Skip to main content

TABIA YA KUJICHUKULIA SHERIA MIKONONI, 124 WAPOTEZA MAISHA ZANZIBAR

 

 

 


 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

RIPOTI ya uhalifu na makosa ya usalama barabarani ya Jeshi la Polisi Tanzania ya mwaka 2020, inaonesha kuwa, wapo wananchi 124 wameshauawa, kutokana na watu kujichukulia sheria mikononi visiwani Zanzibar.

Uchunguzi umebainika, hao ni wa kipindi cha miaka 10, kati ya mwaka 2011 hadi mwaka 2020, kwa mikoa mitano pekee ya Zanzibar.

Kwa idadi ya wananchi hao waliouawa, kwa tuhuma za kufanya uhalifu, ni sawa na kila mwaka, wastani wa watu 13 kuuawa visiwani humo katika kipindi hicho.

Kwa idadi hiyo, ilisababisha punguzo la watu kutoka milioni 1,303,569 waliohesabiwa kwenye sensa ya mwaka 2012, hadi kufikia watu milioni 1,303,445.

Watuo hao waliouawa kwa Zanzibar, Mkoa wa Mjini Mgharibi Unguja, ulioongozwa kwa miaka yote hiyo na takwimu hizo haijwahi kushuka.

Imebainika kuwa, mwaka 2011, Zanzibar kuliripotiwa matukio manne (4), mkoa wa Mjini Magharibi pekee, uliripoti matukio matatu (3).

Uchunguzi ukabaini kuwa, mwaka 2015 ambayo Zanzibar ilifanya uchaguzi wake mkuu wa tatu wa vyama vingi, ilikusanya matukio nane (8), mkoa wa Mjini Magharibi uliripoti matukio matatu, ingawa mwaka 2016 kati ya matukio 21, mkoa huo uliripoti matukio 16.

Hali hiyo, iliripotiwa kutisha zaidi katika mwaka 2017, kulikoripotiwa wananchi 26 waliouawa, ambapo kati yao, 18 walikuwa wa mkoa wa Mjini Magharibi.

Kwa mwaka huo mikoa mingine ya iliyoripoti matukio mengi zaidi, ni mkoa wa kusini Unguja kwa matano (5), kusini Pemba matatu (3) na mikoa mengine kukiwa hakuna vifo vilivyoripotiwa.

Mwaka 2019 ulibeba matukio 17, uchunguzi ukaonesha matukio 12 yalikuwa mkoa wa Mjini magharibi pekee, kusini Pemba matukio mawili (2) na mikoa mengine kukiwa na idadi sawa na tukio moja moja.

Hata mwaka 2020, mkoa wa Mjini magharibi, ulikusanya matukio 10, ya mauwaji kwa wananchi kujichukulia sheria mikononi, kati ya matukio yote 15 yaliyoripotiwa. 

NINI CHANZO CHA WANANCHI KUJICHUKULIA SHERIA MIKONONI?

Hafsa Issa Khamis Ali wa Mwanakwerekwe mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, ambae mwaka 2018 kijana wake wa miaka 18, aliauwa kwa tuhuma za wizi wa ndizi nne zenye thamani ya shilingi 200,000 katika soko la Mwanakwerekwe anasema, chanzo ni jamii kukosa maadili.

‘’Wanaotuhumiwa kwa mauwaji wakiwa na hasira ikiwa hawafungwi, lakini wanaotuhumiwa kwa wizi, wanafikishwa mahakamani na wakati mwengine wanafungwa, tabia hiyo itaendelea,’’anasema.




Khadija Mansour Haji wa Kikwajuni wilaya ya Mjini Unguja, ambae mwaka 2019 mume wake alipoteza uhai kwa kushambuliwa na wananchi wakati wa usiku, anasema chanzo ni sheria kuwa lege lege za wanaoua.

‘’Kama sheria za anaeua hazitafanyiwa kazi, basi makosa haya ya wananchi kujichukulia sheria mikononi hayatopungua’’, anasema.

Mohamed Kassim Othman wa Gulioni wilaya ya Mjini Unguja, anasema chanzo ni jamii kukosa uwelewa, juu ya kumfikisha katika vyombo vya sheria mtuhumiwa wa aina yoyote.

Kheir Makame Haji wa Chake chake Pemba, anasema bado jamii haijapata elimu ya athari ya kujichukulia sheria mikononi na ndio maana visa hivyo mkaoni humo viko juu.

Mwanakhamis Muhidin Juma wa Mzingani Mkoani Pemba, anasema mifumo ya haki jinai, kuanzia siku ya kwanza ya kuripotiwa kwa tukio hadi siku ya hukumu ni shida.

VYOMBO VYA ULINZI VINASEMAJE?

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kaskazini Pemba, Kamishna wa Msaidizi wa Polisi Juma Saadi Khamis anasema, chanzo ni ukosefu wa elimu ya sheria husika, kwa wananchi walio wengi.

Jingine anasema inaweza kuwa ni urasimu wa kisheria, uliopo katika vyombo vya sheria, ambao huchukua muda mrefu, bila ya mtuhumiwa kesi yake kumalizika.

‘’Kwa kule wananchi kutokujua sheria, ndio maana mwaka 2021 ndani ya mkoa wangu, kulikuwa na matukio manne (4) ya mauwaji, ingawa kwa mwaka 2022, kulikuwa na tukio moja,’’anafafanua.

Mwanasheria wa serikali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Ali Amour Makame, anasema wananchi wanadhani kujichukulia sheria mikononi, kama vile wanavisaidia vyombo vya ulinzia na usalama kukomesha, jambo ambalo sio sahihi.

‘’Kama jamii inataka kutusaidia, wawafikishe katika vyombo sheria, ambako huko ndio haki ya mtuhumiwa inapatikana na sio kujichukulia sheria mkononi,’’anashauri.

Kamishna wa Polisi Zanzibar ‘CP’ Hamad Khamis Hamad, anasema chanzo ni inawezekana ni mifumo ya haki jinai ilivyo, ikiwemo haki za mtuhumiwa, hasa dhamana.

Chanzo chingine ni mtuhumiwa kuwa anarejea makosa na anapofikishwa mahakamani anashinda kesi, inayochangiwa na wananchi wakati mwengine kutotoa ushahidi.

‘’Kama kuna mtu amefanya uhalifu na kushuhudiwa, lakini baada ya kufikishwa mahakamani wananchi wakishindwa kutoa ushahidi ataachiwa huru,’’anasema.

WANAHARAKATI WA HAKI BINAADAMU

Mkurugenzi wa Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali anasema, kasi ndogo katika vyombo vya sheria, kuyashughulikia makosa ya jinai, ndiko kunakozaa fikra chafu ya kujichukulia sheria.

‘’Elimu ya athari ya kujichukulia sheria mikononi, bado iko chini na ndio maana imekuwa jambo la kawaida, hata mtu akituhumiwa kuchungulia kwenye jengo la jirani anauawa,’’anafafanua.

Aliyekuwa Mratibu wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ Pemba Safia Saleh Sultan, anaona chanzo ni urasimu wa uliopo katika vyombo vya sheria.

Jengine ni ufinyu wa ufahamu kwa jamii, juu ya haki za mathumiwa, jambo ambalo wanadhani kila anayetuhumiwa ana haki ya kuuawa ama kufungwa.

Mratibu wa Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora Tanzania ofisi ya Pemba Suleiman Salim, anasema hata tafiti mbali mbali zinaonesha wavunjifu wakubwa wa haki za binadamu, ni wananchi wenyewe.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wasioona Pemba ‘ZANAB’ Suleiman Manssour anasema, haki inayofikiwa mahakamani ya watuhumiwa kuachiwa huru, ndio chanzo cha wananachi kujichukulia sheria mikononi.

Mjumbe wa Baraza la Wazee mkoa wa Mjini magharibi Haraoub Shein Hassan, anasema uhuru wa kufanya kila mmoja apendavyo bila ya kuchukuliwa hatua, ndio chanzo cha mauwaji hayo.

 VIONGOZI WA DINI

Sheikh Said Ahmad Mohamed, anasema chanzo ni waumini kukosa hofu ya Muumba wao, ambae ameshaahidi adhabu kwa atakayeondoa uhai wa mwengine, kinyume na sheria.

‘’Uislamu unakataza na hautambui, kumuondolea uhai mwengine kwa sababu ya tuhuma ya wizi, kwani sheria ya dini ya kiislamu, imeweka wazi kwa mwizi, ikiwemo kukatwa mkono pindi ushahidi ukikaa vyema.

Mchungaji Samuel Eliyas Maganga ambae ni Mwangalizi wa Makanisa ya Pemba Tanzania Assembles of God ‘TAG’, anasema Kanisa linakataza kujitoa muhanga, kulipiza kisasi na kuua.

‘’Kitabu cha ‘Kutoka’ kwenye milango yake mbali mbali, inakataza moja kwa moja, mtu mmoja kuchukua kazi ya Muumba ya kuondoa roho ya mwengine, kwani huko hakuondoi tatizo,’’alieleza.

KISAIKOLOGIA SABABU ZA WANANCHI KUJICHUKULIA SHERIA MIKONONI

Dokta Ali Yussuf, mtaalam wa saikolojia ya binaadamu, anasema wananchi hufikia uamuzi huo, kutokana na kujirerejea reje kwa makosa kwa mtu mmoja husika, katika maeneo yao.

Jengine ni wananchi kukata tamaa na vyombo vilivyowekwa kwa ajili ya kuwashughulikia wahalifu, hivyo akili zao hukosa imani na kufanya uamuzi wa kuua, ambao sio sahihi.

Daktari wa saikolojia Mtumwa Hija Mzale anasema, uwezo wa akili ya mwanadamu ni kuvumilia kosa la mwanzo, hivyo la pili likitokezea hupenda kujichukulia sheria mwenyewe, ili kukomesha.

‘’Kisaikolojia mwanadamu haridhishwi na kukosewa yeye kisha adabu akaitoa mtu au mamlaka nyingine na ndio maana hasira za wananchi hupenda kujichukulia sheria mikononi,’’anafafanua.

NYARAKA MBALI MBALI

Katiba ya Zanzibar yam waka 1984, kifungu cha 13 kimebainisha kuwa ‘kila mtu anayo haki ya kuwa na hifadhi ya maisha yake kwa mujibu wa sheria’.

Kifungu hicho kifafanua kuwa, ‘kila mtu anayo haki ya kuishi na kupata hifadhi na ni marufuku kuteswa, kuadhibiwa kinyama au adhabu zinazomdhalilisha’.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 Ibara ya 15 ikafafanua kuwa, ‘kila mtu anayo haki ya kuwa huru na kuishi kama mtu huru’.

Mkataba wa haki za binadamu wa mwaka 1948 kuanzia ibara yake ya 3 hadi ya 8, imekataza kwa mtu kuteswa, kuadhibiwa, kwani yuko huru kulindiwa.

Mkataba wa kimataifa wa haki za kiraia na kisiasa wa mwaka 1966, ambao Tanzania uliuridhia mwaka 1976, Ibara ya 1, umeanisha haki ya kuishi, ukamilifu na usalama wa mtu.

 

ATHARI YAKE

Ussi Khamis Haji wa mkoa wa Mjini Magharibi, anasema ni kuendeleza visasi, kati ya familia ya waliouliwa kijana wao na familia ya watuhumiwa wa mauwaji.

Mtumwa Saadi Ibrahim Mwinyi wa Mtambile Mkoani, anasema athari nyingine ni wananchi kupoteza imani na vyombo vya ulinzi na usalama, ambavyo ndio kimbilio lao.

Kamada wa Polisi mkoa wa kusini Pemba Msaidizi wa Kamishna Abdalla Hussein Mussa anasema, ni kuvunjwa Katiba ambazo zinakataza kuondoa uhai wa mtu.

Mratibu wa Tume ya Haki za binadamu na Utawala bora Tanzania ofisi ya Pemba Suleiman Salim, anasema ni kuyachukua mamlaka kisheria ya mahakama, kumpa mtu mwengine kuhukumu.

Mwenyekiti wa Jumuiya mwemvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’ Sifuni Ali Haji, athari inayojitokeza ni kujenga hofu miongoni mwa vijana katika shughuli zao za kila siku.

Sheikh Mohamed Juma Issa, anasema athari nyingine ni kujitia katika makosa ambayo wakati mwengine adhabu yake inaweza kuanza hapa ulimwenguni.

  Jaji Mkuu wa Zanzibar Khamis Ramadhan Abdalla, athari ni vyombo vinavyosimamia haki jinai, kukasimiwa madaraka yake kimakosa ikiwemo mahakama.

‘’Kisheria mahakama ndiyo ambayo inaweza kutoa hukumu ya kifo, kama sheria zilivyo, lakini badala yake sasa, wananchi ndio wamechukua nafasi hiyo jambo ambalo ni kosa,’’anasema.

NINI KIFANYIKE

Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Kamishna Msaidizi Juma Saad Khamis, anashauri elimu itolewa ya athari ya kujichukulia sheria mikononi.

Wananchi Juma Seif Khamis na Mayasa Himid Kassim, wanasema kinga ya kuwa na hasira, baada ya mmoja kumuua mwenzake, iondolewe na badala yake ikibainika watiwe hatiani.

Afisa Sheria kutoka Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar ofisi ya Pemba Bakar Omar Ali, anasema wananchi waelimishwe athari ya matokeo ya kujichukulia sheria mikononi.

Sheha wa shehia ya Wawi Sharifa Waziri Abdalla, anasema vyombo vya ulinzi na usalama, viharakishe upelelezi wa makosa mbali mbali, ili kupunguza hasira kwa wananchi waliotendewa kosa.

Afisa kutoka baraza la vijana wilaya ya Chake chake, Sara Khamis Juma anasema vijana ndio waathirika wakubwa, waanzishiwe mpango maalum, ambao unaweza kuzaa ajira.

Mwanamke ambae muume wake alipoteza uhai kwa tuhma za kuvunja na kuiba eneo la Wete Pemba mwaka 2022, anasema anaeuwa, nae mahakama iondowe uhaki wake.

Hidaya Mjaka Ali mwenye ulemvu wa viungo, anasema lazima sheria ziwekwe ambazo zitaharakisha uendeshaji wa kesi za jinai kwa haraka.

                         Mwisho

 

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch