyo Nassor Ahmed Mazurui, alisema uchunguuzi umebaini kuwa, maji hayo yamebeba kloraida kiasi cha miligramu 149 hadi 2059 kwa kila lita moja ya maji hayo ya chem chem.


Ambapo alisema ,kwa kwaida ya maji ya kunywa, hutakiwa kuwa na kiwango cha chumvi sifuri (0), ingawa hayo yanayodaiwa kuwa ni tiba yamebaba chumvi 2.8 hadi 3.8 ambayo ni hatari kwa binadamu.

Hata hivyo Waziri huyo aliwataka wananchi wote, ambao wameshawahi kuyatumia maji hayo, kufika vituo vya afya mbali mbali kwa ajili ya uchunguuzi wa afya zao.

                 Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch